Zakazakazi: Yanga sio Mabingwa mara 29 na Simba sio Mabingwa mara 22

Zakazakazi: Yanga sio Mabingwa mara 29 na Simba sio Mabingwa mara 22

Akitumia takwimu za walioshiriki Klabu Bingwa/Ligi ya Mabingwa Afrika pekee anaweza kuwa anakosea. Nafikiri kuna wakati aliyekuwa anashiriki Klabu Bingwa ni aliyechukua Kombe la Muungano, kama sikosei kwa hiyo hapo tayari Bingwa wa Tanzania Bara alikuwa amepatikana, unless hakuwa anatambulika kama bingwa. Ila aangalie na hizo data na taratibu za kipindi kile za kupata mabingwa. Yanga wana tabia za kupotosha kwa hiyo sitashangaa kama na hili wamelilazimisha.

Ila ningependa Yanga wakumbushwe kuwa hadi mashindano ya CECAFA level ya vilabu yanasitishwa, Simba ndiyo anashikilia rekodi ya kulichukua mara nyingi.
Hapana yeye anahesabu mashindano ya FAT (Football Association of Tanzania) ambayo ilisajiriwa na FIFA mwaka huo 1965 na TFF tu; anasahau kuwa kabla ya FAT kulikuwa na mashindano TFA (Tanganyika Football Assosciation) ambayo yalikuwa hayakusajiliwa na FAT yal;iyoanza kabla ya uhuru ingawa hayakuwa maarfu sana. Kumaliza ubishi yeye aende ofisini akahesabu makombe yao.
 
Hapana yeye anahesabu mashindano ya FAT (Football Association of Tanzania) ambayo ilisajiriwa na FIFA mwaka huo 1965 na TFF tu; anasahau kuwa kabla ya FAT kulikuwa na mashindano TFA (Tanganyika Football Assosciation) ambayo yalikuwa hayakusajiliwa na FAT yal;iyoanza kabla ya uhuru ingawa hayakuwa maarfu sana. Kumaliza ubishi yeye aende ofisini akahesabu makombe yao.
Kuhesabu mashindano ya kabla ya uhuru siyo sahihi pia na sidhani kama hiyo mara 29 ya Yanga inajumuisha ubingwa kabla ya uhuru.
 
Screenshot_20230619-103557.png
KWAKO MCHAMBUZI MKUBWA MWAISABULA - 3

Kaka mkubwa @mwaisabula_mzazi, siyo tu kwamba ligi ile ya zamani ilishirikisha timu za Zanzibar ili kuleta sura ya utaifa, bali pia ilifanyika juu ya ardhi ya Zanzibar.

Mwaka 1977, uwanja wa Amaan ulikuwa moja ya vituo vya ligi hiyo, kama kipande hicho cha andiko la msimu huo kinavyosema...naamini hii hukuwa ukiijua!

Ni hivi...

Nimekuwa nikisisitiza sana kwamba ligi iliyoanza 1965 haikuwa ya bara bali ya nchi nzima, kwa maana ya bara na visiwani.

Hii ni kwa sababu ndiko hesabu za mataji 29 na 22 ya waje jamaa zinakoanzia.

Wanaosema wana mataji 29 na 22 ya ligi ya bara, wanaanzia kuhesabu yale mataji ya zamani...hilo ni kosa linalotakiwa kukemewa kama pepo.

Yale hayakuwa mataji ya bara, yalikuwa ya Muungano.

Najua hiki ndicho hata wewe kaka Mwaisabula ulikuwa hukijui... ndiyo maana ukakurupuka vile!

Mataji ya kuanzia 1965 hadi 1981 ni ya ligi ya taifa, yaani Jamhuri ya Muungano, siyo bara pekee.

Narudia tena, kaka Mwaisabula hii ilikupiga chenga, na siyo wewe tu...na wengine wote ambao waliamini yale mataji 29 na 22 ni ya bara.

