Wizara kuweka gharama za kulipia nguzo 1,2,3 = Tsh 27000/= linaleta kero kubwa, TANESCO hawana uwezo wa kufidia punguzo hilo

Yaani unalipia nguzo siku ukiondoka kwani unaondoka nayo (au nguzo ni mali yao) wenyewe waconcetrate kusambaza umeme pote sababu ndio kupata wateja wenyewe hayo mambo ya kulipia miundombinu ambayo sio yako ni kuleta ukakasi (ukizingatia pia kila mwananchi akilipia Luku anakatwa REA)

Kama ni kulipia hayo makato basi siku mteja akianza kulipia luku arudishiwe hizo pesa alizotoa
 
Hasara inatoka wapi wakati ukinunua umeme unalipishwa Kodi ya Rea,

Anayepata hasara ni sisi wananchi siyo Tanesco.
 
Kumbukeni hizo nguzo mnazolalamika siku zikiharibika utabadilishwa mpya bila ghafama yoyote kadhalika mita pia ikiharibika utabadilishiwa mpya bure transfoma likiharibika tanesco wanafunga jingine bure wala huchangii
 
Mnaosema huduma iwe bure hamjui jinsi ilivyongumu kupata umeme tanesco kwa hiyo 27000/=, ni Bora ulipie million 1 upate umeme ndani ya mwezi kuliko kulipia 27000 uupate baada ya miaka miwili,
Ni Watanzania wangapi wana shs 1,000,000/=kulipa nguzo za umeme, tembea uone.
 
Hakuna gharama za kulipia nguzo. Ukilipia nguzo maana yake upewe nguzo tu na usipate umeme. Sema gharama za kuwekewa umeme ndani ya mita 70 mpaka 120.
"Kulipia nguzo" ni lugha tu iliyozoeleka ikimaanisha malipo ya umeme nje ya zile mita 30 zilizoainishwa. Kusema nguzo inamaanisha na viambata vyote vinavyokamilisha hiyo huduma.
 
Sekta binafsi iruhusiwe kushindana na TANESCO kusambaza umeme. Bila kufanya hivyo TANESCO hawatakaa wazinduke kutoka usingizini
 
Acha uongo wako wewe!

Umeme wa 27,000 ni wa REA ambao gharama zake zinabebwa na selikali!

Sehemu ambayo hukuna mradi wa REA ukitaka umeme na nguzo laki 5 inakuhusu.
Serikali ipi sasa inayobeba hizo gharama? Kipi ni chanzo kikubwa cha mapato cha REA kwa kuanzia?
 
Kwani tanesco inamilikiwa na nani?
 
Hilo shirika Ni mzigo tu...nawaza tu ...ingependeza LIKABINAFSISHWA...maana hakuna namna Sasa!!!ah!
Aisee ujui unachokisema mzee hilo shirika likibinafishiwa, Umeme hautakuwa huduma tena bali anasa hamtaweza ku afford kuanzia new connection mpaka monthly bill acha liendelee kuwa state owned kwa 100% mana hata hio connection ya mjini ya 321K bila nguzo ni cheap sana sana achilia mbali ile ya vijijini 27k Yani hizo sio bei realistic kabisa ndo mana tanesco anajiendesha kwa hasara na serikali ndio inali fund ili wananchi mpewe service nkikupa breakdown ya new connection hakika utafunga mdomo
 
3% unayolipa haiwezi kutosha kufund izo project za Rea mana nyingine zipo remotely sana kiasi kwamba mpaka wakandarasi hukimbia na contract kupewa JKT, Misaada ya wafadhili sio reliable
 
3% unayolipa haiwezi kutosha kufund izo project za Rea mana nyingine zipo remotely sana kiasi kwamba mpaka wakandarasi hukimbia na contract kupewa JKT, Misaada ya wafadhili sio reliable
Mbona ndio zinafund sasa hivi?ni vijiji vichache sana vimebaki navyo vitaisha, ni suala la muda tuu
 
Serikali ipi sasa inayobeba hizo gharama? Kipi ni chanzo kikubwa cha mapato cha REA kwa kuanzia?
Ukinunua LUKU kuna percent unakatwa kwa ajili ya REA, pia kuna hela zinatolewa na wafadhili kwa ajili ya REA.

Au wewe unahisi hela za umeme wa REA anatoa nani?
 
Sekta binafsi iruhusiwe kushindana na TANESCO kusambaza umeme. Bila kufanya hivyo TANESCO hawatakaa wazinduke kutoka usingizini
Sector binafsi ikiingia kwenye iyo industry umeme hautakuwa bei rahisi tena imagine mtu anakuwa connected kwa 27k kwa breakdown hii
-Survyed Bure
-Transport cost Bure
-Labour charge bure
-Material cost bure

Mteja anacholipa ni Value added Tax VAT tu 27K bado hapo akipata emergency hata iwe 60kM atafatwa na kuhudumiwa bure kabisa hakuna Monthly service charge ambapo awali ilikuwepo ila serikali ikaifuta ilikuwa 6k bado mteja huyo huyo anauziwa umeme kwa 100 per unit? Can you imagine ni mwekezaji gani anaweza kufanya iyo biashara even if Rea iko contributed na Watumiaji wote wa umeme kwa 3% kwa kila purchase ila still serikali inabeba mzigo mkubwa sana na inafanya poa katika hili
 
Ukinunua LUKU kuna percent unakatwa kwa ajili ya REA, pia kuna hela zinatolewa na wafadhili kwa ajili ya REA.

Au wewe unahisi hela za umeme wa REA anatoa nani?
Umeme wa REA
Watu wanataka waunganishiwe umeme dezo eti
Hakuna huduma kama hiyo duniani

Ova
 
Kuna unafuu gani kulipa 27K ya nguzo ukae miaka kusubiri umeme?!

Kinachotakiwa sekta binafsi na wao waruhusiwe kusambaza umeme kwa watumiaji wa mwisho huku TANESCO nayo ikiendelea kama kawaida na biashara yake, wananchi wao wachague wachukue umeme kwa kampuni ipi na kwa gharama gani.
 
Sekta binafsi iruhusiwe kushindana na TANESCO kusambaza umeme. Bila kufanya hivyo TANESCO hawatakaa wazinduke kutoka usingizini
Hata huyo mtu binafsi atalipisha gharama ya kuunganishiwa umeme

Ova
 
Sawa, sekta binafsi waruhusiwe sasa.

Tatizo lilipo hapa sio kulipia, tatizo ni watu wanalipia umeme halafu wanasubiri mwaka mzima kuunganishwa huo umeme.Urasimu wa aina hiyo hauwezi kutokea kama kampuni binafsi ingekuwa inasambaza umeme.
Hata huyo mtu binafsi atalipisha gharama ya kuunganishiwa umeme

Ova
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…