Wito wangu kwa DGIS na Taasisi yako: Msipomtumia Tundu Lissu kupata Katiba Mpya na Bora sasa, mtajuta milele.

Halafu kuna takataka na majizi maccm yanakwambia lissu ni kichaa aisee ila yanasahau kuna yule bwana magufuri aliyetaka jimiliksha taifa hli kama vicoba yeye alijiita kichaa kbs
Huu uzi sio wa matusi, jirekebishe kama huwezi kutoa maoni bora ukae kimya. Uwaachie watu wanaojielewa. Sawa?
 
Hapana
Tunaweza sana kutoka.

Tukiweka mifumo mizuri ya utawala na kuzuia Rushwa na Ufisadi for almost 90 percent tu tutaweza.

Tunachopaswa ni kutumia vizuri akili zetu tulizopewa na Mungu.
 
Kwa jinsi unavyomhusudu km Mungu hutaona mapungufu yake. Acha siasa ya aina hiyo, huo ni unazi
 
Muhimu watangulize utaifa na maslahi ya Taifa yatunzwe kwa vizazi vijavyo na Katiba nzuri Ndiyo itapelekea kutunza rasilimali za Taifa.
Lakini wakitanguliza uchama na kufikiria maslahi yao ya uteuzi na ajira za watoto wao shida itazidi kuwa kubwa na watalaaniwa na vizazi vyao.
Na Mungu ataaadhibu.
 
Wawiwe kuona haki i kitokewa kila mahala kivitendo.
Mwenyezi Mungu anapendezwa na utolewaji wa haki na sio dhuruma, ghiliba, ufisadi, wizi udhalimu, mauaji, uonevu n.k.
Na Mungu haishii kuchukizwa tu lakini huadhibu pia na adhabu yake huwa ni kubwa kuliko ya mwanadamu kama mwenyewe alivyo mkubwa sana kuliko mwanadamu bila kujali chochote yakiwepo madaraka.
Mfano utakuta adhabu ya laana inaenda kula vizazi vya mtu cha kwanza hadi cha 4 hata cha 7.
Kwani Imeandikwa; “ nawapatiliza wana uovu wa baba zao kizazi cha kwanza hata cha nne”
Bali nawarehemu maelfu kwa maelfu ya wale wanipendao kizazi cha kwanza haya cha nne.
Na maana ya kumpenda Mungu ni kuishi kwa kufuata na kuzingatia alichoagiza.
Mfano alisema acha mabaya uache, Fanya mema na haki ufanye ktk kufanya kazi kwako na kuishi kwako hicho ndicho kipimo cha kumpenda Mungu.
Imeandikwa; “ mkinipenda mtazishika amri zangu nami nitakuwa pamoja nanyi siku zote.
 
Aisee! Asante! Mungu akubariki sana!
 
Kweli kabisa!
Wana nafasi nzuri sana ya kuionyosha hii nchi na kuifanya iwe salama na imara kiuchumi kwa miaka mingi ijayo kupitia kuipatia Katiba Mpya iliyo bora kipindi hiki.

Wasipomtumia Tundu Lissu kufanikisha hili. Kwa namna tunavyozidi kuwa na watawala wa hovyo kila kukicha, future yetu iko mashakani sana.
 
Uchama na Maslahi binafsi ndo mambo yanayokuza sana Rushwa na Ufisadi nchini.
 
Tuna taasisi ya ajabu sana, hawajui kusoma nyakati ni muda gani wawe catalyst au reactor. Hawajifunzi kinachofanyika Sudan zote kusini na kaskazini.
Wananchi wanalalamikia dominant ya watu wachache kwenye nchi wako kimya tu. Siku yakitokea yake ya Brotherhood kule Egypt ndipo wataanza kuumiza vichwa.
TISS wajibikeni au mnasubiri muwajibishwe wananchi?
 
Wakifanya maamuzi sahihi sasa, wataisaidia hata hiyo taasisi yao. Wakimtumia Lissu vizuri sasa na tukapata Katiba Mpya na Bora, hii itakuwa moja ya mafanikio yao makubwa sana katika kulitengeneza Taifa hili kuwa imara na salama kwa miaka mingi ijayo.

Historia itawakumbuka milele
 
Asante Mungu pia kwa kutukirimia WEWE ambaye unaona ambayo wengine hawayaoni. Kupitia bandiko hili umedeclare nia yako njema kwa taifa hili. Ubarikiwe zaidi🙏
 
Asante Mungu pia kwa kutukurimia WEWE ambaye unaona ambayo wengine hawayaoni. Kupitia bandiko hili umedeclare nia yako njema kwa taifa hili. Ubarikiwe zaidi🙏
Hatuna Tanzania ingine zaidi ya hii. Tufanye kila liwezekanalo tuisadie Tanzania yetu.
 
Problem kuna political element juu yake, how can he do that?
Akiamua na Taasisi yake wanaweza.

The backbone ya CCM ni wao na wakiamua leo hii kusema wanainyoosha hii nchi watainyosha kweli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…