Zitto ataka wabunge wote walioko Dodoma wawekwe kwenye karantini

Zitto ataka wabunge wote walioko Dodoma wawekwe kwenye karantini

Habari kutoka Bungeni Kama ilivotolewa na Naibu Spika Tulia ya kwamba kuna Mbunge mmoja amepatikana na maambukizi ya Covid-19 zinasikitisha,zinatisha na zinanyong'onyesha katika mapambano dhidi ya Covid-19!

Kabla ya Bunge kuanza watu walishaingiliana Bunge liahirishwe kutokana na tishio la Covid-19. Lakini Spika Ndugai alikuja na hoja dhaifu za kuwa ATI Kuna mikakati imara itakayo wahakikishia Wabunge kuwa watakuwa salama wa salimini.

Hata baada ya Bunge kuanza Kuna Wabunge wa Upinzani kina Mh.Mbowe.Lema, Halima Mdee. Mch. Msigwa na Matiko WALISHAURI WABUNGE WAPIMWE KWANZA ILI KUJUA AFYA ZAO KABLA YA KUENDELEA NA KIKAO. Siku zote Wapinzani hata wakiwa na hoja yenye mashiko inawekwa kapuni.

Sasa Basi kwa Hali hii Mhe. Job Ndugai Spika wa Bunge la JMT na Tulia Ackson Naibu wa Spika mpigieni simu Rais Magufuli kumtaarifu kuwa maji yamezidi Unga na Ni LAZIMA BUNGE LIAHIRISHWE MARA MOJA NA WABUNGE WOTE WAPIMWE COVID-19 NA WAENDE QUARANTINE YA SIKU 14.

Nje ya hapo ni kutaka kuliangamiza Taifa kwa UZEMBE ulio wazi na dhahiri na hii mtawajibika mbele za Mungu na Watanzania wote.

Nawasilisha.
supika tu ajiangalie sana Corona ni mahiiri Kama Messi ndani ya 18 kwenye umaliziaji, haikukosi na haikupi nafasi ya kurudi India
 
Vipi ndugu Zitto ka tweet chochote kuhusu kifo cha mama mchungaji? Hata RIP?

Sent From Galaxy S9
 
Ukiacha wabunge wa upinzani ambao Wapo pale kujaribu kutafuta upenyo wa nafaai ya kuwasemea watz.....maccm yapo pale kwa ajili ya posho tuuu........
Sasa hebu washauri waende karantini uone watakavo ng'aka.....
Eti kutafuta upenyo wa kuwasemea wananchi [emoji23][emoji1787][emoji2960] si wangetowa posho zao kuwapa wanainchi hata majimboni kwao hawawapi msaada hao wanainchi wao wapo pale kwa ajili ya matumbo yao na mwenyekiti wao Ni mradi wake hao wabunge umesahau anavyo wakata wabunge wake posho zao kwa ajili ya Sacco's yake [emoji1787][emoji23]
 
Yaani na uheshimiwa wangu huu,niwekwe karantini?..
Aah, wapi,ikibidi nitaji isolate lakini sio nikachanganywe na common people's,over my dead body....
 
Lema aliwaambia ni aibu kwa viongozi wa juu wa nchi kutembea na kukaa sehemu hatarishi katika kipindi hiki akitolea mfano. Rais anakunywa kahawa na wananchi huko mtaani; Spika na naibu wake; waziri mkuu; mwanasheria mkuu; waziri wa mambo ya ndani wote wako bungeni na still Mbowe alisharipoti familia yake kuugua ugonjwa wa Corona.

Hao viongozi wa juu walioko Bungeni wakiukwaa ni raisi kuwaambukiza jaji mkuu..makamu wa rais..rais mwenyewe...mkuu wa majeshi..IGP..

Kibaya zaidi bado wakuu wengine wa mikoa wanakusanya watu na wao pia wanakutana na mawaziri wenye uwezo wa kuwaambukiza wakuu wa vyombo muhimu
 
Hivi Mdee si alishauri wabunge wote wapimwe,wazo halikutekelezwa?

Sent using Jamii Forums mobile app
Tatizo hoja zenye mantiki zinazotolewa na wapinzani zinaishia kwenye droo kisa tu ni mpinzan katoa hoja, wakt hoja za ovyo ovyo za kina kibajaji na msukuma ndio zinazopewa kipaumbele na wabunge wa ndio wakiongozwa na ndungai

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo viongoz wetu wanataka mpaka serekal iseme ndio wajitenge utakuta zito to katoa io hoja alafu serekal isipo waweka karantin na yeye hato kaa karantin ataendelea ku swampa
Ujumbe wake huu hapa chini kupitia twitter:

Wabunge wote mliopo Dodoma muwekwe karantini, mpimwe na mfuatiliwe ( contact tracing ). Minister Mwalimu there shall be no two set of laws - for MPs and for the people. Wabunge watengwe, wapimwe na wafuatiliwe. Tulishauri toka mwanzo kuwa Bunge lisiendelee na vikao. Ni hatari


Sent using Jamii Forums mobile app
 
soma na hii, google hii:Event 201

utashangaa mengi sana。
 
Ujumbe wake huu hapa chini kupitia twitter:

Wabunge wote mliopo Dodoma muwekwe karantini, mpimwe na mfuatiliwe ( contact tracing ). Minister Mwalimu there shall be no two set of laws - for MPs and for the people. Wabunge watengwe, wapimwe na wafuatiliwe. Tulishauri toka mwanzo kuwa Bunge lisiendelee na vikao. Ni hatari


Halafu unakuta MISUKULE YA CCM inatamba na kupigapiga meza na kupayuka ati, "SERIKALI YA CCM NI SIKIVU NA MAKINI" Non-sense!!!
 
Siioni faida ya Bunge kwa sasa. Lifungwe tu.

Ummy Mwalim hata siku moja hajaonesha mfano kuvaa burqa (barakoa) utafikiri kishajipangia kuwa yeye corona hawezi kumpata.

Ulevi wa madaraka.
 
Kwani haiwezekani kuendesha vikao vya Bunge online?

Tuseme ni uzuzu, ujinga na Upumbafu wa Serikali hii jeuri ya CCM isiyotaka kusikia ushauri na maoni ya Watz!

Tumeshuhudia Waziri Mkuu akifanya mikutano/vikao na Ma RC&DC kwa VIDEO CONFERENCE na inawezekana...!!!

Lakini kwa vile hii ni SERIKALI ya watu wenye kuji-mwambafy na kibri CCM wanafanya maksudi ATI kuwakomoa Wapinzani...!!
 
Back
Top Bottom