Uchaguzi 2020 Yaliyojiri Vikao vya CHADEMA: Tundu Lissu aibuka kidedea kuwania Urais wa Tanzania kwa kupata kura 405 dhidi ya Nyalandu 36 na Dkt. Majige 1

Uchaguzi 2020 Yaliyojiri Vikao vya CHADEMA: Tundu Lissu aibuka kidedea kuwania Urais wa Tanzania kwa kupata kura 405 dhidi ya Nyalandu 36 na Dkt. Majige 1

comment nyingi humu si za wana chadema . hapa nimestuka , nyakati hizi ni za lisu ,over!!!!
 
Haisemi hivyo ila ni mawazo yangu tuu nimejaribu kuwaza tuu watafanya mbinu hiyo ili kumdhibiti makusudi
Itakuwa ni mbinu chafu itakayoonesha udhaifu wa watakaoutumia na genge lao. Ni kama mtu kutoka nje ya ulingo na kumpiga kiti kichwani aliyeko ndani ya ulingo aanguke halafu uliyekuwa unapigana utangazwe mshindi.

Waruhusu mtanange wa wazi hata watazamaji wafurahi. Huoni hata hizi mechi baada ya Corona hazinogi bila watazamaji?[emoji3][emoji3]
 
Maneno hayo ameyasema wakati akiomba kura kwa wajumbe wa baraza kuu la Chadema ili aweze kupeperusha bendera ya chama hicho kwa nafasi ya urais.

Amesema uchaguzi wa mwaka huu hautakuwa rahisi kwa kuwa Tume ya uchaguzi haiko huru na vyombo viko upande wa CCM.

Amesema yeye hatamwachia Mungu ila kwa Mungu atapeleka mahesabu tu!

Amesisitiza kuwa yeyote akaye jaribu kuiba uchaguzi atasombwa na kimbunga!

Maneno hayo yanashabihiana na yale aliwahi kuyesema wakati alipokuwa akizungumza na Watanzania waishio Marekani kuwa 'CCM itang'olewa madarakani kwa Tsunami'!

Tuwape tahadhari CCM, uchaguzi huu hamtabebeka kirahisi, jipangeni kutafuta kura halali, mipango ya kutangazwa bila kushinda inaweza isifanikiwe!
 
Itakuwa ni mbinu chafu itakayoonesha udhaifu wa watakaoutumia na genge lao. Ni kama mtu kutoka nje ya ulingo na kumpiga kiti kichwani aliyeko ndani ya ulingo aanguke halafu uliyekuwa unapigana utangazwe mshindi.

Waruhusu mtanange wa wazi hata watazamaji wafurahi. Huoni hata hizi mechi baada ya Corona hazinogi bila watazamaji?[emoji3][emoji3]
Yaa ni kweli kabisa kuna mbinu ovu inasukwa ili kumkomoa tatizo watu hawaoni mbali ndio maana tarehe imesogezwa mbele mwishoni mwa mwezi wakati huo ile mbilike mbilike ndio itakuwa inaanza na wao hapo ndio watatumia hiyo fursa
 
Sikukuelewa aliposema *hatamuachia Mungu* nikasema heeek! Inakuwaje sasa hapa wkt hili Neno huleta FARAJA kwa waliopigwa! Shindwa!
 
Aliyeagiza kuuawa kwa Tundu Lissu na aliyetekeleza maagizo ya kipumbavu ya kutaka kumuua Tundu Lissu kwa kumpiga risasi Mungu ana waona.
 
Hakuna uvumilivu usio na mwisho, sasa basi. Kama mbwai na iwe mbwai.

Tucalculate ratio ya Makamanda to policcm tupate solution ya mbinu rahisi ya kuwakabili.
 
Ni uhakika na taasisi kama tatu hivi ambako piga ua kiwete hawezi kuajiriwa au kuongoza, Urais, Upadri na Jeshi!
 
Hivi kipindi hiki mbona polisy wameufyata hivi sioni wakitembeza virungu hapo mliman city kama kawaida yao
 
Kwa hiyo safari hii Chadema hawahitaji utafiti wa ubora wa mgombea kama walioufanya 2015 ili kumpata Mzee Lowassa!? Au wamefanya!? Kama wamefanya, wanatarajia kupata kura ngapi za urais, na idadi ya wabunge na madiwani!? Au muda bado, chochote chaweza kutokea!?
 
Ni uhakika na taasisi kama tatu hivi ambako piga ua kiwete hawezi kuajiriwa au kuongoza, Urais, Upadri na Jeshi!
Dhambi ya Ubaguzi haijawahi kumwacha salama anayeitenda.Haujafa haujaumbika,usijione umesimama...
 
Back
Top Bottom