Uchaguzi 2020 Yaliyojiri Vikao vya CHADEMA: Tundu Lissu aibuka kidedea kuwania Urais wa Tanzania kwa kupata kura 405 dhidi ya Nyalandu 36 na Dkt. Majige 1

Uchaguzi 2020 Yaliyojiri Vikao vya CHADEMA: Tundu Lissu aibuka kidedea kuwania Urais wa Tanzania kwa kupata kura 405 dhidi ya Nyalandu 36 na Dkt. Majige 1

Nimemsikia bwana mbowe na nimekuelewa sana kwenye kipande hicho[emoji116]yani chama kinahitaji Sana watu wapya Hili kikue ila chama akihitaji watu wapya kwenye nafasi ya uwenyekiti taifa ili kikue chama kinamuhitaji Mbowe tu kwenye nafasi hiyo very shame!!
Screenshot_2020-08-03-16-56-46.jpg
 
alimshinda wapi?

Kwenye mchujo wa watia nia 10 ndani ya CHADEMA na kubaki hawa wa3....

Ndo nauliza, ni vigezo gani vilitumika hata mama huyu akaonekana bora kuliko mtia nia mwenzake Mch. Peter Simon Msigwa?
 
Habari kutoka chanzo cha kuaminika zimethibitisha kuwa LAZARO NYALANDU anaongoza katika kura za maoni.

Mmoja kati ya wanaomuunga mkono NYALANDU amesikika akisema kuwa:-

"Mzee NYALANDU anaongoza lakini Baadhi ya viongozi wa juu wa chama chetu wanahaha kupora kura zake ili tu asiwe mshindi, kinachoonekana hapa wanamtaka LISSU ndo awe mshindi wao lakini Leo ndio tutaudhihirishia umma wa Watanzania na Dunia kuwa sisi ni chama cha Demokrasia au la! Hatuwezi kukubali"
Mbona mnakuwa wambeya!? Uchaguzi ndio unaendelea na upigaji Kura haijaisha, hao Viongozi wakuu wanaporaje Kura!?
 
Akilihutubia Baraza kuu LA Chadema, Mwenyekiti wa Chadema Taifa mhe Kamanda mkuu Freeman Mbowe amesema SASA BASI.

Kuonewa, kuibiwa kura, kushambuliwa, kupigwa risasi nk sasa mambo hayo BASI.

Uchaguzi mkuu 2020 unaelekea kuwa mtamu sana, na kondoo wanaenda kugeuka Nyati na huo muziki wake sio mchezo.
 
Mbona mnakuwa wambeya!? Uchaguzi ndio unaendelea na upigaji Kura haijaisha, hao Viongozi wakuu wanaporaje Kura!?
Kwa nini hamjaruhusu watu wa habari waingie? Au mnaogopa mtapigana makonde ?Upigaji kura ulipoanza naona live online tv hazionyeshi tena.
 
Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo imewapitisha Tundu Antipas Lissu Lazaro Nyalandu na Dr Mayrose Majige kusaka nafasi ya kuwania Urais Tanzania.

Katika kikao chake cha Kamati Kuu kilichomalizika usiku mnene majina hayo Leo yataletwa ndani ya Baraza Kuu ambao watakata mzizi wa Fitna kumpata Mgombea mmoja baada ya kupigiwa kura na jina moja kuwasilisha ndani ya Mkutano Mkuu kesho kuidhinishwa.

Yeyote atakayepitishwa na Baraza Kuu anafaa kuwania Urais Kama vigezo vilivyowekwa na kuchambuliwa na chama hicho.


Stay Tuned.


UPDATES:

======

Ratiba ya leo Tarehe 3, Agosti 2020, Baraza Kuu la Chama litakutana katika kikao chake, ambapo litajadili masuala mbalimbali ikiwemo “kufanya mapendekezo ya wagombea wa Urais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Zanzibar na kuyawasilisha katika Mkutano Mkuu kwa uamuzi,” inavyoelekezwa kwenye ibara ya 7.7.12(a).

Aidha, kwa mujibu wa ibara ya 7.7.12 (n) Baraza Kuu litajadili rasimu ya Ilani (manifesto) ya Uchaguzi Mkuu na kuwasilisha mapendekezo yake kwa Mkutano Mkuu kwa maamuzi.

= > Viongozi Wakuu wa Chadema wameshafika hivyo shughuli rasmi inatarajiwa kuanza hivi punde. Kwa sasa Viongozi hao wapo mbele na Wimbo wa Taifa unaimbwa.

