Yaliyojiri kesi ya Mbowe leo Novemba 05, 2021: Inspector Mahita Mohamed atoa ushahidi

Yaliyojiri kesi ya Mbowe leo Novemba 05, 2021: Inspector Mahita Mohamed atoa ushahidi

Ni wahuni tu ndiyo wamo humo na sababu ya wao kuchukiwa sana na Watanzania wengi ni tabia yao mbovu iliyokithiri ya kubambikia watu kesi FEKI.

Kumbe huyu afande Jumanne mwenyewe ameshawahi kusimamishwa kaz kwa kumbambikia mtu meno ya tembo, jeshi letu la polisi limeoza imagine huyo ndio mkubwa sijui kwa walio chini yake wakoje.
 
Kibatala; unafahamu afande jumanne amesi amishwa kazi kwa kumbambikia mtu Meno ya tembo kwenye mzinga wa nyuki na yeye ni miongoni mwa mashahidi kwenye hii kesi?

Shahidi; sifahamu Kama kasimamishwa kazi

Kibatala; unafahamu kuwa afande jumanne anatuhumiwa kumbambikia mtu Meno ya tembo kwenye mzinga wa nyuki?

Shahidi; nafahamu

Makubwa!!!!!!
 
Kumbe huyu afande Jumanne mwenyewe ameshawahi kusimamishwa kaz kwa kumbambikia mtu meno ya tembo, jeshi letu la polisi limeoza imagine huyo ndio mkubwa sijui kwa walio chini yake wakoje.
ASP Bageni alihukumiwa kunyongwa hadi kufa na Mahakama Kuu kwa kuwapora na kuwaua wale ndugu wafanyabiashara wa madini toka Morogoro na dereva taxi; alipokata rufaa the Supreme Court ikakazia hukumu; sina hakika kama alishalishwa kitanzi au bado. Hao ndio mabosi wa jeshi la polisi; imagine huko chini hao "nyoka" wanaosaka senti za ku-brush viatu wakoje!
 
Kibatala; unafahamu afande jumanne amesi amishwa kazi kwa kumbambikia mtu Meno ya tembo kwenye mzinga wa nyuki na yeye ni miongoni mwa mashahidi kwenye hii kesi?...
😁😁😁😁 Hawa jamaa wanajiaibisha aisee! Hii kesi ya Profesa wa watu mstaafu kuwekewa meno ya tembo nyumbani kwake halafu wakamtishia kumpeleka polisi, au atoe milioni 70 ili wamalizane, uzi wake ulikuwemo humu jukwaani, na pia vyombo vya habari vili irusha hii taarifa! Kumbe na Jumanne naye alikuwemo!!

Kwa hali hii sasa mbona ukweli uko wazi kabisa! Polisi ni wabambikiaji wa kesi.
 
Kibatala; hati ya mashtaka inataja kudhuru viongozi, hao viongozi ni akina nani

Shahidi; sabaya

Kibatala; mwingine?

Shahidi; sabaya

Kibatala; sabaya umemtaja na walikua wengi tutajie mwingine

Shahidi; sabaya

Hii sasa kali.
 
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16] Hawa jamaa wanajiaibisha aisee! Hii kesi ya Profesa wa watu mstaafu kuwekewa meno ya tembo nyumbani kwake, au atoe milioni 70 uzi wake ulikuwemo humu jukwaani! Kumbe na Jumanne naye alikuwemo!!

Kwa hali hii sasa mbona ukweli uko wazi kabisa! Polisi ni wabambikiaji wa kesi.
Na kibatala amempa break akapumue kidogo amemwabia anayo maswali mengi Sana kwake.
 
Yule Shahidi Afande Jumanne amesimamishwa kazi kwa kumuwekea mzee huyu meno ya Tembo na kuchukua milioni 100 zake.

