Zakazakazi: Yanga sio Mabingwa mara 29 na Simba sio Mabingwa mara 22

Zakazakazi: Yanga sio Mabingwa mara 29 na Simba sio Mabingwa mara 22

lengo la ligi ya muungano ilikuwa ni kudumisha Muungano wetu na kutoa usawa wa kiuwakilishi katika michuano ya kimataifa ya vilabu, hii ni kutokana na Tanzania bara kuwa na ligi yake na Zanzibar kuwa na ligi yake huku upande wa pili (Zanzibar) ukiwa sio mwanachama wa shirikisho la soka barani Africa caf, hivyo kukosa sifa ya timu zake kushiriki michuano ya vilabu bingwa africa na kombe la washindi (ilijulikana hivyo miaka hiyo). Kwa kuwepo kwa ligi ya Muungano ambayo ilikuwa inajumlisha timu 3 zilizomaliza nafasi juu kwenye ligi husika basi timu kutoka Zanzibar nazo zilipata nafasi ya kuiwakilisha Jamhuri ya Muungano kwenye michuano ya CAF.
Kwa hiyo swali langu liko pale pale, timu 3 zilizotoka bara kwenda kushiriki kombe la Muungano, je aliyeshika nafasi ya kwanza katika hao 3 alikuwa anatambulika "Bingwa wa Tanzania Bara" na kupewa kombe au wote 3 walitambulika tu kama wawakilishi wa Tanzania Bara katika Kombe la Muungano?
 
Kwa hiyo swali langu liko pale pale, timu 3 zilizotoka bara kwenda kushiriki kombe la Muungano, je aliyeshika nafasi ya kwanza katika hao 3 alikuwa anatambulika "Bingwa wa Tanzania Bara" na kupewa kombe au wote 3 walitambulika tu kama wawakilishi wa Tanzania Bara katika Kombe la Muungano?
Wa kwanza alikuwa Bingwa wa Tz Bara.
 
changaule
Tate Mkuu
Bila bila

Someni hapo

Kumbe ligi ya muungano ambayo leo hii mnaiona inferior ndio iliyokuwa yenye hadhi kuliko ligi zetu na mmetulia tu
Nililisema hili toka mwanzo. Na pia huu mjadala unawahusu wale waliokuwa wanabeza CAF Cup kwa hoja ya kuwa na timu chache au kuwa ya mtoano. Inaonyesha katika vipindi tofauti, hata ligi yetu ilikuwa na mfumo huo.

Huu mjadala sijapata mzuka sana wa kuutafutia data zake maana najua kuna ugumu wa kuzipata hizi mitandaoni hasa mabadiliko ya ligi yaliyokuwa yanatokea. Kwa hiyo I hope hizi taarifa anazotoa ni sahihi na tutaendelea kuzitumia mbele ya safari.

Ingekuwa vizuri akaandika sasa mwaka kwa mwaka na kueleza mfumo gani ulitumia kupata bingwa katika kila mwaka.
 
Notts County ilianzishwa mwaka 1862 kabla hata ya shirikisho.
Kwenye almost every nation ni lazima kuwe na founding members.

Yaani vilabu vilivyopelekea kuanzishwa kwa FA.


Issue ya Notts County FC Bado sio sababu tosha ya kusema msimu wa ligi wa mwaka 1990/91 ulikuwa sawa na Ndondo Cup kwa sababu tu EPL haikuwa imeanzishwa.
 
64 - 65 ni kwamba ligi ilirasimishwa na bingwa wa kwanza akawa Sunderland...

Kabla ya hapo ligi ilikuwa ikichezwa pasipo urasmi na mabingwa walikiwa wakipatikana...

Jaribu tu kujiuliza timu za Simba na Yanga zilizoanzishwa miaka ya 30, je zilikuwa zipo zipo tu hadi huo mwaka 64/65?
Sasa kukosa urasmi si ilikuwa sawa na ndondo cup.
 
Anaandika Zakazakazi,

YANGA SIYO MABINGWA MARA 29 NA SIMBA SIYO MABINGWA MARA 22

Hii ni changamoto kwa wadau wote wa soka nchini Tanzania; wachambuzi, waandishi wa habari, mamlaka za soka na serikali kwa maana ya wizara ya michezo na baraza la michezo.

Fanyeni utafiti na mje na majibu sahihi maana siku zinavyozidi kwenda, uongo unakuwa ukweli kwa sababu watu wanaamini yasiyo sahihi.

Ligi ya Tanzania ilianza mwaka 1965 ikiitwa Klabu Bingwa ya Taifa. Hadi mwaka huu, 2023, ni miaka 58. Maana yake kuna mabingwa 58 wanatakiwa kuwepo.