= > Baada ya wimbo wa taifa imefanyika dua kwa ajili ya kufungua Mkutano.

= > Baada ya dua utambulisho wa Kanda mbalimbali zilizohudhuria, Wajumbe wa Bodi ya Udhamini, Wajumbe wa kamati kuu na wageni waalikwa unafanyika.

Katibu Mkuu wa chama John Mnyika akabidhiwa kipaza sauti kwa ajili ya kuongoza mkutano
Nimesimama kufanya kazi mbili tu kwa sasa. Kazi ya kwanza ni kueleza hakiki ya kikao hiki. Baraza kuu letu kwa sasa lina jumla ya Wajumbe 456 wa kikatiba na mpaka nasimama kuzungumza na nyinyi jumla ya Wajumbe 367 sawa na asilimia 80.5wamekwisha ingia kwenye kikao.

La pili ni kueleza kwa muhtasari Ajenda za kikao hiki. Kikao hiki kina jumla ya ajenda saba;

Ajenda za Kikao/ Mkutano:
  • Ufunguzi wa Kikao ambao utafanywa na Mwenyekiti wa Chama
  • Ajenda ya pili ni kuthibitisha ajenda zitakazofuata
  • Ajenda ya tatu ni kujadili rasimu ya ilanio ya Uchaguzi Mkuu kwa mwaka 2020
  • Ajenda ya nne ni kupendekeza majina ya Mgombea wa Urais, Mgombea Mwenza na Mgombea Urais wa Zanzibar
  • Ajenda ya tano ni kuthibitisha mikakati na rasilimali za kuendesha kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2020
  • Ajenda ya Sita ni kufanya mapendekezo ya ajenda za kikao kitakachofanyika kesho
  • Ajenda ya saba ni kuhitimisha kikao.

Ufunguzi wa kikao

Freeman Mbowe
Kwa niaba ya chama kama kiongozi mkuu wa chama nachukua nafasi hii kuwapongeza kwa kukiimarisha chama na kukipigania chama wakati watesi wetu walitegemea mkate tamaa nyinyi mliopo katika ukumbi huu mmesimama kukilinda chama, mmekipigania chama, mmekuza thamani ya Chama chetu.

Na binadamu anasema kila jambo ni mpango wa Mungu. Yawezekana tulikwazika sana tulipoona baadhi yetu tuliowaamini na kufanya kazi pamoja wakikisaliti chama chetu, wakiisaliti dhamira yetu. Natambua ni namna gani tuliumia tulipoona Wabunge wetu wakitukana viongozi, wakikidhalilisha chama hiki. Hatukuwaombea mabaya kwa sababu anayetoa adhabu ni Mwenyezi Mungu. Lakini binadamu tunasema malipo ya dhambi yanaweza kuwa hapahapa na si lazima akhera.

Lakini niwaambie ndugu viongozi, hatuna sababu hata moja ya kusikitika. Waliokata shauri la kuondoka katika chama chetu hatuna sababu ya kujutia, tuna sababu ya kujifunza. Lakini tutambue wakati wote, chama cha siasa ni watu. Ili muweze kuwa chama kinachokua lazima utamaduni wa kuwapata wanachama wapya, viongozi wapya, watu wapya uwe ni utamaduni wa kudumu katika chama cha siasa.

Nasema hili kama kiongozi wa Chadema, kwamba chama hiki tumekijenga na kimefikia hapa kwa kuwa siku zote tumefungua milango. Tumeruhusu watu waje hapa kwa mamia, tumeruhusu watu waje hapa kwa maelfu. Chama hikitumekijenga kuwa chama cha watu na sio kikundi kidogo cha watu kinachojiita Chadema ambacho hakitaki kufungua milango wengine waingie. Tunatamani siku moja kila Mtanzania awe mwanachama wa Chadema.

Nimesikia kauli kutoka kwa viongozi mbalimbali wakitamka kuwa mtu yoyote akitoka Chama cha Mapinduzi asiingie katika chama hiki hiyo sio sera ya CHADEMA mtu akitoka chama chochote anakaribishwa CHADEMA lakini atambue akifika anawajibu wa kuishi kwa mila, desturi, katiba, kanuni na muongozo wa Chadema.

