750k(take home) ni mshahara unaweza kumfanya mtu aishi kidogo bila wasi hapa Bongo?

750k(take home) ni mshahara unaweza kumfanya mtu aishi kidogo bila wasi hapa Bongo?

Je una familia, usafiri, unapanga? All factors included.. yote kwa yote inatosha akili kumkichwa. Nikiangaliaga security guard analipwa 130k kwa mwezi na ana familia ndio huwa naona budget ni wewe mwenyewe! Kuna watu viwandani kwa siku anapata elf 7, kuna wale saidia mama ntilie kwa siku elfu 3 mpaka 5 na maisha yanasonga!
 
Tujaribu hapa mwenye familia saiz ya kazi

Mchele kg2 Tshs 7000
Unga kg1½. Tshs 3000
Mboga na viungo 10000
Kodi na umeme. 5000
Jumla 25000/-

25000 x 30 = 750,000/-

Ukiishi maisha hayo utakosa nauli tuu ya kwenda kazini ila hayo ni matumizi makubwa kwa siku nimeweka maximum ila kikawaida matumizi huwa 10,000/- had 15,000// perday ni sawa 450000/- chakula tuu baki 300,000/-
 
Kwa nyanda za juu upo sahihi mkuu ila kwa Singida hapana aisee maisha ya Singida ni shida kuna Tatizo kubwa la maji na chakula na ukame ni mkubwa sana kule ,nimeishi Singida miaka mingi sana ,mambo ya kula ugali wa mtama,mihogo na viaz vitamu kila siku yaliboa sana,kitu ambacho ahueni Singida ni mifugo kama mbuzi na kuku bei yake n ndogo sana lakini kwa maisha ya kawaida Singida ni gharama

Umetumwa uje uichafue Singida [emoji276]
 
Wakuu nilikuwa nauliza tu kama 750k ni takehome inayoweza kumfanya mtu aishi kidogo standard life.

Maana isikute nadharau kumbe naweza kufanya kitu.
Mshukuru Mungu kwa kila jambo, pesa uipatayo kwa jasho lako wewe unapaswa uipangilie utaitumiaje, ili itoshe wewe mwenyewe kuna vitu ujikataze na kuna vitu ujikubali na ujipangie mwenyewe malengo yako ndio kanuni kubwa katika maisha.

Kumbuka daima hakuna pesa wala mshahara wa kumtosheleza mwanadamu. Mtumainie Mungu na umtangulize katika mipango yako ya kila siku, Barikiwa sana.
 
Kwa nyanda za juu upo sahihi mkuu ila kwa Singida hapana aisee maisha ya Singida ni shida kuna Tatizo kubwa la maji na chakula na ukame ni mkubwa sana kule ,nimeishi Singida miaka mingi sana ,mambo ya kula ugali wa mtama,mihogo na viaz vitamu kila siku yaliboa sana,kitu ambacho ahueni Singida ni mifugo kama mbuzi na kuku bei yake n ndogo sana lakini kwa maisha ya kawaida Singida ni gharama
Uliishi Singida ipi mzee? Labda hapo town ambapo hamlimi chochote ila ndani ndani huko Mkalama vyakula vya kumwaga sana. Karanga, viazi vitamu, alizeti, mahindi, mtama n.k vyote vinalimwa!
 
Kama una familia na unalipa zile bills mfano kodi chakula malazi kila kitu kinatoka hapo kwenye uo mshahara basi hamuna kitu utasave
Unasave vizuri tu, pamoja na vyakula kupanda bei
Familia ya watu 4
Mume, mke, watoto 2

Mchele 90k
Unga 60k
Maharage 20k
Nyama 20k
Umeme 30k
Gesi 50k
Mengineyo 200k
Kodi 150k
Jumla 620

Baki 130k
 
Tujaribu hapa mwenye familia saiz ya kazi

Mchele kg2 Tshs 7000
Unga kg1½. Tshs 3000
Mboga na viungo 10000
Kodi na umeme. 5000
Jumla 25000/-

25000 x 30 = 750,000/-

Ukiishi maisha hayo utakosa nauli tuu ya kwend kazin ila hayo ni matumiz makubwa kwa siku nimeweka maximum ila kikawaid matumiz huw 10,000/- had 15000// perday ni saw 450000/- chakula tuu baki 300,000/-
Familia ya watu wangapi hiyo wanayokula mchele kilo 2 na unga kilo 1.5 kwa siku?

Nyie watu mnaishi Mars au?
 
Mshahara ni budget...ukipokea 750k kwa mwezi matumizi yako hayatakiwi yapindukie 15000 kwa siku. Utafanyaje ili ukutoshe? Hakikisha kwanza unaweka shehena ya nafaka ndani, nunua unga kg 10, mchele kg 10 ,ngano kg 10, sukari kg 5, maharage kg 7-10 na mafuta ya kupikia atleast 5litre na gesi inategemea na ujazo ila ule mtungi wa elfu 55-60 unakutosha kumaliza mwezi-miezi miwili.

Mbogamboga jitahidi uwe unapitia sokoni kununua maana kuna unafuu kiasi, ukipata sado zako mbili za viazi, Dagaa kg 2-3, vitunguu kg 2-3, viazi vitamu au ndizi mbichi. Hapa bajeti ya kula mwezi mzima humalizi laki na 20 ikiwa una familia ya mke na watoto 2-3.

Jitahidi kukaa maeneo ambayo ni karibu na kazi! Sio unafanya kazi posta halafu unaishi mpiji magoe ndani ndani huko...nauli tu kwa siku unamaliza zaidi ya 6,000. Ishi sehemu ambayo utatumia gharama ndogo ya sh 500 kwenda na 500 kurudi. Epukana na kupenda sana kutumia bodaboda kwani zinacost. Usiishi maisha ya kujinyima sana kwa wiki jitahidi ule hats nyama mara 2. Epukana na anasa za ulevi wa pombe,kamari na wanawake. Hapo utaona jinsi utakavyosave zaidi ya 300k kila mwezi.

Kama ni bachela jitahidi sana uwe na life skills kama kujua kupika, kuosha vyombo,kufua nguo zako n.k utasave pesa nyingi sana unazoenda kuzipotezea migahawani.

Kama umepanga chumba kimoja basi jitahidi kodi isizidi 50k kama ni vyumba viwili isipindukie 100k kwa mwezi
 
Back
Top Bottom