Afisa Elimu Jiji La Tanga, wazazi tunaomba ufafanuzi wa hii michango ya fedha

Afisa Elimu Jiji La Tanga, wazazi tunaomba ufafanuzi wa hii michango ya fedha

Wazazi sijui mnataka nini? Watoto wakifeli mnalalamika waalimu wakiwasaidia watoto kujiandaa na mitihani mnalalamika. Hizo shule za private mnaona wanavyoandaa watoto na mitihani. Watoto hao wa private wanashindana na hao watoto wenu.

Wazazi msipende vya bure wajibika kwa elimu ya mtoto wako kughalamia shilingi elfu tatu kwa wiki kwa ajili ya elimu ya mtotk wako unaona ni gharama?
Unataka mwalimu afanye kazi ya ziada lakini usimlipe. Wasikilizeni wana siasa wenyewe watoto wao wako private wanawalipia wewe wanakudanganya.
Hakika umenena. Unajitambua sana mama wewe!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sijakupata hapo pa mfumo wa kuhama darasa na Mwalimu kuwa mmiliki wa darasa.Fafanua kidogo Mkuu
Kwamba mfano unasoma PCM
Physics utaenda darasa jingine, Chemistry utaenda jingine, Maths utaenda jingine, music utaenda jingine, CS utaenda jingine, Social Skills utaenda jingine

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Eti na ww nae una watoto unategemea mtoto mda mwingi akae nyumban akifeli mnaanza kutukana walimu wakiwasaidia pia mnawatolea maneno ya hovyo sijui mijitu mingine ina akili za aina gani
 
Wazazi sijui mnataka nini? Watoto wakifeli mnalalamika waalimu wakiwasaidia watoto kujiandaa na mitihani mnalalamika. Hizo shule za private mnaona wanavyoandaa watoto na mitihani. Watoto hao wa private wanashindana na hao watoto wenu.

Wazazi msipende vya bure wajibika kwa elimu ya mtoto wako kughalamia shilingi elfu tatu kwa wiki kwa ajili ya elimu ya mtotk wako unaona ni gharama?
Unataka mwalimu afanye kazi ya ziada lakini usimlipe. Wasikilizeni wana siasa wenyewe watoto wao wako private wanawalipia wewe wanakudanganya.
Huku sio kufundisha. Ni kukaririsha. Kupumzika pamoja na michezo ni sehemu muhimu ya elimu. Ufundishaji wa aina hii ndio unaowafanya watoto washindwe kumudu masomo ya baadae maana walikariri tu bila kuelewa. Lengo la elimu halipaswi kuwa kupasi mitihani tu.
Badala ya kujipima na hizi praiveti za Akademi n.k. kaangalie IST wanafundishaje watoto wao ambao wanawafanya wakubalike katika Vyuo Vikuu vyenye hadhi kubwa duniani. Na hao watoto wa IST ndio watoto wetu watashindana nao kupata ajira katika mashirika ya kimataifa na taasisi kama BOT n.k. Na wote tunajua wakina nani wanapata ajira huko.

Amandla...
 
Kwamba mfano unasoma PCM
Physics utaenda darasa jingine, Chemistry utaenda jingine, Maths utaenda jingine, music utaenda jingine, CS utaenda jingine, Social Skills utaenda jingine

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
Hapo nimekupata.Point ya kuwa na Clubs tofauti hapo nimeelewa,kwamba wanamaliza masomo mapema kisha wanakuwa kwa hizo clubs wakifanya mambo mengine na si kusoma muda wote.
 
Hapo nimekupata.Point ya kuwa na Clubs tofauti hapo nimeelewa,kwamba wanamaliza masomo mapema kisha wanakuwa kwa hizo clubs wakifanya mambo mengine na si kusoma muda wote.
Hata Ratio ya walimu ni kubwa

Wanafunzi 465
Walimu 67

Elimu yetu inaumizwa na uchache wa walimu

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Hapo nimekupata.Point ya kuwa na Clubs tofauti hapo nimeelewa,kwamba wanamaliza masomo mapema kisha wanakuwa kwa hizo clubs wakifanya mambo mengine na si kusoma muda wote.
Hizo club ni sehemu muhimu ya elimu. Wanafunzi wanajifunza kufanya kazi pamoja na kujifunza wenyewe.

Amandla...
 
