Wilaya ya Ruangwa wamwambia Rais Samia hakuna changamoto yoyote ya kufanyia kazi

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Rais Samia Suluhu amesema amekuta Ruangwa hali ni tofauti na maeneo mengine ambapo kote alikopita amepokea changamoto nyingi za kwenda kufanyia kazi, lakini Ruangwa wamemwambia hawana changamoto yoyote, Ruangwa wametaja mazuri waliyofanyiwa na Serikali. Rais Samia amewapongeza mkoa wa Lindi na wilaya ya Ruangwa kwa maendeleo makubwa.

Rais Samia ameahidi kumtunza waziri mkuu kwa kupeleka maendeleo zaidi Ruangwa kutokana wadhfa wake kuwa na kazi nyingi. Rais Samia amesisitiza lazima Serikali ipeleke maendeleo Rungwa.

Rais Samia Suluhu ameanza ziara yake ya kikazi mkoani Lindi na leo Septemba 18, 2023 amehutubia wilayani Ruangwa baada ya kumaliza ziara mkoani Mtwara.

Your browser is not able to display this video.
 
Mbunge wa huko kuna kitu anatafuta.
 
Hakuna sehemu Dunia nzima ambayo haina changamoto.


Tusimbishie Rais jamani.

Tukafanye utafiti ikiwezekana twendeni Ruangwa tukathibitishe pengine kweli kuna pepo hapa hapa Tanzania na hatuna taarifa.

Ama pengine wananchi wa Ruangwa wame-evolve sana kiasi wao tafsiri ya changamoto ni tofauti na ya dunia nzima.

Mpaka Waziri Majaliwa anawekewa β€œmsaidizi” ndani ya ofisi yake yenye kiti kimoja tu, Ruangwa people might be special.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…