2754997_Ar1.jpg


2754998_Ar2.jpg
 
Shahidi namba 7 anaelekezwa na upande wa Jamhuri kuileza mahakama
  1. Kuwepo kwa watu waliokuwa na mpango wa kufanya ugaidi
  2. Kaeleza pia walivyowakamata.
  3. Kuwatambua na kawaonyesha wahusika.




Wakili wa Serikali: Kwenye Briefing Mlielezwa Mambo gani

Shahidi: Afande Kingai alituambia Kuwa amepewa Maelekezo ya Kuunda Kikosi Maalum, na Kikosi Hilo Ndiyo MIMI, ASP Jumanne, Goodluck, Francis, na PC Aziz Kwamba Kuna Kikundi Cha Watu kinataka Kufanya Vitendo Vya kigaidi

Wakili wa Serikali: Vitendo gani hivyo Shahidi: Kuwa Kikundi hicho kinataka Kufanya Vitendo Vya Kigaidi Mikoa Mbalimbali ikiwemo Arusha, Kilimanjaro, Dar es Salaam, Mwanza na Mbeya Uhalifu walipokuwa wanataka Kufanya ni KUCHOMA Vituo Vya Mafuta, Kuzuia Barabara, Kukata Miti, kuwadhuru Viongozi Wa Serikali Ikiwemo aliyekuwa Mkuu wa Wilaya Hai, Ole Lengai Sabaya Maandamano ambayo haya Ukomo, na Pia alitueleza Washirika ambao wanataka Kufanya Matukio hayo

Wakili wa Serikali: Aliwataja akina nani

Shahidi: Afande Kingai alisema Mpango huo ulikuwa unaratibiwa na Mheshimiwa Freeman Mbowe

Shahidi: alisema Wahalifu Wengine wapo Moshi, Kwa hiyo tuwazuie Twende Mkoani Kilimanjaro Wilaya Ya Moshi Alisema Kuna watuhumiwa 4 ambao walikuwa Moshi

Wakili wa Serikali: Wakina nani

Shahidi: Walikuwa wanakamilisha Mpango wa kwenda Kumdhuru aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya

Wakili wa Serikali: Kingai alisema Madhumuni ya Mpango yote ni nini

Shahidi: Kuleta Taharuki, Ili Nchi is iweze Kutawalika Tunapoelekea Kwenye Uchaguzi Akasema tuzuie Matendo hayo, Ili Nchi eindelee Kuwa Salama

Wakili wa Serikali: Mengine

Shahidi: Hayo tu kwenye Briefing


Sioni maswali ya Kibatala na wenzake yakielekea kupangua hayo

Tulia ndugu...

Acha pre - emptive..

Mahojiano yanaendelea...

Hebu msikilize ndugu yako hapa...
Screenshot_20211105-140038.png
Screenshot_20211105-135853.png
Screenshot_20211105-135502.png
Screenshot_20211105-135454.png
Screenshot_20211105-135532.png
Screenshot_20211105-135718.png
Screenshot_20211105-135628.png
 
Kibatala; hati ya mashtaka inataja kudhuru viongozi, hao viongozi ni akina nani

Shahidi; sabaya

Kibatala; mwingine?

Shahidi; sabaya

Kibatala; sabaya umemtaja na walikua wengi tutajie mwingine

Shahidi; sabaya

Hii sasa kali.
... hao walioandika hati ya mashtaka na wanaotoa ushahidi mahakamani kwamba hata Kiswahili kinawashinda? Kuwadhuru viongozi wa Serikali; sasa taja hao viongozi; Sabaya; wengine? Sabaya! Kwamba Sabaya anatajwa kwa wingi amekuwa Mungu?

Bwana Mungu na akasema, "tumfanye mtu kwa mfano wetu ...". Kwanini hati ya mashtaka na ushahidi visingetaja tu kiongozi wa serikali badala ya viongozi! Another mistake on jamhuri's side! You can see the ill motives behind thise case!
 
Back
Top Bottom