Yawezekana kama Mwanadamu Idi Amin alikuwa na Mapungufu yake ila nimegundua Afrika ya leo iliwahitaji akina Amin wengi ili kupiga hatua

Yawezekana kama Mwanadamu Idi Amin alikuwa na Mapungufu yake ila nimegundua Afrika ya leo iliwahitaji akina Amin wengi ili kupiga hatua

kaulize uganda au waganda nini kizuri alifanya hata kimoja tu, zaidi ya kutaka kuifanya uganda iwe nchi ya kiislam. alinyangánya biashara kwa wahindi akafukuza wazungu na kuwa mzinzi mkuu. ukimsikiliza hata kwenye clip zake tu utajua alikuwa mwanadamu mwenye IQ ndogo sana kama ubongo wa samani pamoja na kuwa na mwili mkubwa.
Habari zingine kuhusu yeye ni propaganda tu....
Sahv yenyewe kuna viongozi wanafanya mabaya Kuliko hata yeye

Ova
 
He was bad lakini sio kama anavyozungumziwa, kuna sifa zingine ameongezewa za ziada ili kuwaaminisha watu ubaya wake kwa maslahi ya ngozi nyeupe........
 
kaulize uganda au waganda nini kizuri alifanya hata kimoja tu, zaidi ya kutaka kuifanya uganda iwe nchi ya kiislam. alinyangánya biashara kwa wahindi akafukuza wazungu na kuwa mzinzi mkuu. ukimsikiliza hata kwenye clip zake tu utajua alikuwa mwanadamu mwenye IQ ndogo sana kama ubongo wa samani pamoja na kuwa na mwili mkubwa.
Aliwafukuza wanyonyaji wa rasilimali za nchi.Chukulia mfano makenikia unadhani wazungu au wahindi ni wazuriii?
 
Marehemu Idi Amin Dada....

1. Alichukia Upuuzi ( Upumbavu )

2. Alichukia Uonevu na Dharau

3. Aliwapenda sana Wananchi wake

4. Hakuwa Mnafiki na wa Kujipendekeza

5. Hakuwa Muoga kuipigania nchi yake

6. Hakuwa Fisadi ( Mwizi ) hata kidogo

7. Alikuwa Mbabe ili Kulinda nchi yake

Sasa wakati umefika kwa Waafrika Kukiri kuwa tulikosea au tulilazimishwa tu na 'Mabeberu' katika Kumchukia Idi Amin Dada hivyo tuombe Radhi kwa Familia yake na hata kwa Mwenyezi Mungu ikiwezekana.

Kwa mtazamo mfupi tu ni kwamba kama nikisema niyapime Madhambi ya Marehemu Idi Amin Dada kipndi chake na hawa Viongozi wa sasa wa Afrika tulionao Mzani wangu utalalia hasa kwa Viongozi wa sasa kwani 90% yao wanafanya ( wanatenda ) maradufu ya aliyokuwa akiyafanya Idi Amin Dada ila Waafrika wengi ama kwa Unafiki wetu au kuwa Kwetu Mapopoma ( Majuha ) au kwa Kushikiwa kwa muda Akili zetu na Mabeberu ( Wazungu ) tunaogopa Kukemea, Kukosoa na hata Kusema Ukweli juu ya Masuala Mtambuka katika nchi zetu nyingi ( kama si zote ) za Kiafrika.

R.I.P sana tu Marehemu Idi Amin Dada.
Hata Mwendazake kuzimu aliwapenda Sana wanyonge ila sasa yuko kuongoza malaika kama alivyoomba 😁😁😁
 
Hata Mimi Mkuu huyu nilikuwa namchukia ila nimekuja Kumtafakari vyema, Kumsoma vyema na hata Kuwahoji Wazee wa Uganda nimegundua Kiuongozi hakuwa na baya japo Kiubinadamu kama tulivyo Wengine nae alikuwa na Mapungufu yake.
Ni kwa Sababu mna share hulka na tabia za kuwa mentally retarded stupid creatures 🏃🏃
 
Madikteta walikula raha duniani sasa hivi wapo kuzimu wanakula msoto. Kuzimu Hakuna madaraja mnawekwa wote watenda dhambi bila kujali ulikuwa nani duniani.
 
nimesema tuambieni kicho chochote cha maendeleo alikifanya idi amini ndio na sisi tuwaletee evidence. au mnataka pia evidence kwamba alikusanya walemavu na kiuwalisha mamba mto kagera? mnataka? msimtetee kwasababu alikuwa muislam, ameichafua sana hiyo dini.
Kumbe unajadili kwa misingi ya udini?

Wewe umesema alikua anakula nyama za watu na kutupa vilema mto Kagera,sasa ndio naomba kama una prove yeyote kutoka kwenye reliable source uweke hapa.
 
tutajie maendeleo yeyote aliyoyafanay idi amini kwa kipindi chote alichotawala, zaidi ya kufukuza wahindi na kunyangánya/kuua biashara zao, kutupa vilema mto kagera, kula nyama za watu na kulala na wanawake.
Yaani afanye hayo yote ya Kuua Watu, kuuua Biashara, kufukuza Wahindi, Kutupa Vilema Mtoni, kula Nyama za Watu, lakini hatimaye hawakumuondoa madarakani mpaka ilipofika Vita vya Kagera..!