Sasa kama Yanga ni mabingwa mara 29, Simba mara 22 maana yake hawa wawili peke yao wamechukua ubingwa mara 51.

Katika misimu 58, imebaki misimu 7 pekee ambayo wamechukua wengine.

Hao wengine ni wafuatao.

Cosmopolitan -1 (1967)
Mseto -1 (1975)
Pan African - 1 (1982)
KMKM - 1 (1984)
Majimaji - 3 (1985, 1986 na 1998)
African Sports - 1 (1988)
Malindi - 2 (1989 na 1992)
Pamba - 1 (1990)
TZ Prisons - 1 (1999)
Azam FC - 1 (2014)

Jumla 13

Ukijumlisha na zile 51 za Yanga na Simba, unapata 64...inawezekanaje?

Ligi iliyochezwa miaka 58 inakuwaje na mabingwa 64...hesabu za wapi hizo?

Timu zilizotajwa hapo ndiyo mabingwa wa Tanzania wanaotambuliwa na CAF na FIFA, na ndiyo walioshiriki Klabu Bingwa/Ligi ya Mabingwa Afrika katika miaka husika.

Ndiyo maana nilianza kwa kutoa changamoto kwa wadau.

Tembeleeni tovuti za CAF na FIFA muone ni timu zipi ziliiwakilisha Tanzania kwenye Klabu Bingwa/Ligi ya Mabingwa Afrika kuanzia 1965.

UKWELI
Yanga ni mabingwa mara 22 na Simba mara 21.

22+21= 43 - Yanga na Simba
43+13=56 - Jumla (kati ya 58)

NB: Kuna misimu miwili (1970 na 2003) Tanzania hakukuwa na bingwa.

Ndiyo maana unapata mabingwa 56 katika misimu 58.

Itaendelea...

Soma sehemu ya pili hapa

Soma sehemu ya tatu hapa

Soma sehemu ya nne hapa
Itoshe kusema hajui hata anacho hoji,K M.K.M na Malindi zimeingiaje kwenye ligi ya Bara?
 
Kwa hiyo swali langu liko pale pale, timu 3 zilizotoka bara kwenda kushiriki kombe la Muungano, je aliyeshika nafasi ya kwanza katika hao 3 alikuwa anatambulika "Bingwa wa Tanzania Bara" na kupewa kombe au wote 3 walitambulika tu kama wawakilishi wa Tanzania Bara katika Kombe la Muungano?
Aliyeshika nafasi ya kwanza anakuwa bingwa wa ligi husika na pia anapewa na kombe. Zanzibar ilikuwa na ligi yao na bingwa anapewa kombe, alikadharika Tanzania bara kulikuwa na ligi yao na bingwa wa ligi ya Tanzania bara (anayeshika nafasi ya kwanza) anapewa kombe
 
Ukiachana na source ya website ya yanga je kwenye vyanzo vingine vinaonesha mara ngapi?
Yanga nayo imekuja kubadilisha siku za hivi karibuni

Angalia kwenye ule uzi wa mwaka jana tuliokuwa tunabishana, waliandika mara 27 lakini miaka ukiihesabu inafika 22
 
Nililisema hili toka mwanzo. Na pia huu mjadala unawahusu wale waliokuwa wanabeza CAF Cup kwa hoja ya kuwa na timu chache au kuwa ya mtoano. Inaonyesha katika vipindi tofauti, hata ligi yetu ilikuwa na mfumo huo.

Huu mjadala sijapata mzuka sana wa kuutafutia data zake maana najua kuna ugumu wa kuzipata hizi mitandaoni hasa mabadiliko ya ligi yaliyokuwa yanatokea. Kwa hiyo I hope hizi taarifa anazotoa ni sahihi na tutaendelea kuzitumia mbele ya safari.

Ingekuwa vizuri akaandika sasa mwaka kwa mwaka na kueleza mfumo gani ulitumia kupata bingwa katika kila mwaka.
Nimeshuhudia utetezi wa nguvu sana kwenye huu mjadala.

Wengine wameonesha kukubali ligi mbili kuunganishwa na kutaka washindi wa ligi zile za mwanzo kabla hazijaunganishwa waendelee kuhesabiwa ushindi wao

Wakati Simba ilipocheza CAF Cup walisema ambayo saizi ni Caf confederation, walisema ile aliyocheza Simba ni Abiora kwakua CAF Confederation Cup imeanza 2004.

Ngoja tuendelee kumsikilizia aje na Makala nyingine huwenda hayo unayoyasema akayaweka
 
Kwenye almost every nation ni lazima kuwe na founding members.

Yaani vilabu vilivyopelekea kuanzishwa kwa FA.