Tunapowakataa wanachama wa chama cha Mapinduzi eti kwa sababu tunasema tunasomo kutoka kwa waliotuhama je wakitupa kura zao tutazikataa au tutazikubali? Tunapoenda kwenye Uchaguzi Wapiganaji wenzangu, tunatamani kura za wote, wa CCM wasio wa vyama vingine, wasio na chama. Haiwezekani tukabaguana, tukawabagua wa vyama vingine halafu kesho tukawashawishi wakatupe kura zao.

Tunahitaji kujenga umoja wa chama wakati huo huo tukijenga umoja wa taifa. Inawezekana tukawachukia sana baadhi ya viongozi wanaofanya maamuzi katika Chama cha Mapinduzi lakini ikaja kama chama hatuwezi kuwachukia wanachama wote wa CCM kama ni maadui zetu.

Tunahitaji kujenga ushawishi wa kisiasa tunahitaji kuonesha upendo huo ndani ya nchi yetu. Tunataka tukiongoza nchi hii tuwe united as a country. Hatuhitaji tuongoze nchi ambayo imepasuka pasuka vipande vya kiitikadi. Tunahitaji umoja wa kitaifa tunahitaji mmoja, tunahitaji wawili wote wawe wamoja.

Ndugu viongozi lazima tuendelee kukilinda chama

Tunahitaji watanzania wote wawe wanachama wa chadema Tunahitaji ushirikiano kukiimarisha chama hiki.

Tufanye nini tofauti zetu za ndani zikiharibu chama hiki hakuna aliebora na hakuna kipindi kibaya cha kukigawa chama kama kipindi cha uchaguzi.

tumepita hatua mbaimbali za kujifunza leo tumefika wakati wa kuwa chama kikuu kwelikweli.

Kazi hiyo na matunda haya ni lazima tuyalinde kwa nguvu zetu kwamba yoyote asitutoe kwenye reli chaguzi zinapita na chama kitabaki na tunawajibika kukiacha salama.

Chama hiki kilikuwa kidogo kweli kweli Mwaka 2010 tukasema mweshemiwa Wilbroad Silaa akiwa katibu wa Chdema alipendekezwa kuwa mgembea wa urais
Hatukumpigia kura Dr Slaa.

Naposema chama hiki kimekuwa ndugu viongozi kwa mara ya kwanza tunakwenda kwenye uchaguzi wa rais na madiwani na tunawagombea 214 katika majimbo yote 214. Halafu anatokea mtu anasema chama hiki kinakufa inabidi tucheke kidogo

Tuliweka mipango kwamba ikifika 2020 Zanzibar tuwe na uwezo angalau wa kusimamisha asilimia 50.

Katika baraza la wawakilishi 112 tunawagombewa asilimia 53 katika bara tuna kata 3659 tunawagombea kata 3920 kuna kata kama 40 tunakamilisha na mpaka kufika mwisho tutasimamisha kata na wabunge asilimia miamoja.

Huko nyuma tuliingia kwenye mazungumzo na vyama vingine. Tusijenge tabia ya kujimwambafai ya kufikiri sisi ni chama kikubwa na ukubwa wetu usitujenge kiburi tumuheshimu kila mtu. Tukiona kuna maslahi mapana kwa chama na nchi tutafanya hivyo. Hatuta ingia kwenye ushirikiano kama fashion.

Na hatutaingia kwenye ushirikiano na watu ambao hawatatuuza njiani. Na sasa tunamazungumzo na chama kimoja ambacho ni ACT. Tunazungumza vilevile kuhusu kuachiana nafasi ya urais kwa visiwa vya zanziabar.

Nimezungumza kwa kifupi nyufa za kiuchaguzi tunafanya kampeni za kuchafuana wenyewe kwa wenyewe.

Tutamaliza mkutano mkuu kesho tutatoka na jina moja la mgombe na tukimaliza wote na wamoja tutoke tumeshikana. Fikiria leo unamkashifu na kumtukana mtu halafu kesho mnataka kunia mamoja

Ni kwa nini tusijifunze kwa chama cha mapinduzi ambacho kimeshindwa kujenga umoja wao kwa makundi ua uchaguzi.

Ni matumaini yangu wagombea wote watatu waliopendekezwa kwenda baraza kuu watania mamoja.

Nguvu yetu ni umoja wetu tutoke hapa na nyuso za furaha tumpate mgombea wetu kwa furaha na sio kujenga mpasuko.

Ni vyema tuwe na akiba kwa hiyo kila mmoja kwenye chama chetu ni wajibu wetu kumpigania na kumpendekeza anaemtaka.

