Zakazakazi: Yanga sio Mabingwa mara 29 na Simba sio Mabingwa mara 22

Zakazakazi: Yanga sio Mabingwa mara 29 na Simba sio Mabingwa mara 22

Anaandika Zakazakazi,

YANGA SIYO MABINGWA MARA 29 NA SIMBA SIYO MABINGWA MARA 22

Hii ni changamoto kwa wadau wote wa soka nchini Tanzania; wachambuzi, waandishi wa habari, mamlaka za soka na serikali kwa maana ya wizara ya michezo na baraza la michezo.

Fanyeni utafiti na mje na majibu sahihi maana siku zinavyozidi kwenda, uongo unakuwa ukweli kwa sababu watu wanaamini yasiyo sahihi.

Ligi ya Tanzania ilianza mwaka 1965 ikiitwa Klabu Bingwa ya Taifa. Hadi mwaka huu, 2023, ni miaka 58. Maana yake kuna mabingwa 58 wanatakiwa kuwepo.

Sasa kama Yanga ni mabingwa mara 29, Simba mara 22 maana yake hawa wawili peke yao wamechukua ubingwa mara 51.

Katika misimu 58, imebaki misimu 7 pekee ambayo wamechukua wengine.

Hao wengine ni wafuatao.

Cosmopolitan -1 (1967)
Mseto -1 (1975)
Pan African - 1 (1982)
KMKM - 1 (1984)
Majimaji - 3 (1985, 1986 na 1998)
African Sports - 1 (1988)
Malindi - 2 (1989 na 1992)
Pamba - 1 (1990)
TZ Prisons - 1 (1999)
Azam FC - 1 (2014)

Jumla 13

Ukijumlisha na zile 51 za Yanga na Simba, unapata 64...inawezekanaje?

Ligi iliyochezwa miaka 58 inakuwaje na mabingwa 64...hesabu za wapi hizo?

Timu zilizotajwa hapo ndiyo mabingwa wa Tanzania wanaotambuliwa na CAF na FIFA, na ndiyo walioshiriki Klabu Bingwa/Ligi ya Mabingwa Afrika katika miaka husika.

Ndiyo maana nilianza kwa kutoa changamoto kwa wadau.

Tembeleeni tovuti za CAF na FIFA muone ni timu zipi ziliiwakilisha Tanzania kwenye Klabu Bingwa/Ligi ya Mabingwa Afrika kuanzia 1965.

UKWELI
Yanga ni mabingwa mara 22 na Simba mara 21.

22+21= 43 - Yanga na Simba
43+13=56 - Jumla (kati ya 58)

NB: Kuna misimu miwili (1970 na 2003) Tanzania hakukuwa na bingwa.

Ndiyo maana unapata mabingwa 56 katika misimu 58.

Itaendelea...

Soma sehemu ya pili hapa

Soma sehemu ya tatu hapa

Soma sehemu ya nne hapa

Soma sehemu ya tano hapa

Polimilai hazisaidii
Wazee wa ukwaju
 
Anaandika Zakazakazi,

YANGA SIYO MABINGWA MARA 29 NA SIMBA SIYO MABINGWA MARA 22

Hii ni changamoto kwa wadau wote wa soka nchini Tanzania; wachambuzi, waandishi wa habari, mamlaka za soka na serikali kwa maana ya wizara ya michezo na baraza la michezo.

Fanyeni utafiti na mje na majibu sahihi maana siku zinavyozidi kwenda, uongo unakuwa ukweli kwa sababu watu wanaamini yasiyo sahihi.

Ligi ya Tanzania ilianza mwaka 1965 ikiitwa Klabu Bingwa ya Taifa. Hadi mwaka huu, 2023, ni miaka 58. Maana yake kuna mabingwa 58 wanatakiwa kuwepo.

Sasa kama Yanga ni mabingwa mara 29, Simba mara 22 maana yake hawa wawili peke yao wamechukua ubingwa mara 51.

Katika misimu 58, imebaki misimu 7 pekee ambayo wamechukua wengine.

Hao wengine ni wafuatao.

Cosmopolitan -1 (1967)
Mseto -1 (1975)
Pan African - 1 (1982)
KMKM - 1 (1984)
Majimaji - 3 (1985, 1986 na 1998)
African Sports - 1 (1988)
Malindi - 2 (1989 na 1992)
Pamba - 1 (1990)
TZ Prisons - 1 (1999)
Azam FC - 1 (2014)

Jumla 13

Ukijumlisha na zile 51 za Yanga na Simba, unapata 64...inawezekanaje?