Issue ya Notts County FC Bado sio sababu tosha ya kusema msimu wa ligi wa mwaka 1990/91 ulikuwa sawa na Ndondo Cup kwa sababu tu EPL haikuwa imeanzishwa.
Kwanza unatakiwa ujue kuwa ilianza timu ndio ikaja ligi.

Hiyo ni hesabu rahisi sana.

Kasome historia ya Gongowazi kwenye website yao, utaona wameanza lini na hicho kipindi walikuwa wanacheza michuano gani ambayo ni rasmi.
 
Itoshe kusema hajui hata anacho hoji,K M.K.M na Malindi zimeingiaje kwenye ligi ya Bara?
Soma Makala zote wewe nimeweka hapo.

Hiyo ni continuation bado hajamaliza ndio maana kuna maneno "itaendelea"
 
Yanga nayo imekuja kubadilisha siku za hivi karibuni

Angalia kwenye ule uzi wa mwaka jana tuliokuwa tunabishana, waliandika mara 27 lakini miaka ukiihesabu inafika 22
Ishu sio website, hoja iliyopo hapa na ndio uliyowasilisha wewe hapa kupitia Zaka Zakazi ni kwamba Simba na Yanga ni waongo. Tuje kwenye fact ziweke list ya mabingwa wa ligi kuu ya Tanzania bara kwanzia ianze ni timu zipi zilizochukua kombe ili tuone kama Simba na Yanga record zao zina uongo. Tatizo mnachanganya mambo Yanga wanajinadi ni kuwa ni mabingwa wa ligi kuu bara mara 29. Elewa neno "Tanzania bara"
 
Nimeshuhudia utetezi wa nguvu sana kwenye huu mjadala.

Wengine wameonesha kukubali ligi mbili kuunganishwa na kutaka washindi wa ligi zile za mwanzo kabla hazijaunganishwa waendelee kuhesabiwa ushindi wao

Wakati Simba ilipocheza CAF Cup walisema ambayo saizi ni Caf confederation, walisema ile aliyocheza Simba ni Abiora kwakua CAF Confederation Cup imeanza 2004.

Ngoja tuendelee kumsikilizia aje na Makala nyingine huwenda hayo unayoyasema akayaweka
Caf cup ni tofaut na caf confederation hilo tumeshalieliza sana tena kwa mifano halisi. Africa cup winner's cup ndio ilikuwa ni sawasawa na caf confederation cup na ndio maana mshindi wa Africa cup winner's cup alikuwa akicheza caf super cup dhidi ya mahindi wa Africa cup of champions club. Mbona lipo wazi hilo, hili swala halifanani na hoja uliyomuwakilisha Zaka Zakazi.
 
Ishu sio website, hoja iliyopo hapa na ndio uliyowasilisha wewe hapa kupitia Zaka Zakazi ni kwamba Simba na Yanga ni waongo. Tuje kwenye fact ziweke list ya mabingwa wa ligi kuu ya Tanzania bara kwanzia ianze ni timu zipi zilizochukua kombe ili tuone kama Simba na Yanga record zao zina uongo. Tatizo mnachanganya mambo Yanga wanajinadi ni kuwa ni mabingwa wa ligi kuu bara mara 29. Elewa neno "Tanzania bara"
Fact kupitia chanzo kipi ambacho tunapswa kukubaliana tangu mwanzo?

Mi hapa ndio napoliona tatizo lilipo
 
Yanga bingwa mara 29..

Ifuatayo ni miaka ambayo yanga alichukua ubingwa.

1968, 1969, 1970, 1971, 1972, 1974, 1981, 1983, 1985,1987, 1989, 1991, 1992, 1993, 1996, 1997, 1998, 2002, 2005, 2006, 2007–08, 2008–09, 2010–11, 2012–13, 2014–15, 2015–16, 2016–17, 2021–22, 2022–23

Sources; Mzee Juma Rasheed kibaigwa wa Malindi.
 
Nimeshuhudia utetezi wa nguvu sana kwenye huu mjadala.

Wengine wameonesha kukubali ligi mbili kuunganishwa na kutaka washindi wa ligi zile za mwanzo kabla hazijaunganishwa waendelee kuhesabiwa ushindi wao

Wakati Simba ilipocheza CAF Cup walisema ambayo saizi ni Caf confederation, walisema ile aliyocheza Simba ni Abiora kwakua CAF Confederation Cup imeanza 2004.

Ngoja tuendelee kumsikilizia aje na Makala nyingine huwenda hayo unayoyasema akayaweka
CAF cup sio confederation mshindi wa hilo kombe alicheza super cup 1994?
 
Back
Top Bottom