Kumekuwepo na taarifa kwenye mitandao ya kijamii lakini pia gazeti la Mwananchi limeandika kuwa Serikali ya Marekani imewawekea vikwazo wanasiasa wanne wa Kenya pamoja na familia zao akiwemo Naibu Rais wa Kenya, Rigathi Gachagua baada ya kupata taarifa kuwa wanasiasa hao walipanga na kufadhili vurugu wakati wa maandamano ya Jumatatu iliyopita.
Wanasiasa wengine katika orodha hiyo ni pamoja na Waziri wa Uwekezaji, Biashara na Viwanda, Moses Kuria, kiongozi wa walio wengi katika Bunge la Kitaifa, Kimani Ichungwa na Mbunge wa Kiharu, Ndindi Nyoro.
Ukweli wa taarifa hii upoje?