Yevgeny Prigozhin, Boss wa Wagner Group ahofiwa kufariki kwenye ajali ya ndege!

Yevgeny Prigozhin, Boss wa Wagner Group ahofiwa kufariki kwenye ajali ya ndege!

Isome kwanza historia ya Urusi ndio ukomenti, yaani kabisa Urusi ipate matatizo Kwa sababu ya huyo mkuu wa Wagner? Kama ni kuwaza, jaribu kuwazua Zaidi.

Hapo Russia imepeleka ujumbe Kwa wote wanaofikiri Moscow ni pepesi kiasi hicho na hapo katika lugha ya picha wanasema kuwa ukicheza na Moscow umecheza na moto.

Kifupi nimefurahi sana, Kila siku yanatolewa maonyo na Urusi juu ya wanaotaka kujaribu kufanya jaribio lolote ndani ya Urusi lakini hawaeleweki, naamini Kuna siku dunia itaandika historia ya kilio kikubwa sana.

Endeleeni kufurahia tu, oooh! Superpower wa mchongo anapigwa na Ukraine ,mara oooh! Drone za Ukraine zimepiga ndani ya Urusi, mara oooh! Kuna siku hiyo oooh! Itasikika uwiiiiii

Kila siku sisi tuliojalowa jicho la hekima tunaona Ukraine anajiingiza kwenye hatari tena kubwa sana na ningepata nafasi Leo ya kumshauri Zelensky Rais wa Ukraine ningemwambia hivi ACHA KUCHEZA NA MOSCOW NA HIZO DRONES ZAKO KUNA SIKU UTALIA KILIO KIKAVU.
What if ni Ukraine kafanya assassination!

Sent from my Infinix X660B using JamiiForums mobile app
 
Ninataka Putin,huyu Prigozhin kaua sana maishani mwake watu wasio na hatia.
Screenshot_20230324-091126.png
 
Pia umezungumzia kuhusu Urusi kushindwa na Finland, chechen na Georgia. Sijui wewe vita huitazama vipi, but kwangu mimi vita ni matokeo ya nani anapata nini baada ya vita kutokana na malengo. Mfano, lengo la US ilikuwa ni kuilinda dola dhidi ya tishio la Gadafi, so licha ya kumuua gadafi, ameiangamiza kabisa libya kiuchumi-haitokuja tena kuwa tishio kwake. So, amefanikiwa.

Finland alisurrender mara zote mbili na kukubali kuachia ardhi yake kwa Soviet, achilia mbali maamuzi ya fedheha ya kukubali kuwashitaki na kuwafunga wanajeshi wake wenyewe waliopigana dhidi ya uvamizi wa soviet. Sawa na leo ukraine iwashitaki majenerali wake eti kwa kosa la kuzuia uvamizi wa Urusi.

Georgia kusini hadi leo iko chini ya Urusi.
Naomba unionyeshe ambapo niliandika Urusi ilishindwa na Finland, Georgia na Chechnya.
Nimesoma majibu yako na mifano uliyoitoa sikumbuki kuwafahamu so siwezi sema chochote.

ila tukiielewa historia ya Russia, ndio utaelewa kwanini iko hivi ilivyo leo.

Russia kwa muda mrefu Imekuwa ni military state, Kwa sababu ya utawala wa kifalme na Mavamizi/matishio ya kutokea nje-napoleon, hitler, NATO. So taifa la dizaini hiyo, unaweza elewa mtazamo wa watawala dhidi ya wapinzani. Hatari ya historia ya mavamizi, huzaa ufisadi na ubwenye. At least baada ya Putin kuingia for 20 yrs amedhibiti power struggle iliyokuwepo kwa miaka mingi. Kwa ufupi Russia bado ni taifa linalojitafuta kuelekea kuwa taifa la 'kisasa' zaidi.

Comperatively, Marekani ina bahati kubwa ya kijiografia. BAHARI. Kuzungukwa na bahari, imeifanya kuwa na jeshi imara la majini, hivyo kuwa ngumu kuvamiwa na rahisi kujilinda.
Israel ina tishio kubwa zaidi la kuvamiwa siku yoyote na haina autocracy. Kuwa na historia ya kuvamiwa sio kisingizio cha kuendekeza subordinates wabovu na kukataa meritocracy.
Hayo matukio yote niliyotaja hayatokani na kuvamiwa kwahiyo usisingizie Marekani kuwa na geographical location nzuri, mfano hiyo Great Purges ya Stalin ndiyo ilifanya uvamizi wa Nazi Germany uwe rahisi. Mna kiongozi ameua competent class ya watu zaidi ya laki saba na wengi wakiwa jeshini hilo linasaidia nini kuwalinda dhidi ya uvamizi.
 
Ili kuijua vizuri FSB na SVR isome vizuri KGB
Nafikiri hapa atapata mwanga kidogo!