Ligi iliyochezwa miaka 58 inakuwaje na mabingwa 64...hesabu za wapi hizo?

Timu zilizotajwa hapo ndiyo mabingwa wa Tanzania wanaotambuliwa na CAF na FIFA, na ndiyo walioshiriki Klabu Bingwa/Ligi ya Mabingwa Afrika katika miaka husika.

Ndiyo maana nilianza kwa kutoa changamoto kwa wadau.

Tembeleeni tovuti za CAF na FIFA muone ni timu zipi ziliiwakilisha Tanzania kwenye Klabu Bingwa/Ligi ya Mabingwa Afrika kuanzia 1965.

UKWELI
Yanga ni mabingwa mara 22 na Simba mara 21.

22+21= 43 - Yanga na Simba
43+13=56 - Jumla (kati ya 58)

NB: Kuna misimu miwili (1970 na 2003) Tanzania hakukuwa na bingwa.

Ndiyo maana unapata mabingwa 56 katika misimu 58.

Itaendelea...

Soma sehemu ya pili hapa

Soma sehemu ya tatu hapa

Soma sehemu ya nne hapa

Soma sehemu ya tano hapa
Sasa kmkm na malindi ni bingwa wa bara tangu lini ndio muandishi huyo nae anajiita?
 
Anaandika Zakazakazi,

YANGA SIYO MABINGWA MARA 29 NA SIMBA SIYO MABINGWA MARA 22

Hii ni changamoto kwa wadau wote wa soka nchini Tanzania; wachambuzi, waandishi wa habari, mamlaka za soka na serikali kwa maana ya wizara ya michezo na baraza la michezo.

Fanyeni utafiti na mje na majibu sahihi maana siku zinavyozidi kwenda, uongo unakuwa ukweli kwa sababu watu wanaamini yasiyo sahihi.

Ligi ya Tanzania ilianza mwaka 1965 ikiitwa Klabu Bingwa ya Taifa. Hadi mwaka huu, 2023, ni miaka 58. Maana yake kuna mabingwa 58 wanatakiwa kuwepo.

Sasa kama Yanga ni mabingwa mara 29, Simba mara 22 maana yake hawa wawili peke yao wamechukua ubingwa mara 51.

Katika misimu 58, imebaki misimu 7 pekee ambayo wamechukua wengine.

Hao wengine ni wafuatao.

Cosmopolitan -1 (1967)
Mseto -1 (1975)
Pan African - 1 (1982)
KMKM - 1 (1984)
Majimaji - 3 (1985, 1986 na 1998)
African Sports - 1 (1988)
Malindi - 2 (1989 na 1992)
Pamba - 1 (1990)
TZ Prisons - 1 (1999)
Azam FC - 1 (2014)

Jumla 13

Ukijumlisha na zile 51 za Yanga na Simba, unapata 64...inawezekanaje?

Ligi iliyochezwa miaka 58 inakuwaje na mabingwa 64...hesabu za wapi hizo?

Timu zilizotajwa hapo ndiyo mabingwa wa Tanzania wanaotambuliwa na CAF na FIFA, na ndiyo walioshiriki Klabu Bingwa/Ligi ya Mabingwa Afrika katika miaka husika.

Ndiyo maana nilianza kwa kutoa changamoto kwa wadau.

Tembeleeni tovuti za CAF na FIFA muone ni timu zipi ziliiwakilisha Tanzania kwenye Klabu Bingwa/Ligi ya Mabingwa Afrika kuanzia 1965.

UKWELI
Yanga ni mabingwa mara 22 na Simba mara 21.

22+21= 43 - Yanga na Simba
43+13=56 - Jumla (kati ya 58)

NB: Kuna misimu miwili (1970 na 2003) Tanzania hakukuwa na bingwa.

Ndiyo maana unapata mabingwa 56 katika misimu 58.

Itaendelea...

Soma sehemu ya pili hapa

Soma sehemu ya tatu hapa

Soma sehemu ya nne hapa

Soma sehemu ya tano hapa
Pana vijana hawajui kama palikuwa na ligi ya muungano na bingwa aliliwakilisha Taifa mashindano ya kimataifa. Bahati mbaya hawajisumbui kutafuta wakiamini kila kitu kipo 'google'.
 
Sehemu ya TanoView attachment 2659398

Ukiwauliza wale jamaa kwamba hayo mataji 43 wanayomiliki kwa pamoja ni ya ubingwa wa mashindano gani, watakujibu kuwa ni ligi ya bara.

