Pre GE2025 Zitto: Tumepata Taarifa Nondo yuko Kituo cha polisi Gogoni, Tumefika tumekuta gari inabadilishwa Plate namba

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Falsafa ya Plato kuhusu philosopher kings inatufundisha kuwa viongozi bora ni wale wenye akili kubwa, maarifa, na maadili mema. Plato alisisitiza kuwa uongozi bora unapaswa kuwa mikononi mwa watu wenye hekima, wanaotanguliza maslahi ya umma badala ya matakwa binafsi. Watu wajinga, wapenda mali, na wasiokuwa na maadili hawastahili kushika madaraka, kwa sababu wanaweza kugeuza nafasi hizo kuwa majukwaa ya ukandamizaji, ulafi, na ubadhirifu wa rasilimali za taifa.

Hali halisi mara nyingi imeonyesha jinsi wajinga wanavyoweza kushika madaraka na kutumia vibaya mamlaka yao. Badala ya kuzingatia maendeleo ya jamii, viongozi wa aina hii huzingatia kulinda maslahi yao kwa gharama yoyote. Matokeo yake ni kwamba wanatumia vyombo vya dola kama polisi na usalama wa taifa kutekeleza mauaji, utekaji, na vitendo vya kikatili dhidi ya wale wanaowakosoa, kuwashauri, au kushindana nao kwa njia za kidemokrasia. Kwao, madaraka ni njia ya kujilimbikizia mali na kuhujumu haki za wananchi badala ya kuboresha maisha yao.

Matumizi ya vyombo vya dola katika vitendo hivi vya kikatili huwa na ukomo. Historia imetufundisha kwamba vyombo hivi, baada ya muda, huanza kuchoshwa na jukumu la kinyama la kuwakandamiza wananchi, hasa pale wanapolazimishwa kuwaua au kuwadhuru watu wao wa karibu kwa faida ya viongozi wachache. Wakati mwingine, wanapoanza kufahamu "utamu" wa madaraka kupitia nafasi zao za kiutendaji, maafisa wa vyombo vya dola huanza kugeuka dhidi ya waliowatuma, wakitafuta nafasi za kushika madaraka wenyewe.

Hali hii mara nyingi huchangia mapinduzi ya kijamii na kisiasa. Vyombo vya dola vinapopoteza imani kwa viongozi wanaowatuma, na wananchi wanapochoshwa na ukandamizaji, kunazuka hali ya machafuko ambayo mara nyingi huishia katika mabadiliko ya kiutawala kupitia njia za nguvu au mapinduzi ya kiraia.

Kwa sababu hizi, ni muhimu kuhakikisha kuwa madaraka hayashikwi na wajinga au watu wenye maslahi binafsi pekee. Jamii inapaswa kuwa na mifumo madhubuti ya uwajibikaji na maadili, kuhakikisha kuwa viongozi ni watu wenye hekima, maono, na nia ya dhati ya kutumikia wananchi. Ni muhimu pia kudhibiti matumizi ya vyombo vya dola ili viendelee kuwa walinzi wa raia badala ya chombo cha kuendeleza ukandamizaji na ubinafsi wa wachache. Katika kufanya hivyo, tunaweza kujenga jamii yenye haki, maendeleo, na utulivu wa kweli
 
Una sOhida ya kimalezi na utachelewa kupata mtaendeleo ya uhakika kwasababu yan neno kutake risk kwako ni msamiati mgumu sana .Ina wezeufakana umetokea
1.Kwenye familia masikini sana
2.Umekulia kiijijini zaidi kuliko mjini
3.Elimu yako haijakusaidia na wala hukuwai kusoma historia zozote za UKOMBOZI


Nikuulize

Unajua chohote kuhusu namna Tanganyika ilivyopata Uhuru wake?
Unajua ni watu wangapi walikufa wakatika wa kupigia Uhuru ?