Huku sio kufundisha. Ni kukaririsha. Kupumzika pamoja na michezo ni sehemu muhimu ya elimu. Ufundishaji wa aina hii ndio unaowafanya watoto washindwe kumudu masomo ya baadae maana walikariri tu bila kuelewa. Lengo la elimu halipaswi kuwa kupasi mitihani tu.
Badala ya kujipima na hizi praiveti za Akademi n.k. kaangalie IST wanafundishaje watoto wao ambao wanawafanya wakubalike katika Vyuo Vikuu vyenye hadhi kubwa duniani. Na hao watoto wa IST ndio watoto wetu watashina nao kupata ajira katika mashirika ya kimataifa na taasisi kama BOT n.k. Na wote tunajua wakina nani wanapata ajira huko.

Amandla...
Sasa Mkuu hapa tatizo ni Walimu au mfumo wa Elimu yetu kwa ujumla? Unaongelea IST,HOPAC or Braeburn,ISM na shule za caliber hiyo.Hawa tayari walishajitofautisha,hawafuati mfumo wa Elimu ya Tanzania ndiyo maana hawafanyi mitihani ya NECTA.

Nadhani hapa lawama ziende kwa mfumo wa Elimu yetu na si kwa walimu
 
Sasa Mkuu hapa tatizo ni Walimu au mfumo wa Elimu yetu kwa ujumla? Unaongelea IST,HOPAC or Braeburn,ISM na shule za caliber hiyo.Hawa tayari walishajitofautisha,hawafuati mfumo wa Elimu ya Tanzania ndiyo maana hawafanyi mitihani ya NECTA.

Nadhani hapa lawama ziende kwa mfumo wa Elimu yetu na si kwa walimu
Kwa kweli tatizo sio walimu peke yake. Ni mfumo mzima wa elimu unao weka kipaumbele kwenye kupasi mitihani na sio kutoa elimu. Wakina IST wamejitoa katika mfumo wetu kwa sababu hauna tija katika dunia ya sasa.
Kibaya ni kuwa mfumo wetu unasababisha kuwa na walimu ambao hawana wito, sio wabunifu na wanaodhani kazi yao ni kuhakikisha tu kuwa watoto wanapasi mitihani. Mfumo ambao unaoona kazi ya ualimu ni kazi ya walioshindwa kuendelea na masomo hauwezi kutoa elimu inayo stahili kwa watoto.

Amandla...
 
Tatizo lingine ni kuwa tunadhani kuwa elimu inapatikana darasani tu. Tunasahau mambo kama hizo clubs na libraries. Watoto wanatakiwa kufundishwa kupenda kujielimisha. Kujielimisha huko kunapatikana zaidi nje ya mfumo rasmi wa elimu. Wakati sisi tunasoma tulikuwa na Maktaba kuu iliyosheni vitabu, Maktaba ya British Council, Maktaba ya American Embassy, ya Goethe Institute n.k. Na shuleni pia tulikuwa na maktaba na librarian. Shule ilikuwa ya serikali.

Sijawahi kutembelea Central Library hivi karibuni lakini sidhani kama ina vitabu vya kutosha na vilivyo up to date. Mikoani library nyingi zimejaa popo na zimekuwa sehemu za watoto kwenda na vitabu vyao wenyewe kujisomea. Nadhani watoto wengi wanakutana kwa mara ya kwanza na maktaba ya maana wanapoenda chuo kikuu. Kwa mwendo huu hatutafika mbali kielimu.

Mwisho hivi wangapi tuna kabati la vitabu nyumbani kwetu? Nyumbani tuna Flat Screen ya nchi 44 lakini hatuna hata kitabu kimoja cha kujisomea. Ukikuta kabati ni tulilorithi pamoja na vitabu vyake. Tukijitahidi tuna magazeti ya udaku na ya bure tunayokuja nayo kutoka kazini. Halafu tunalalamika kuhusu viwango vya elimu!

Amandla...
 
1. Kila asubuhi watoto eti wanafanya mitihani. Mtoto anawajibika kuripoti shuleni saa 12 asubuhi na kuanza mtihani saa 12.30 asubuhi. Ada shiling 200 kila asubuhi.

2. Jumamosi mtihani. Toka saa 1 mpaka saa 7 mchana. Ada ya mtihani shilingi 1,200. Hii ndiyo utaratibu kutoka ofisini kwako? Au ni invention ya walimu kwamba kila mtu anakula kwa urefu wa kamba yake?

3. Mtoto anarudi saa 11 jioni. na break ya saa nne ni kama haipo maana wanapewa dakika 5 kwenda kujisaidia. Shule inafungwa saa ngapi?