Hapa ndipo wanapojifichia kwa kuwa hatuna udadisi na tunakosa vitengo vya rekodi, kumbukumbu na historia kwenye taasisi zetu za mpira.

Kimsingi ni kwamba Ligi ya Bara haikuishi miaka mingi kiasi cha kutoa mataji yote hayo.

Ilianza mwaka 1982 na kuisha mwaka 2003...miaka 21 tu. Yanga mara 11 na Simba mara 6!

Sasa wao wanayahesabu mataji haya na kuyachaganya na yale ya ligi ya kwanza ya 1965 hadi 1981, kisha wanahesabu mataji ya ligi ya sasa, ndiyo wanapata 43!

Iwe kwa kutojua au kwa makusudi, hayo ni makosa makubwa.

Ligi iliyoanza 1965 haikuwa ya Bara, ilikuwa ya Muungano na hata vilabu vya Zanzibar vilishiriki, kama nilivyofafanua kwenye sehemu zilizopita.

Kwa hiyo bingwa wa ile ligi ya zamani hakuwa wa bara, alikuwa wa Muungano.

Wao kama wanataka kuhesabu mataji ya bara pekee, basi wahesabu ya 1982 hadi 2003...kwa sababu hiyo ndiyo ilikuwa ligi ya bara.

Ligi iliyoanza 1965 kama klabu bingwa ya taifa, ilikuwa ya muungano na kuanzia 1982, ikabadishwa jina muundo na mfumo.

Jina la kwanza lilikuwa Klabu Bingwa ya Taifa, jina jipya likawa Ligi ya Muungano.

Muundo wa kwanza ulikuwa kuanzia ngazi ya wilaya hadi taifa, muundo mpya ukawa wa madaraja, la kwanza hadi nne, kutokea pande zote mbili za Muungano.

Mfumo wa kwanza ulikuwa kwa mtoano, muundo mpya ukawa wa mzunguko, nyumbani na ugenini na kuhesabu alama.

Lakini licha ya mabadiliko hayo, bingwa alibaki na hadhi ile ile, yaani kutambuliwa na FIFA na CAF na kupata tiketi ya kushiriki Klabu Bingwa/Ligi ya Mabingwa Afrika.

Sasa hawa jamaa wanaacha kuhesabia ubingwa wa ligi ya muungano wa kuanzia 1982 hadi 2003, wanahesabu ubingwa ile ligi ya bara ambayo ilikuwa sawa na mtihani wa moko.

Kwa sababu kwenye hiyo ligi ya Muungano hawakupata mataji mengi hivyo haina maana kwao.

Kwa hiyo wanajifariji kwa kuwa Tanzania One kwenye Moko na kujitangaza walifaulu, kisha wanayaacha matokeo ya mtihani wa taifa kwa sababu walipata Zero!

Itaendelea...
Mkuu, wanahesabu na ngao ya jamii.
 
yaliunganishwa kwa sababu washiriki wa caf cup na wale wa winners cup wote wanashiriki confederation cup.....

mfano kwa tanzania, (tanganyika)

Champions league anaenda bingwa wa ligi,
Winners Cup anaenda bingwa wa ASFC,
CAF Cup anaenda alieshika nafasi ya pili kwenye ligi (kama hajawa bingwa wa ASFC, otherwise wa nafasi ya 3 kwenye ligi)


kwenye muundo mpya
Bingwa na 2nd team kwenye ligi wanaenda CL,..
3rd team na bingwa wa ASFC wanaenda CC....

mpk hapo utagundua waliunganisha winners na CAF cup
Cha kuongezea, CAF wanavyosema hayo mashindano mawili yaliunganishwa, huyo mwenzetu anaangalia tu jambo moja la uwakilishi lakini anasahau pia resources ambazo zilikuwa zinatumika kwenye CAF Cup zikiwemo zawadi ambazo nazo zililetwa katika shindano jipya. Kuna mambo mengi hayazingatii.
 
Ikumbukwe kwamba kombe la klabu bingwa Afrika ilianzishwa mwaka 1965 na kombe la kwanza likitolewa na aliyekuwa rais wa kwanza wa Ghana marehemu Kwame Nkurumah na makao makuu ya Caf wakati huo yakiwa Accre, Ghana.
 
