Uchaguzi 2020 Yaliyojiri kwenye Uzinduzi wa Kampeni za Mgombea Urais kupitia CHADEMA Tundu Lissu katika viwanja vya Zakheim Mbagala, TBC Wafukuzwa

Hawafai hawa,yaani Magufuli akisemwa tu wanakata,halafu picha zao wala hawazungushi Camera.Camera imebase kwenye jukwaa tu.Tunataka tuone na Nyomi bwana.Magufuli siyo malaika bwana ,akisemwa mnataka matangazo.SHAME ON YOU TBCMAGUFULI.
Kwani mpaka mumuongelee Magu, si muongee ilani ya chama.... Mkimwongea Magu mnampaisha sana
 
Jamani Lissu kapoa Sana hii sio dalili njema
 
Ndio Mkuu, naona kaanza kuhamasisha watu kuvuruga amani ya nchi kisa kuenguliwa kwa Wagombea.

TBC wamekata baada ya kuona Mbowe kaanza kuongelea suala la kuligawa Taifa.

Labda kumgawa mama ako, siyo taifa.
 
Wafuasi wenu wanatumia bundles zao internet kufuatilia mnachozungumza hasa baada ya kukosekana kwa tv kurusha mikutano yenu.

Tunaomba tafadhari nendeni moja kwa moja kwenye mada na maana ya mkutano ili kusaidia mifuko yetu.

Acheni kusema ya kwenu
 
Kuna siku Lissu alikuwa anahutubia katika mji mmoja, Lissu akawa anapigapiga microphone kwa sababu alikuwa anahisi sauti haitoki
Nilichogundua ni kuwa kuna hujuma kwa fundi mitambo wa Chadema, anapunguza sauti ya Lissu systematically ili Lissu asisikike vizuri.

Kwa mfano hata leo huko Mbagala inaonekana huyo fundi mitambo amefanya mchezo huohuo. Wakati akina Mnyika na Mbowe wanaongea wakawa wanasikika vizuri, ila muda wa Lissu kuongea kukawa na kupungua kwa Intensity ya Sauti mpaka wananchi kwenye mkutano wakawa wanalalamikia sauti ya Lissu.

CHADEMA chunguzeni katika timu ya fundi mitambo wenu huenda kuna kirusi, Fundi mitambo anaminya sauti ya Lissu.

Sound Engineer wenu anamhujumu Lissu mbadirisheni au mkanyeni!
 
Mkuu kama huna bundle ya kutosha imekula kwako lakini hilo ombi lako halikubaliki.
 
Atakiponza chama mpeni tu likipaza sauti..😂
 
Ila wakuu kuna Watu wandani ya chadema wanahujumu chadema huu ufunguzi ni wa ovyo sana na makosa ni mengi sana ya waziwazi
 
Hapana mkuu TBC hawafel hata kidogo chombo Cha habari Cha Taifa hakiwezi kurusha matamko ya Chuki na vurugu namna hiyo hata siku moja, CHADEMA hawana stahe hizi sio siasa bali chuki tu na kuhamasisha vurugu tupu.
mkuu Hawa watu hawajielewi.

wanachojua Ni kuhamasisha chuki tu
 
Ndo kusema sera ya kwanza ya CHADEMA ni kufanya vurugu, kwani hao waliokatwa wamekatwa na wananchi?, Kama hapana, basi hizo vurugu zifanywe na hao viongozi wa chadema dhidi ya wakataji, maana kuwahusisha wanaanchi ni kuwaonea tu,
 
Ila wakuu kuna Watu wandani ya chadema wanahujumu chadema huu ufunguzi ni wa ovyo sana na makosa ni mengi sana ya waziwazi
Uhovyo wake ni nini
Au unadanganyika na camera angle za tbc
Kuna nyomi la maana tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…