Zitto Kabwe asema Kikwete alimwambia CCM hakina muda mrefu madarakani na kumshauri abaki upinzani. Aliahidiwa uwaziri wa fedha iwapo angejiunga CCM

Hakika akili zilikuwa zimewaruka kichwani.
Kwa hiyo ni kwa msingi wa ushauri huo wa Kikwete, Zitto akaanzisha chama haraka ili achukue nafasi ya CCM iliyokuwa mahututi?

Zitto ndani ya CHADEMA ulikuwa ni mradi wa kuiangamiza CHADEMA.
 
Kumbe biashara ya CCM kununua wapinzani ilianza kitambo sana?
 
Watale tulotumia muda wetu kujifunza propaganda hatuoni mpya hapo
 
Tulistuka mapema sana
Ni kama mna roho ya paka.
Kuna msemo unasema paka ana "maisha tisa",... najuwa tafsiri hii si rasmi, lakini nnina hakika naeleweka.
Chama kimepita kwenye misukosuko ya kutisha sana; lakini hofu yangu kubwa ni kwamba mtu asiyekuwa na uwezo kama Samia ndiye anakuja kuwamaliza. Inashangaza sana!
 
Samia aweza kuwa ndio Rais wa mwisho kutokea ccm , hana uwezo wa kumaliza Chadema , vinginevyo atamalizika yeye kama Sizonje
 
Samia aweza kuwa ndio Rais wa mwisho kutokea ccm , hana uwezo wa kumaliza Chadema , vinginevyo atamalizika yeye kama Sizonje
Mmmmh. Mki'survive' safari hii huenda hamtapotea tena.

Sitegemei kamwe kwa kada mwaminifu wa chama kama wewe kuona hatari inayo wanyemelea mapema hivi. Mtakuja kustuka kukisha kucha, na wakati huo 'stori' zitakuwa nyingine kabisa. Kirusi cha Samia tayari kimo damuni mwenu, subirini tu kiwamalize, au kwa bahati tu mwili wa chama chenu kiote usugu dhidi ya kirusi hicho. Lakini siku ndiyo zinayoyoma hizo.
Hili tuliachie hapa mkuu wangu 'Erythro.'
 
Hahaha mama akawapumbaza na juisi za ikulu wakawa wanakenua haooo ,,baadae wanashtuka wamepigwa banzi la kisogoni wakigeuka hawaoni mtu ,,,walijua wanapambana na watu wa mwendazake kumbe nao wanatumika tu
 
Mama hana uwezo huo , alichoweza ni kuuza Bandari kwa Wajomba zake
 
Hahaha mama akawapumbaza na juisi za ikulu wakawa wanakenua haooo ,,baadae wanashtuka wamepigwa banzi la kisogoni wakigeuka hawaoni mtu ,,,walijua wanapambana na watu wa mwendazake kumbe nao wanatumika tu
Inabidi kucheka, ingawaje haya ni mambo mazito sana yanayohusu hatma ya taifa letu.
Nimekuelewa jinsi ulivyoliwasilisha hili.
 
Sina sababu ya kubisha Zitto anasema ukweli.

JK is pro talent hata Muhongo, Matarigio na Matindi kawarudisha yeye Tanzania na wengine kadhaa waliokuwa wanapigiwa kelele na jamii ndani ya Tanzania ni talent aliwapa nafasi.

The sad truth japo alikuwa anawapa so called talent nafasi alifanya ivyo kwa milio yao kushinda uwezo wao halisi.

Zitto hana sifa za kuwa waziri wa fedha kuna watu more qualified kumshinda yeye Tanzania wengi tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…