Sasa ukitaka kuijua ligi ya bara ilikujaje, soma andiko linalofuata.

Karibu sana 'Mzazi'
 
Screenshot_20230619-152244.png
KWAKO MCHAMBUZI MKUBWA MWAISABULA - 4

Bosi wangu @mwaisabula_mzazi, ligi yetu imepitia mabadiliko mengi sana ya kimuundo, mfumo na majina, hadi kufika hapa ilipo leo.

Mabadiliko makubwa yalifanyika katika awamu tatu, lakini hata hivyo hadhi ilibaki kuwa ile ile kwamba bingwa wa ligi hii ndiyo bingwa wa nchi na anawakilisha Tanzania kimataifa.

AWAMU YA KWANZA

Ule wakati ambao ligi ilikuwa ikiitwa mashindano ya kutafuta klabu bingwa ya taifa, yaani kuanzia 1965 hadi 1981.

Mengi kuhusu awamu hii nimeshayaelezea sana huko nyuma.

AWAMU YA PILI

Hii ilikuwa kuanzia 1982 hadi 2003. Nimeweka kipande cha andiko linaloelezea kwa kina msimu huo.

FAT ilibadilisha mfumo na muundo wa ligi ya zamani na kuja na mfumo na muundo mpya.

Mabadiliko hayo pia yalihusu jina, kutoka Klabu Bingwa ya Taifa hadi Union Super League, yaani Ligi Kuu ya Muungano.

Bingwa wa Ligi hii alikuwa sawa na bingwa wa ile ligi ya zamani, na alienda kushiriki mashindano ya Afrika.

Mabingwa

Pan African (1)
Yanga (6)
KMKM (1)
Simba (5)
Majimaji (3)
African Sports (1)
Malindi (2)
Pamba (1)

NB:Mwaka 2003 hakukuwa na bingwa kwa sababu ligi ilivunjika.

Katika awamu hii pia zilianzishwa ligi zingine mbili; Ligi ya Bara na Ligi ya Zanzibar.

Kwa hiyo kaka yangu Mzazi, ile ligi ya bara uliyosema mimi siijui, ndiyo nakuelezea kwamba ilianzia hapa.

Ligi ya bara ilishirikisha timu za bara pekee, na ilikuwa ya madaraja, kuanzia la kwanza hadi la nne.

Lengo la ligi hii ilikuwa kupata timu zitakazoenda kushiriki Ligi Kuu ya Tanzania, ambayo iliitwa Union Super League.

Kwa hiyo ligi ya bara ilikuwa sehemu ya ligi kuu ya Tanzania...Ligi ya Muungano!

Mwaka 1997 ligi ya bara ikafanyiwa mabadiliko kufuatia udhamini mnono wa Safari Lager.


Zile timu zilizokuwa daraja la kwanza zikapandishwa hadhi na kuwa Ligi Kuu...ndipo ikaanza Safari Lager Premier League!

Mabingwa wa Bara

Yanga (11)
Simba (6)
Mtibwa Sugar (2)
Coastal Union (1)
Tukuyu Stars (1)

Hii haikuwa ligi rasmi na ndiyo maana mabingwa hawa hawakupata tiketi ya kushiriki Ligi ya Mabingwa Afrika katika miaka hiyo!

Itaendelea....
 
Dakika ya 65

Zakazakazi 5 Simba na Yanga 0

Ajabu ni kwamba Yanga ndio wanaonekana kuumizwa sana na matokeo wakati Simba wamekubali kuwa mpira una matokeo matatu
 
Bas sasa Inabidi TFF waje na data sahihi sasa
 
View attachment 2662353KWAKO MCHAMBUZI MKUBWA MWAISABULA - 4

Bosi wangu @mwaisabula_mzazi, ligi yetu imepitia mabadiliko mengi sana ya kimuundo, mfumo na majina, hadi kufika hapa ilipo leo.