Sisi ni familia Chadema na familia inaimirika wakati wa majaribu na tuioneshe dunia sisi tutaimarika wakati wa majaribu.

Sisi tumeonewa sana tumebezwa sana tumefungwa sana uchaguzi huu tukasema sasa basi.

Nyarandu ajielezea

Asema mimi nilikuwa kipofu nilikuwa sioni ni kama yule kipofu anaelezwa kwenye biblia baadaya kupakwa matope na mzee wa siku akaona tena.

Na mimi nimeguswa tena katika hiki chama naomba mkiona vyema mnipe nafasi ya kusisimama kama mgombea uraisi wa CHADEMA.

Nasema uwezo wa kuiondoa CCM tunao na tupate Urais madiwani na wabunge wa kutosha nipo tayari na nimejiandaa tufanye kampeni kwenye majombo manne kwa siku twende ardhini twende kwa anga na kwa maji.

Turudishe tena tabasamu la wazee wetu tunataka wazanzibar wamiliki tena rasilimali zao za mafuta na gesi na uchumi wa baraza kuu.

Tunataka CHADEMA wasiisome namba tena nao wana CCM wasiisome namba tena na watanzania wasiisome nammba tena, watanzania watamiliki rasmi rasilimali, tutahakikisha tunapunguza madaraka rukuki ya rais, na tutaandika upya katiba ya Tanzania tukianzia na rasimu ya jaji Warioba tutaanzisha benki ya vijana tutaanzisha tena bima ya afya.

Tutashusha kodi, tutaimarisha uchumi wa nchi yetu, tutarekebisha ubora wa elimu kote nchini na tutashirikiana na wanachama wetu tutashusha kodi na kuongeza uzalishaji na kuimarisha ushiriki wa wanawake katika uchumi na uzaishaji kote nchini. Na tutahakikisha CHADEMA inaendelea kukua kutoka utukufu hadi utukufu.

Nilijiunga na CHADEMA 2017 na nikawa kiongozi wa kawaida nikawa mjumbe wa
Kamati tendaji ya Wilaya Singida kasikazini.

Alichokiongea Mh. Mbowe ndicho nilichohitaji kisemwe mapema ili "sisi" tusioamini katika ushirikiano tujue umuhimu na jinsi ya kushirikiana kwa faida isiyokoma.
 
Akilihutubia Baraza kuu LA Chadema, Mwenyekiti wa Chadema Taifa mhe Kamanda mkuu Freeman Mbowe amesema SASA BASI.
Kuonewa, kuibiwa kura, kushambuliwa, kupigwa risasi nk sasa mambo hayo BASI.
Uchaguzi mkuu 2020 unaelekea kuwa mtamu sana, na kondoo wanaenda kugeuka Nyati na huo muziki wake sio mchezo.
Akae mstari wa mbele tu, sio kuwatanguliza wasiojitambua.
 
Jamaa kwa kuongea tuu yupo vizuri, tatizo utekelezaji. Atawaweka bavicha mbele yeye haonekani
 
Mhe.Msigwa hakuchukua form ya urais bali alitiania tu

1. Mpaka hatua hii bado wote wapo kwenye hatua ya kutia nia tu ndani ya vyama vyao.

2. Hatua ya awali ilikuwa na watia nia 10 kutaka wapitishwe na chama kuwa wagombea rasmi. Wakachujwa na kubaki "watia nia bora" wa 3 ambao ndiyo hawa walio katika mchujo wa hatua hii.

3. Hakuna mgombea aliyekwisha kuchukua fomu ya kugombea Urais toka NEC mpaka sasa.

CCM wameshamthibitisha tayari mgombea wao aitwaye ndugu John Pombe Magufuli. CHADEMA bila shaka atakuwa Tundu Lissu.

Baada ya hapo kuanzia tarehe 5/8/2020 NEC imefungua dirisha la wagombea kuchukua fomu za uteuzi wa NEC kuwa wagombea rasmi kwa tiketi za vyama vyao.

Sasa sijaelewa unamaanisha nini kusema Msigwa hakuchukua fomu ya uteuzi? Kama ni fomu ya NEC, yes, hakuchukua na hawezi kuchukua mpaka sasa kwa kuwa ni illegible.
 
Nimepita hapo Mlimani city muda huu, hakuna bendera za CDM nje zilipozoeleka kuwekwa. Je wamepigwa mkwara?
 
Back
Top Bottom