Zambia, Mwanaume aamua kuvunja ndoa baada ya mke wake kulipia milioni 2 kupiga picha na Chris Brown akimkumbatia na kumbusu

G Tank

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2023
Posts
2,297
Reaction score
8,760


Imetokea Zambia hii, Chris Brown alienda Sauzi kupiga show wiki iliyopita, Mke wa mtu akafunga safari kwenda kumuona, haikuishia hapo akalipia meet and greet, hiki ni kiingilio kwa wale wanaotaka kumuona msanii kule back stage na kupiga nae picha, Chris Brown huwa anatoza dola elfu 1 (shilingi milion 2 na laki 4),

Ilipofika zamu ya mke huyo wa mtu, Chris brown kama kawaida yake alimkumbata kwa nyuma (kumbambia) na kumpiga busu shavuni

Mwanamke kapagawa akaanza kuirusha picha yake mitandaoni kwenye status za whatsapp, anaringishia wenzake kapiga picha na Chris

Wanaume wa kiafrika kwenye mambo ya ndoa hawana dogo, Mume yupo kwenye harakati za kuvunja ndoa,

  • Hakuna mwanamke anaemuheshimu mme wake atamruhusu mwanaume mwengine kumbusu na kumbambia hadharani
  • Kulipia milioni 2 na laki 4 kwa picha ni kukosa nidhamu ya pesa
  • Mwanamke kama unataka uhuru endelea kuwa single au mchepuko, huna haja ya ndoa
 
Wanaume tukiendelea na misimamo kama hii wanawake watanyoka na kutulia
 
Kwani ingekuwa ndio mimi ungemind mpenzi wangu? Mdakuzi
Maana mimi pia ni shabiki wa CB.
 
Na mume aliagwa kabisa kwamba mke anaenda owenye Show ya CB SA?
Na yeye akatoa greenlight?
Kama hapana akirudi na wewe anakuta haupo, huo muda wa talaka ataomba yeye
 
Mbaya zaidi unakuta hata hela aliyotoa kwa CB alichukua kwa mumewe.
 
Mwanamke ana sura nzuri sana. Lijamaa Lina vidole vya mikono kama shetani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…