Mh.Samia ebu jaribu kuvaa ujasiri,,,achana na akina Sirro wanakuchafua ni miongoni mwa watu wanaoamini mifumo dume,wanakupigia saluti kwa sababu ni sheria tu!!! Ila wanakudharau kama hulijui hili basi lijue,Mtoe ndg Mbowe Magereza na Ushirikiane nae atakusaidia mambo mengi!! Ni bingwa wa siasa za aina zote,,mbali na hilo utaendelea kulalamika usipate msaada ndani ya chama chako maana wamejaa wanafiki ndo hao unaosema wanakuangushia jumba bovu,,,amini mwanzoni ulikuwa umejipatia mtaji mkubwa wa kisiasa kutoka kwa mashabiki wa upinzani hasa chadema ,,wahuni ndani ya chama chako wakatafuta mbinu ya kukunyang'anya mtaji huo wakamkamata Mbowe ili uchukiwe na wameelekea kufanikiwa,,,ebu shtuka mama!! Wapinzani ndo walikuja na kauli mbiu ya "MAMA ANAUPIGA MWINGI" Jiulize toka akamatwe Mbowe neno hilo unalisikia!!!? Wahuni wanataka wakugombanishe na kila kundi ..Usiogope maneno kama katiba mpya kutana na wapinzani myajenge.....Mama nakuhurumia kwa jinsi wanafiki walivokuzunguka ndani ya chama hukutakiwa kugombana na Chadema maana utajiongezea presha,,Chadema ilimpeleka puta Magufuli na udikteta wake mpaka akanyoosha mikono pamoja na matumizi makubwa ya vyombo vya dola..Chadema itakuumiza mama chagua kushirikiana nayo achana na Mbowe.