Mbona MNAUMIA SANA????maumivu makali ni sehemu ya KUJIFUNZA...SIWALAUMU
 
Screenshot_20230618-152320.png


KWAKO MCHAMBUZI MKUBWA MWAISABULA - 1

Nianze kwa kutoa heshima kubwa kwako, @mwaisabula_mzazi mchambuzi mkubwa.

Wewe ni mtu muhimu sana kwa soka la Tanzania. Umelicheza, umelifundisha na sasa unaendeleza vijana pale Majimatitu kwa Martin Lumbanga...unastahili maua mengi sana.

Kupata nafasi ya kiufundisha klabu kubwa kama Yanga kunaonesha ni kiasi gani wewe ni mbobevu...saluti kwako mzazi!

Wewe unajua mengi sana, lakini hakuna binadamu anayejua yote. Kwenye hili suala la Ligi yetu, Mzazi nikuhakikishie, nalijua sana zaidi yako...tena mbali mno!

Nimelifanyia utafiti wa kina na wa muda mrefu...sijakurupuka!

Ungekuwa umefuatilia vizuri mfululizo wa makala zangu za awali kuhusu hili jambo, ungejua ni kiasi gani naijua hii ligi ya Tanzania.

Muda bado unao, unaweza kuzipitia, lakini anza na hizi za sasa ambazo sijui zitakuwa ngapi.

Ligi yetu ilianza mwaka 1965 na katika msimu wa kwanza vilitumika viwanja viwili; Ilala Stadium ambao sasa ni Karume, na Tanga Municipal Stadium ambao sasa ni Mkwakwani.

Mechi ya kwanza kabisa ilifanyika uwanja wa Ilala, kati ya Sigara (Tobacco) ya Dar Es Salaam dhidi ya TPC (Tanganyika Plantation Company) ya Moshi.

Ilikuwa Jumamosi ya Mei 29, na TPC ilishinda 2-1.

Kule Tanga, mechi ya kwanza ilifanyika Jumapili ya Mei 30, kati ya Coastal Union na Manchester United, zote za Tanga. Mechi hii iliisha kwa sare ya 2-2.

Ligi hii haikuwa ya Bara, bali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na iliitwa Mashindano ya kutafuta Klabu Bingwa ya Taifa.

Zilitakiwa zishiriki timu kutoka Bara na Visiwani, lakini kwa bahati mbaya timu za Visiwani, yaani Zanzibar, zilishindwa kuja.

Timu zilizoshiriki zikawa SITA tu.

TPC - Moshi
Sigara - Pwani
Yanga - Pwani
Sunderland - Pwani
Coastal Union - Tanga
Manchester United - Tanga.

NB
Wakati huo Dar Es Salaam bado haijawa mkoa. Mkoa ulikiwa Pwani na Dar Es Salaam ilikuwa makao makuu ya mkoa.

Nasisitiza. Ligi iliyoanza 1965 ilikuwa ya Muungano, siyo ya Bara.

Itaendelea
 
Screenshot_20230618-153006.png


KWAKO MCHAMBUZI MKUBWA MWAISABULA - 2

Mzazi @mwaisabula_mzazi, tofauti kati ya Ligi ya Bara na Ligi ya Muungano naijua vizuri sana.

Nadhani wasiojia ndiyo wanaohesabu mataji waliyonayo sasa.

Narudia, Ligi iliyoanza 1965 ilikuwa ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, japo miaka ya mwanzoni timu za Zanzibar zilishindwa kushiriki.

Kutoshiriki kwao hakukuondoa uhalali wa ligi kuwa ya kitaifa kwa sababu milango ilikuwa wazi na hawakuja kutokana na sababu zao, kubwa zikiwa ni za kiuchumi.

Mwaka 1972 timu za Zanzibar ndiyo zikaaza kushiriki.

Hicho kipicha ni cha andiko la mwaka 1973 likizungumzia ligi ya mwaka huo.

Unaiona hapo Ujamaa ya Zanzibar, hii ina maana kwamba ile ligi haikuwa ya Bara pekee.

Na nikuongezee kitu. Nadhani unaikumbuka Nyamagana Thriller, ile mechi ya Yanga na Simba iliyofanyika Agosti 10, 1974 kwenye uwanja wa Nyamagana Mwanza.

Mechi ile ilikuwa fainali ya Klabu Bingwa ya Taifa, na ndiyo mechi ya kwanza rasmi kuzikutanisha Yanga na Simba nje ya Dar Es Salaam.