Una Elimu yoyote kuhusu vibaraka wa Wakoloni kwa Watanganyika?

KWANINI ULIENDA SHULE BABA YAKO HIZO HELA ANGENUNUA MASHAMBA
 
Exactly.
 
Mama mwenyewe anaogopa maaskari hawezi kutoa hata tamko kukemea, Sana Sana anawatetea na kukemea WAATHIRIKA Hulu akiwasifia mapolisi
 
Hakushinda.

Kaongo hako kajamaa.

Anyways siasa zina mambo mengi ikiwa ni pamoja na public sympathy.

Mimi huwezi nidanganya bwana mdogo maana huwa ninafahamu mambo from the ground.
Hakuna cha public sympathy,soma hapa Abdul Nondo: Kiongozi wa wanafunzi Tanzania ashinda kesi ya 'kujiteka' - BBC News Swahili kwamba BBC walidanganya umma?,unakuwa miongoni mwa wa puuzi ,tukiangalia kwenye kitabu cha kumbukumbu Za hukumu Za kesi mbalimbali(kipo kwenye tovuti ya Judiciary) una uhakika tutaona kwamba alikutwa na hatia?. Kuna haja yakupunguza ujuha na masihara
 

Attachments

  • C5FB7AE7-B0C4-49B1-8D60-871F494B703E.png
    4 MB · Views: 4
Kama asingelihusika kwa namna moja ama nyingine, tungelisikia hata akifokafoka!

Kupiga kimya inamaanisha anahusika ama anakubaliana na huo uozo.
 
Mi
Mi nazani wanaume wote tulioko upinzani, tuwe tunambea na panga au kisu.maana huu ni ujinga!! tutauwawa mpaka lini?
 
Huyu dogo aliwahi jiteka lakini.

Alikuwa na kesi Iringa pale mahakama ya wilaya.

Kajinga flani hivi.
Akili za ki_ccm hizi. Ila haishangazi hii statement Toka kwako, ni ule upuuzi aliowamezesha yule dikteta kichaa mwendakuzimu maana yeye alimteka Nondo na kumsingizia sio Raia. Sasa ule upuuzi ndio uko kichwani Mwako mpaka Sasa. Wapumbavu sana nyie jamaa.
 
Duh,
Wanaolipwa kwa kodi za wananchi wote ili kulinda usalama wa raia na mali zao ndo wamegeuka kuwa hatari yenyewe!!!

Tlaatlaah Lucas Mwashambwa
Njooni huku, wanyonge wamefikiwa.
Gentleman,
huyo kijana anafahamika kwa ujanja ujanja wa kujipatia fedha au simpathy kwa jamii,
.Hata hivyo hatuwezi kupuuza au kuvumilia aina hii ya matukio yenye kuibua hisia na taharuki kwa jamii,

wahusika watabainika soon, na kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

ni muhimu ustahimilivu na subra vikachukua mkondo wake 🐒
 
Acha unaa ,hujui kama ile kesi alishinda,baada ya polisi kushindwa kuithibitishia mahakama,tusiwe wapuuzi kwa maisha na haki Za wenzetu zinaznyang’anywa kwa nguvu
Usimshangae huyo jamaa. Ni mfuasi wa yule kichaa dikteta mwendakuzimu. Aliwalisha sumu mbaya sana Hawa wafuasi wake, kiasi cha kuona sawa watu wakiuawa TU kama mende wanaozurula ndani ya nyumba.
 
Bro, kusema upinzani waache siasa, ni kuhalalisha vitendo hivi vya kishenzi. Let's fight for our right of existence.
 
Raia namba 1 anasemaje
 
Zitto naye ni mmoja wa watu ambao wamekuwa kimya huku wapinzani wenzake wa ChaDeMa wakifanyiwa Ukatili.
 
Listen mkuu, kwa hali ilivyosasa kilichobaki ni watekaji, watesaji na wauaji kupimiwa kadri wanavowapimia wengine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…