Yaingia Akilini Kweli? Na waliokuwa wakiishi kwa wakati huo Nchini Uganda, walikuwa wakiishi kwa vigezo vya namna gani?

Walau sasa hii drama zinaanza kufifia na Wengi wameng'amua.
 
Yaani afanye hayo yote ya Kuua Watu, kuuua Biashara, kufukuza Wahindi, Kutupa Vilema Baharini, kula Nyama za Watu lakini hawakumuondoa madarakani mpaka ilipofika Vita vya Kagera..!

Yaingia Akikini Kweli? Na waliokuwa wakiishi kwa wakati huo Uganda walikuwa wakiishi kwa vigezo vya namna gani?

Walau sasa hii drama zinaanza kufifia na Wengi wameng'amua.
alikuwa mtu hatari sana, na asiyetumia akili vizuri, ukisema fyokofyoko tu kesho wanakukuta umeshadenji. kwani hata nchi fulani tu sitaki kuitaja, walikuwa na rais kipindi fulani wananchi wake walikuwa hawaongei, ukiongea tu wasiojulikana wanapita na wewe. kuna mtu alikuwa ananyanyua mdomo wake kipindi kile? same kwa idi amini, kipindi chake alikuwa akikohoa tu watu wanaitika wanafikiri anawaita wao. kila mtu alikuwa anaponya maisha yake. ukionekana msomi tu unamchallenge na kumshauru mambo ya kisomi ambayo yeye hakuwa msomi, anakuchinja.
 
He was bad lakini sio kama anavyozungumziwa, kuna sifa zingine ameongezewa za ziada ili kuwaaminisha watu ubaya wake kwa maslahi ya ngozi nyeupe........
Mimi hii ya kwamba sijui alikuwa akila Nyama za Binadamu nitaikataa na siiamini hadi Pumzi yangu ya mwisho hapa duniani.
 
alikuwa mtu hatari sana, na asiyetumia akili vizuri, ukisema fyokofyoko tu kesho wanakukuta umeshadenji. kwani hata nchi fulani tu sitaki kuitaja, walikuwa na rais kipindi fulani wananchi wake walikuwa hawaongei, ukiongea tu wasiojulikana wanapita na wewe. kuna mtu alikuwa ananyanyua mdomo wake kipindi kile? same kwa idi amini, kipindi chake alikuwa akikohoa tu watu wanaitika wanafikiri anawaita wao. kila mtu alikuwa anaponya maisha yake. ukionekana msomi tu unamchallenge na kumshauru mambo ya kisomi ambayo yeye hakuwa msomi, anakuchinja.
Hakuwa mmbaya kivile
Tafuta wasaa uonge na waganda
Waliyokula chumvi watakuambia

Ova
 
Naomba Msamaha Kwake na kwa Mungu kwa Kuiamini hasa pale nilipokuwa Chalii ( Mdogo ) ila sasa Ukweli nimeshaanza Kuung'amua ( Kuujua )
Asee ilikuwa hatari Sana kweli ukitaka kumaliza adui mchagulie Jina baya
 
Nguvu ni uwezo wa kuliamrisha jeshi likutii,ambayo ikishaondolewa Hakuna utii.
Sasa hiyo nguvu hata viongozi au marais wasiokuwa madikteta wanayo pia kwa maana majeshi yanawatii pamoja ya kwamba wao
sio madikteta.
 
Sasa hiyo nguvu hata viongozi au marais wasiokuwa madikteta wanayo pia kwa maana majeshi yanawatii pamoja ya kwamba wao
sio madikteta.
[/QUOT
Nguvu utoka sehemu mbili kwa Mungu au Shetani maamuzi ni ya mwanadamu mwenyewe kuchagua upande autakao
 
Madikteta walikula raha duniani sasa hivi wapo kuzimu wanakula msoto. Kuzimu Hakuna madaraja mnawekwa wote watenda dhambi bila kujali ulikuwa nani duniani.
Jinsi mnavyowazungumzia hao madikteta utadhani hapa duniani tumekuja kufanya demokrasia na kwamba demokrasia ndio njia ya kwenda peponi, nasema hivyo kwa sababu unakuta mtu ana machafu yake kibao kiasi kwamba kinachomzuia yeye kuwa huko kuzimu ni kwa sababu hajafanya tu bado ila akifa nae anaenda huko kuzimu kutokana na madhambi aliyokuwa nayo ila ajabu mtu huyo unakuta amejisahau ya kwake na kujiona ni msafi kisa tu ni muumini wa demokrasia hapa duniani.

Hakuna pepo ya wapenda demokrasia.
 
Back
Top Bottom