Shadeeya
JF-Expert Member
- Mar 12, 2014
- 49,759
- 118,798
MWINYI ZAHERA ATAJA SABABU YA KUTO MTUMIA JUMA ABDUL
.
Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema hana tatizo na beki wa kulia wa timu hiyo Juma Abdul na anafahamu ni mchezaji mzuri lakini amesisitiza ni lazima awe 'fit' kuweza kwendana na kasi anayotaka
Kumekuwa wa presha kubwa kutoka kwa mashabiki ambao wamekuwa wakihoji sababu ya Abdul kutocheza kwenye kikosi cha kwanza huku Zahera akiwatumia baadhi ya wachezaji katika nafasi wasizostahili
Mfano beki ya kulia anapokosekana Paulo Godfrey 'Boxer', amekuwa akiwatumia Ally Ally, Mustafa Suleyman, Mapinduzi Balama na Cleofas Sosopeter badala ya Abdul ambaye miaka yote amekuwa akicheza nafasi hiyo
Aidha Zahera amewataka mashabiki wawe watulivu na kuacha kuingia majukumu ya kiufundi "Unajua mashabiki wao wanataka kuwa makocha wapange wao kikosi mimi ndiye ninayekaa na wachezaji muda mwingi hivyo nafahamu nani ni bora zaidi ya mwingin" "Juma msimu uliopita hajacheza michezo mingi wachezaji ninaowapa nafasi wamecheza wakiwa katika timu zao," amesema "Sina maana kwamba ni mchezaji mbaya hapana ni mzuri na amekuwa akipambana kusaka nafasi ya kucheza muda ukifika atapana nafasi hiyo kwasasa naomba majukumu yangu niachiwe mwenyewe nisiingiliw," "Mpira wa Tanzania unaendeshwa na ushabiki wao wakipata matokeo wanasahau kabisa kuwa waliocheza ni wachezaji wasiowapenda wakikosa matokeo pia hawakosi kitu cha kuzungumza"
Abdul alikuwa sehemu ya kikosi kilichosafiri Zambia wiki iliyopita ambapo mwishoni mwa wiki kilicheza Zesco United mchezo wa ligi ya mabingwa na kupoteza kwa kufungwa mabao 2-1
Zahera alimtumia Ally Ally beki ya kulia huku Abdul akiwa miongoni mwa wachezaji waliokuwa benchi
Pegine beki huyo anaweza kupata nafasi ya kucheza kwenye michezo ya ligi kuu ya Vodacom ambayo Yanga itacheza wiki hii
Alhamisi Yanga itacheza na Polisi Tanzania uwanja wa Uhuru kisha kurejea dimbani hapo siku ya Jumapili kuikabili Coastal Union.
Yangafulldozz
.
Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema hana tatizo na beki wa kulia wa timu hiyo Juma Abdul na anafahamu ni mchezaji mzuri lakini amesisitiza ni lazima awe 'fit' kuweza kwendana na kasi anayotaka
Kumekuwa wa presha kubwa kutoka kwa mashabiki ambao wamekuwa wakihoji sababu ya Abdul kutocheza kwenye kikosi cha kwanza huku Zahera akiwatumia baadhi ya wachezaji katika nafasi wasizostahili
Mfano beki ya kulia anapokosekana Paulo Godfrey 'Boxer', amekuwa akiwatumia Ally Ally, Mustafa Suleyman, Mapinduzi Balama na Cleofas Sosopeter badala ya Abdul ambaye miaka yote amekuwa akicheza nafasi hiyo
Aidha Zahera amewataka mashabiki wawe watulivu na kuacha kuingia majukumu ya kiufundi "Unajua mashabiki wao wanataka kuwa makocha wapange wao kikosi mimi ndiye ninayekaa na wachezaji muda mwingi hivyo nafahamu nani ni bora zaidi ya mwingin" "Juma msimu uliopita hajacheza michezo mingi wachezaji ninaowapa nafasi wamecheza wakiwa katika timu zao," amesema "Sina maana kwamba ni mchezaji mbaya hapana ni mzuri na amekuwa akipambana kusaka nafasi ya kucheza muda ukifika atapana nafasi hiyo kwasasa naomba majukumu yangu niachiwe mwenyewe nisiingiliw," "Mpira wa Tanzania unaendeshwa na ushabiki wao wakipata matokeo wanasahau kabisa kuwa waliocheza ni wachezaji wasiowapenda wakikosa matokeo pia hawakosi kitu cha kuzungumza"
Abdul alikuwa sehemu ya kikosi kilichosafiri Zambia wiki iliyopita ambapo mwishoni mwa wiki kilicheza Zesco United mchezo wa ligi ya mabingwa na kupoteza kwa kufungwa mabao 2-1
Zahera alimtumia Ally Ally beki ya kulia huku Abdul akiwa miongoni mwa wachezaji waliokuwa benchi
Pegine beki huyo anaweza kupata nafasi ya kucheza kwenye michezo ya ligi kuu ya Vodacom ambayo Yanga itacheza wiki hii
Alhamisi Yanga itacheza na Polisi Tanzania uwanja wa Uhuru kisha kurejea dimbani hapo siku ya Jumapili kuikabili Coastal Union.
Yangafulldozz