Mabadiliko makubwa yalifanyika katika awamu tatu, lakini hata hivyo hadhi ilibaki kuwa ile ile kwamba bingwa wa ligi hii ndiyo bingwa wa nchi na anawakilisha Tanzania kimataifa.

AWAMU YA KWANZA

Ule wakati ambao ligi ilikuwa ikiitwa mashindano ya kutafuta klabu bingwa ya taifa, yaani kuanzia 1965 hadi 1981.

Mengi kuhusu awamu hii nimeshayaelezea sana huko nyuma.

AWAMU YA PILI

Hii ilikuwa kuanzia 1982 hadi 2003. Nimeweka kipande cha andiko linaloelezea kwa kina msimu huo.

FAT ilibadilisha mfumo na muundo wa ligi ya zamani na kuja na mfumo na muundo mpya.

Mabadiliko hayo pia yalihusu jina, kutoka Klabu Bingwa ya Taifa hadi Union Super League, yaani Ligi Kuu ya Muungano.

Bingwa wa Ligi hii alikuwa sawa na bingwa wa ile ligi ya zamani, na alienda kushiriki mashindano ya Afrika.

Mabingwa

Pan African (1)
Yanga (6)
KMKM (1)
Simba (5)
Majimaji (3)
African Sports (1)
Malindi (2)
Pamba (1)

NB:Mwaka 2003 hakukuwa na bingwa kwa sababu ligi ilivunjika.

Katika awamu hii pia zilianzishwa ligi zingine mbili; Ligi ya Bara na Ligi ya Zanzibar.

Kwa hiyo kaka yangu Mzazi, ile ligi ya bara uliyosema mimi siijui, ndiyo nakuelezea kwamba ilianzia hapa.

Ligi ya bara ilishirikisha timu za bara pekee, na ilikuwa ya madaraja, kuanzia la kwanza hadi la nne.

Lengo la ligi hii ilikuwa kupata timu zitakazoenda kushiriki Ligi Kuu ya Tanzania, ambayo iliitwa Union Super League.

Kwa hiyo ligi ya bara ilikuwa sehemu ya ligi kuu ya Tanzania...Ligi ya Muungano!

Mwaka 1997 ligi ya bara ikafanyiwa mabadiliko kufuatia udhamini mnono wa Safari Lager.


Zile timu zilizokuwa daraja la kwanza zikapandishwa hadhi na kuwa Ligi Kuu...ndipo ikaanza Safari Lager Premier League!

Mabingwa wa Bara

Yanga (11)
Simba (6)
Mtibwa Sugar (2)
Coastal Union (1)
Tukuyu Stars (1)

Hii haikuwa ligi rasmi na ndiyo maana mabingwa hawa hawakupata tiketi ya kushiriki Ligi ya Mabingwa Afrika katika miaka hiyo!

Itaendelea....
jamaa anakuja na dawa taratibu inaingia, mwisho wote tutakubali kwamba 29 na 22 ni vikombe vya mchongo
 
jamaa anakuja na dawa taratibu inaingia, mwisho wote tutakubali kwamba 29 na 22 ni vikombe vya mchongo
Wale critics wamekimbia washaona maswali yao waliyokuwa wanaona ni very reasonable yamejibiwa kirahisi

Saizi hawana uvungu wa kujifichia
 
Maisha yanaenda kasi sana, sasa zile tisheti tutazivalia wapi au kina Hesi walijumuisha na vikombe vyetu vya CAF? Na mbona mtoto wa Mayele anafanana na Diarra?
 
Maisha yanaenda kasi sana, sasa zile tisheti tutazivalia wapi au kina Hesi walijumuisha na vikombe vyetu vya CAF? Na mbona mtoto wa Mayele anafanana na Diarra?
ukiwa mbele za watu jaribu kuficha tabia zingine wewe unaufahamu ukoo wa kina Mayele?
 
Uto wamekimbia mjadala baada ya kuona ukweli hauko upande wao. Msipende kudanganywadanganywa kenge nyie 🤣😂🤣
 
Back
Top Bottom