Zitto Kabwe: Watu wazima kujadili Milioni na Bilioni ni kukosa kazi za kufanya

Zitto Kabwe: Watu wazima kujadili Milioni na Bilioni ni kukosa kazi za kufanya

Yaani huyu kijana Zito ni moja ya watu kuzaliwa kwao Tanzania ni bahati mbaya sana. Anazibia vijana wengi mno kwa mawazo yake finyu. Kipindi cha Dkt Magufuli alikuwa ni kutukana tu kwenda mbele na mpaka kifo aliendelea kumdhihaki. Ma mpaka alifikia hatua ya kufurahia kwa kuzusha kifo cha Dkt Magufuli kipindi kile kule rais Dkt Magufuli alipopata dharula, yeye akaposti picha za kumpongeza Mama Samia kuonesha furaha yake kwa kifo cha Dkt Magufuli. Leo amekuwa muungaji wa kila jambo kupitia mgongo wa Dini. Ila ngoma bado mbichi. Tunahitaji taifa huru kiuchumi na fikra.
 
Hii nchi ngumu sana, mtu anakataza watu kujadili kitu ambacho yeye mwenyewe anakijadili.

Hadi anaandika haya si inamaana na yeye yumo kwenye hao anaowaita wamekosa kazi?
Labda yeye anajidhania siyo mtu mzima, hivyo ana ruksa ya kujadili.
 
Mi nashangaa watu kushupalia kosa la m na b
Lazima ushangae kwa sababu huna unalolijua. Kuna tofauti kubwa mnooo kuwaambia wana nchi una dola bilioni 6 VS dola milioni 6... Na kama umekosea si usahihishe basi Mara moja??
 
Sioni tofauti ya akili yako mbovu na ya Zitto. Kwa hiyo siku hizi bilioni ni Sawa na milioni? Yaani ukitaka kusema milioni unaweza tu kusema bilioni ukaeleweka?
Halafu cha ajabu zaidi ni kuwahutubia watanzania kwa dola ya kimarekani badala ya shilingi ya kitanzania...
 
Ila kusema ukweli chadema wana hoja kipumbavu sana jamani!

Yani huwa wanshupalia vitu vya kijinga mno
 
Kwahiyo Zitto Kwa Akili zake Timamu anaona Hamna Haja Ya Kujadiri kati ya Millioni na Billioni? Eeeeh Ndio maana Sio Mbunge!

Zingekuwa ni ‘KURA’ Je asingeona Umuhimu wa Kujadiri?
Wenye mapenzi mema na nchi hii msinhepaza sauti wananchi wangeendelea kudanganywa kwamba nchi yao ina akiba ya fedha za kigeni kuliko Japan.
 
We umeishia darasa la ngapi?
Yule Msukuma Mwendazake aliishia la ngapi wakati aliposimamisha msafara Dumila aliweka mhindi wa kuchoma sikioni na simu aliyopigiwa akiitafuna?
Sukuma Gang acheni kumuandama mama tafuteni la kukosoa
 
jamaa yako badala alazimishe msemaji wa serikali atoe ufafanuzi eti yeye ndio anawatolea ufafanuzi kwa niaba yao

Zitto kageuka msemaji wa serikali

Zitto anajipendekeza aisee mpaka anatia kinyaa

Kana kwamba haitoshi, eti anajipa mamlaka ya kuamulia watu wajadili kitu gani na kitu gani wasijadili.

Ndio maana wanasiasa na viongozi wengi kama sio wote wamezitelekeza ID zao hapa. Hawawezi hata kidogo kutetea au kujenga hoja wakapigwa maswali na kujibu kwa staha.

Ikulu yenyewe wameamua kutolea ufafanuzi eti yeye aliona sio jambo la kujadili.
 
Awamu hii zito kabwe hata sio mpinzani tena bali ni chawa wa mama samia
 
Hivi Kiongozi unasoma hotuba unajiamini Nini na kilichomo
 
Maandiko na matamshi ya rais kwamba nchi yetu Ina reserve ya bilioni 6 nuktakadhaa Dola za kimarekani ,si jambo dogo Kama Zitto anavyo sema , Ni vyema Kama Kulikuwa na makosa ikulu ije irekebishe mbele ya vyombo vya Habari kama ilivyo tangazwa kwenye vyombo vya Habari.


Lakini pia Kuna wasiwasi mkubwa ju ya maelezo ya rais kuhusu takwiimu za mufumko wa bei ya vitu nchini ,rais kasema ni 2-3 % lakini kiuhalisia mtaani mufumko wa bei ni mkubwa sana Kati ya 20-40 % ndani ya mwaka.
Zitto hajitambui, kimshahara cha mchongo anachopokea kila mwezi kutoka kwa Mwinyi na Samia ndo kinampumbaza, na kwani ni mara ya kwanza?
 
Back
Top Bottom