4. Wazazi tujue shule inafungwa saa ngapi tuweze kuwafuatilia watoto vema kama wanafika nyumbani inavyotakiwa.

OMBI: Waacheni watoto Jumamosi wapumzike na kuwasaidia wazazi.
Kama Elimu ni ghali Basi jaribu ujinga yaani usitowe.
Elimu ya siku hizi ni results oriented Sasa kila kiongozi haswa wa Elimu wanajitahidi kila mbinu kuleta matokeo mazuri hivyo Mzazi toa ushirikiano wenzio wasijetumbuliwa
 
Mwisho hivi wangapi tuna kabati la vitabu nyumbani kwetu? Nyumbani tuna Flat Screen ya nchi 44 lakini hatuna hata kitabu kimoja cha kujisomea. Ukikuta kabati ni tulilorithi pamoja na vitabu vyake. Tukijitahidi tuna magazeti ya udaku na ya bure tunayokuja nayo kutoka kazini. Halafu tunalalamika kuhusu viwango vya elimu!

Amandla...
Hapa umegusa penyewe kabisa,wengi wetu umetushika pabaya japokuwa hatutakujibu hili swali.
 
zamani hakukua na shinikizo la kufaulisha, hata likifeli darasa zima poa Tu. Sasa hiv tamisemi wamekuja na Key performing Indicators, shule zimepewa malengo zifikie, kila mwalim, kila shule, kila wilaya na kila mkoa wanatakiwa kuwa na mpango kazi kufikia malengo.

Heb tuwape ushirikiano walimu maana wanaosaidiwa ni watoto wetu, tusitafute vikwazo tu, Kwanza zamani tulikua tunachelewa Sana kuanza shule, wengi wetu tulianza na miaka 9 ama 10, Sasa hiv miaka hiyo ni la 4 au 5 hivyo hawajielew hata wamefata nini shule. Sisi zamani tulikua tunaulizana maeneo kwenye Atlas, miji mikuu, tuna madaftari tunaandika viongozi wa serikali, mawaziri, wakuu wa wilaya na mikoa, Tulikua na vitabu vya JIANDAE VEMA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI. Kwa kiasi kikubwa tulikua tunajiongoza wenyewe.

Hawa watoto wa sasa hawajakomaa kisawasawa hawana self determination kama tulivyokua Sisi, Siri moja kubwa wanatumia Sana seminary na shule binafsi na kumkeep mtoto busy Kwa kumpa mazoez ya kutosha.Idle brain is a source of evils ndo maana hata private mtoto akirud jioni anakuja homework akifunga shule anakuja na home package anapambana na maswali mpaka shule zinafunguliwa. Kama unataka mtoto acheze mpeleke shule yenye sports academy.
Sasa mtu hawezi kusoma na kuandika vizuri atafaulu vipi?
Ndio maana mitihani inaibiwa.

Kwani kunaulazima gani wakufaulisha watu lukuki maana hata ajira hamna.
Kupotezeanatu muda
 
Sasa mtu hawezi kusoma na kuandika vizuri atafaulu vipi?
Ndio maana mitihani inaibiwa.

Kwani kunaulazima gani wakufaulisha watu lukuki maana hata ajira hamna.
Kupotezeanatu muda
Kimsing hii KPI ina changamoto zake, walimu wamejaza mkataba Kwa kufaulisha Zaid ya 50% huku mazingira hayaruhusu. Najiulizaga Daktar akiua mgonjwa anafanywa nini? kwanini mwalim apewe mkataba wa kufaulisha, Kwan kufaulu ni issue ya mwalim peke yake?
 
Ningekuwa Mwalimu sidhani kama ningehangaika na mtoto wa mtu, kwasababu watu wanajaribu kutafuta namna kuinua Elimu kwenye mazingira magumu ila mtuemia mbili ya copy anaona kubwa,basi wapelekeni Fedha huko wakasome,kila siku naona waalimu wanaonekana wanawaibia wazazi......hela zenyewe Sasa kichekesho kabisa.

Tuwaache waalimu wanafanya kazi mazingira magumu sana
 
Kimsing hii KPI ina changamoto zake, walimu wamejaza mkataba Kwa kufaulisha Zaid ya 50% huku mazingira hayaruhusu. Najiulizaga Daktar akiua mgonjwa anafanywa nini? kwanini mwalim apewe mkataba wa kufaulisha, Kwan kufaulu ni issue ya mwalim peke yake?
Wameona hajielewi
 
Back
Top Bottom