Sasa mwaka ule, mechi ya ufunguzi iliyofanyika Julai 18, ilizikutanisha timu za Magunia kutoka Moshi dhidi ya Jeshi Zanzibar.

Mechi hii iliyoisha kwa ushindi wa 5-4 kwa Magunia, ilikuwa na msisimko mkubwa kutokana na funga nifukufunge yake.

Yanga walitinga fainali baada ya kuitoa Miembeni ya Zanzibar kwa ushindi wa 2-1.

Ligi hii iliyoitwa mashindano ya kutafuta Klabu Bingwa ya Taifa, ilianza 1965 hadi 1981.

Mabingwa

Yanga (7 - 1)
Simba - (8)
Cosmopolitan (1)
Mseto (1)

Hawa ndiyo mabingwa wa Klabu Bingwa ya Taifa, mashindano yaliyokuwa na sura ya Muungano.

Sasa baada ya hapa, yaani kuanzia 1982, ndiyo mfumo mpya wa mashindano ukaja.

Huo mfumo mpya ndiyo uliokuia kuleta ligi ya bara, ligi ya Zanzibar na ligi ya Muungano.

Soma sehemu inayofuata...
 
Katika hili Yanga na Simba waliungana kutupiga kamba, TFF waje waweke hesabu sawa
 
Katika hili Yanga na Simba waliungana kutupiga kamba, TFF waje waweke hesabu sawa
Hata kama ni makubaliano ila Yanga walikuwa vinara walijimegea keki kubwa kuliko mwenzake
 
View attachment 2661405

KWAKO MCHAMBUZI MKUBWA MWAISABULA - 1

Nianze kwa kutoa heshima kubwa kwako, @mwaisabula_mzazi mchambuzi mkubwa.

Wewe ni mtu muhimu sana kwa soka la Tanzania. Umelicheza, umelifundisha na sasa unaendeleza vijana pale Majimatitu kwa Martin Lumbanga...unastahili maua mengi sana.

Kupata nafasi ya kiufundisha klabu kubwa kama Yanga kunaonesha ni kiasi gani wewe ni mbobevu...saluti kwako mzazi!

Wewe unajua mengi sana, lakini hakuna binadamu anayejua yote. Kwenye hili suala la Ligi yetu, Mzazi nikuhakikishie, nalijua sana zaidi yako...tena mbali mno!

Nimelifanyia utafiti wa kina na wa muda mrefu...sijakurupuka!

Ungekuwa umefuatilia vizuri mfululizo wa makala zangu za awali kuhusu hili jambo, ungejua ni kiasi gani naijua hii ligi ya Tanzania.

Muda bado unao, unaweza kuzipitia, lakini anza na hizi za sasa ambazo sijui zitakuwa ngapi.

Ligi yetu ilianza mwaka 1965 na katika msimu wa kwanza vilitumika viwanja viwili; Ilala Stadium ambao sasa ni Karume, na Tanga Municipal Stadium ambao sasa ni Mkwakwani.

Mechi ya kwanza kabisa ilifanyika uwanja wa Ilala, kati ya Sigara (Tobacco) ya Dar Es Salaam dhidi ya TPC (Tanganyika Plantation Company) ya Moshi.

Ilikuwa Jumamosi ya Mei 29, na TPC ilishinda 2-1.

Kule Tanga, mechi ya kwanza ilifanyika Jumapili ya Mei 30, kati ya Coastal Union na Manchester United, zote za Tanga. Mechi hii iliisha kwa sare ya 2-2.

Ligi hii haikuwa ya Bara, bali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na iliitwa Mashindano ya kutafuta Klabu Bingwa ya Taifa.

Zilitakiwa zishiriki timu kutoka Bara na Visiwani, lakini kwa bahati mbaya timu za Visiwani, yaani Zanzibar, zilishindwa kuja.

Timu zilizoshiriki zikawa SITA tu.

TPC - Moshi
Sigara - Pwani
Yanga - Pwani
Sunderland - Pwani
Coastal Union - Tanga
Manchester United - Tanga.

NB
Wakati huo Dar Es Salaam bado haijawa mkoa. Mkoa ulikiwa Pwani na Dar Es Salaam ilikuwa makao makuu ya mkoa.

Nasisitiza. Ligi iliyoanza 1965 ilikuwa ya Muungano, siyo ya Bara.