FSB likely targeted Prigozhin's plane - UK defence sources

UK defence sources say that Russia’s FSB domestic intelligence agency (the successors to the KGB) are those most likely to have targeted Yevgeny Prigozhin’s plane.

They are totally loyal to Vladimir Putin and also run the border force.

Source: BBC:24/08/2023
 
Mimi nauliza hivi:

Je, inawezekana vipi viongozi wote wakubwa wa wagner wasafiri siku na muda mmoja huku ikijulikana wazi walikuwa wanawindwa wauawe?

Nawaza tena :

Inawezekana wote walikamatwa kwa pamoja kisha wakaingizwa kwenye ndege halafu ikalipuliwa.

Nawaza tena:

Siku aliyofukuzwa kazi mkuu zamani wa jeshi la anga (Gen Sergei Surovikin) ndiyo ajali hii inaenda kutokea!!!

Russian general who ran Ukraine war fired - report​


22 hours ago — One of Russia's leading military figures, Gen Sergei Surovikin, has reportedly lost his job as air force chief after weeks of speculation ...

BBC - Homepage › news › world-europe


Ukweli anao Putin mwenyewe!


'Putin's revenge' and Prigozhin's death 'no surprise'



6 hours ago — The Telegraph leads with UK security sources believing Prigozhin was killed in an assassination by Putin. They told the paper the aircraft ...

BBC - Homepage › blogs-the-papers


Ni mtazamo tu!
 
Wanawaza karibu sana hao wanaosema Putin angekamatwa akiwa SA, kitendo cha kumkamata Putin ndani ya nchi yoyote ni kumtangaza vita na Moscow na Urusi itamtoa kafara Putin lakini hiyo nchi itajiandaa kuua mamilioni kama sio mabilioni ya watu
Vijana wanaongea kwa ushabiki,nchi yyte wamkamate waone ICMB inavyofanya kazi.zaidi ya hapo nchi itakataa Putin kutembelea nchi husika ili kukwepa kadhia hiyo
 
Kitu ambacho sikielewi prigozin aliuwawa akiwa angani akitokea Moscow kwenda st petersburg sasa hivi unawezaje kujiachia kizembe kwenye mji mkuu wa makao makuu ya serikali uliyotaka kuipindua? Yani utake kumpindua samia umpelekee na vifaru mpka chalinze halafu eti akudanganye kakusamehe nawewe uendelee kuzurura dodoma au dar inawezekanaje?
 
Uko sahihi, ila kiutawala inakuwa imejipunguzia majukumu, na hayo majukumu kuhamishiwa kwa kampuni binafsi (wabobezi wa vita) ambao wanalipwa na utawala.

Kwa namna nyingine, utawala wao unakuwa umewapa maazimio hicho kikundi, nini wanataka yawe matokeo.

Ni sawa na wewe uingie mkataba na hicho kikundi, ukitaka kikalinde labda Niger; kwa hiyo wewe majukumu yako yatategemea na maazimio ya mkataba, je ni kuwapa silaa na fedha, usafiri, chakula n.k

Tunahitimisha; kwa sababu wameajiriwa na Urusi kwenye hayo mapigano na wanalinda maslai ya Urusi, kwa hiyo anayepigana pale ni mrusi.
Barikiwa mkuu.
 
Swali ninalojiuliza....Je,Marekani ilijua kama tukio hili lingetokea!!!!! Maana wiki iliyopita ilihimiza raia wake waondoke Belarus haraka Sana then wiki hii limetokea hili.[emoji848]

Sent from my Mi 9T using JamiiForums mobile app
Kwani hiyo ndege imeua watu walioko Belarus au imeua hao waasi tu?
Jibu ni kwamba hawakujua
 
Wanawaza karibu sana hao wanaosema Putin angekamatwa akiwa SA, kitendo cha kumkamata Putin ndani ya nchi yoyote ni kumtangaza vita na Moscow na Urusi itamtoa kafara Putin lakini hiyo nchi itajiandaa kuua mamilioni kama sio mabilioni ya watu
Uwezo huo wa kuuwa Mabilion ya watu huku Dunia itakuwa imelala tu wanasubiri Russia awamalize? Acheni basi kutupea matango pori.Yes, inaweza kuingia kwa vita lakini kusema atauwa Mabilion ya watu hapo umeongeza chumvi
 
Nafikiri hapa atapata mwanga kidogo!

FSB likely targeted Prigozhin's plane - UK defence sources

UK defence sources say that Russia’s FSB domestic intelligence agency (the successors to the KGB) are those most likely to have targeted Yevgeny Prigozhin’s plane.

They are totally loyal to Vladimir Putin and also run the border force.

Source: BBC:24/08/2023
Hawa jamaa huwa ni waongo na wataalam wa kupika stori. Kila wanachotunga kwenye SMO kinafeli.
 
Back
Top Bottom