Aache kazi private anakolipwa 1.6m au aende government atakapolipwa laki 7.6?

Aache kazi private anakolipwa 1.6m au aende government atakapolipwa laki 7.6?

Wife kapata kazi serikalini huko,mshahara ni TGS D ambayo ni sawa na laki 7.6, kwa sasa anafanya kazi private sector ambako mshahara ni 1.6m gross.

Kampuni anayofanyia ina pressure za hapa na pale ila kuna a lot of incentives kama bima ya afya ya Jubilee,holidays allowance na nyingine nyingi.

So right now yuko dilemma, aache hapo private au aende government?
Mwambie kama anataka kutoa kimaisha yeye na familia yake abaki huko Private. Ila kama ameamua kuwa na maisha magumu na kuua carier yake aje Serikalini.
 
Chukua ushauri wa bure. Abaki huko Private. Afanye kazi na kuwekeza kwenye biashara hata za Pub na Duka ndogo la kawaida, ufugaji mdogo mdogo na kilimo maeneo yenye umwagiliaji. Serikalini ataenda kufa na umaskini wa kipato.
 
Kama ni mke wako na wewe unajiweza. Aende goverment. Hiyo tofauti utajazia wewe.

Mengine pambana kama mwanaume.

Kukaa na mwanamke ana presha za kazi na unataka akulelee watoto ni uongo.

Baba stress mama stress...

Kwa ustawi wa familia aende goverment.
 
Mzee kwa nafasi yake, akimbilie hiyo nafasi serikalini haraka Sanaaaa.... Ahakikishe anasoma CPA.... Sio maeneo yote serikalini ni TGS D hivyo baada ya confirmation anayo room ya kuomba kuhamia taasisi nyengine yenye maslahi bora.
 
Kuna mwanangu alikua private analipwa 1.1M take home, plus per diem za kutosha akitoka nje ya Dar, akapata kazi government akahama, mshaara laki 6, saivi utamuonea huruma alivopauka, anaishi kwa budget kali sana.
Mwambie wife abaki private afanye uwekezaji tu, job security ni poor mindset.
 
Kila walipotawala wakoloni elimu yao na utawala wao ulilenga kutujaza fikra (brainwashed) kuwa watumwa wa kuutumikia utawala wa mfalme/malkia daima. Kwa bahati nzuri au mbaya, tumeurithi mfumo huo na tumeuendeleza kwa miaka zaidi ya 60 ya uhuru.

Tutaendelea kuwa watumwa daima kama hatujabadilika kifikra.
Alaf unakuta wewe uliajiriwa mpaka ulipostaafishwa na umri
 
Wife kapata kazi serikalini huko,mshahara ni TGS D ambayo ni sawa na laki 7.6, kwa sasa anafanya kazi private sector ambako mshahara ni 1.6m gross.

Kampuni anayofanyia ina pressure za hapa na pale ila kuna a lot of incentives kama bima ya afya ya Jubilee,holidays allowance na nyingine nyingi.

So right now yuko dilemma, aache hapo private au aende government?
Job security na kama anania ya kugrow mfano kama bado anauwezo wa kukiendeleza kimasomo basi aende serikalini
 
Extra duty 60k per day, posho za vikao, posho za madokezo, per diem 150k...ukijumlisha vyote inazidi hio 1.6M inategemea tu ye ni profession gani.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nilisema hichi kitu huko juu nikaambiwa kwamba mhasibu wa serikalini tangu lini akasafiri yani mhasibu awepo bunge ashundwe kufikisha 1.6 per month basi atakuwa mzembe wa kuandika madokezo aisee na akiwa halmshauri akawa mwekahazina ndio hata 6m per month ni za kufikia maana mshahara tu ni LSSE1 Hapo ni 3,425,000 hujasafiri hujaingia vikao ujaenda safari ya kujifunza mfumo wa kukusanya mapato hamjaenda kwenye reconciliation hujaenda kwenye final account jamani hata serikalini pesa ipo inategemea ulisoma kada gani .....
 
Back
Top Bottom