Itaendelea
Ok tufanye assumption kuwa mwaka 1965 ligi ilikuwa ya muungano ila timu za Zanzibar zilishindwa kuja.
Swali je baada ya mwaka 1965 ni mwaka upi timu za Zanzibar ziliamua kuja?
Ligi ya muungano halafu timu zishindwe kuja, hapo inaama ligi ya muungano ilikuwa haina umuhimu ni kama bonanza?
 
Ok tufanye assumption kuwa mwaka 1965 ligi ilikuwa ya muungano ila timu za Zanzibar zilishindwa kuja.
Swali je baada ya mwaka 1965 ni mwaka upi timu za Zanzibar ziliamua kuja?
Ligi ya muungano halafu timu zishindwe kuja, hapo inaama ligi ya muungano ilikuwa haina umuhimu ni kama bonanza?
Soma post 273
 
Ok tufanye assumption kuwa mwaka 1965 ligi ilikuwa ya muungano ila timu za Zanzibar zilishindwa kuja.
Swali je baada ya mwaka 1965 ni mwaka upi timu za Zanzibar ziliamua kuja?
Ligi ya muungano halafu timu zishindwe kuja, hapo inaama ligi ya muungano ilikuwa haina umuhimu ni kama bonanza?
1972 team za Zenji zilishiriki ligi ya Muungano
 
Anaandika Zakazakazi,

YANGA SIYO MABINGWA MARA 29 NA SIMBA SIYO MABINGWA MARA 22

Hii ni changamoto kwa wadau wote wa soka nchini Tanzania; wachambuzi, waandishi wa habari, mamlaka za soka na serikali kwa maana ya wizara ya michezo na baraza la michezo.

Fanyeni utafiti na mje na majibu sahihi maana siku zinavyozidi kwenda, uongo unakuwa ukweli kwa sababu watu wanaamini yasiyo sahihi.

Ligi ya Tanzania ilianza mwaka 1965 ikiitwa Klabu Bingwa ya Taifa. Hadi mwaka huu, 2023, ni miaka 58. Maana yake kuna mabingwa 58 wanatakiwa kuwepo.

Sasa kama Yanga ni mabingwa mara 29, Simba mara 22 maana yake hawa wawili peke yao wamechukua ubingwa mara 51.

Katika misimu 58, imebaki misimu 7 pekee ambayo wamechukua wengine.

Hao wengine ni wafuatao.

Cosmopolitan -1 (1967)
Mseto -1 (1975)
Pan African - 1 (1982)
KMKM - 1 (1984)
Majimaji - 3 (1985, 1986 na 1998)
African Sports - 1 (1988)
Malindi - 2 (1989 na 1992)
Pamba - 1 (1990)
TZ Prisons - 1 (1999)
Azam FC - 1 (2014)

Jumla 13

Ukijumlisha na zile 51 za Yanga na Simba, unapata 64...inawezekanaje?

Ligi iliyochezwa miaka 58 inakuwaje na mabingwa 64...hesabu za wapi hizo?

Timu zilizotajwa hapo ndiyo mabingwa wa Tanzania wanaotambuliwa na CAF na FIFA, na ndiyo walioshiriki Klabu Bingwa/Ligi ya Mabingwa Afrika katika miaka husika.

Ndiyo maana nilianza kwa kutoa changamoto kwa wadau.

Tembeleeni tovuti za CAF na FIFA muone ni timu zipi ziliiwakilisha Tanzania kwenye Klabu Bingwa/Ligi ya Mabingwa Afrika kuanzia 1965.

UKWELI
Yanga ni mabingwa mara 22 na Simba mara 21.

22+21= 43 - Yanga na Simba
43+13=56 - Jumla (kati ya 58)

NB: Kuna misimu miwili (1970 na 2003) Tanzania hakukuwa na bingwa.

Ndiyo maana unapata mabingwa 56 katika misimu 58.

Itaendelea...

Soma sehemu ya pili hapa

Soma sehemu ya tatu hapa

Soma sehemu ya nne hapa

Soma sehemu ya tano hapa

Soma sehemu ya sita hapa

Soma sehemu ya saba hapa
Chemsha majani mabichi ya mwarobaini halafu uyaache yapoe; baada hapo chuja maji uyanywe. Matatizo yako yote yatakwisha.
 
Chemsha majani mabichi ya mwarobaini halafu uyaache yapoe; baada hapo chuja maji uyanywe. Matatizo yako yote yatakwisha.
Majibu ya maswali yenu mliyokuwa mnaiza karibia yote yamejibiwa.

Mna lipi la kusema kuuonesha Umma kurwa nyie ni mabingwa mara 29?
 
Back
Top Bottom