#COVID19 Afisa Elimu Mkoa wa Arusha na Muuguzi waliofanya maigizo ya chanjo wasimamishwe kazi mara moja

#COVID19 Afisa Elimu Mkoa wa Arusha na Muuguzi waliofanya maigizo ya chanjo wasimamishwe kazi mara moja

Ujinga huu wa ajabu kabisa hapo kuna tukio gani la kushangaza?video haijakamilika
 
Wanahujumu zoezi la chanjo,kama hawakuwa na mpango wa kuchanja kwanini waigize!
Wajinga sana hao watumishi.Ni Afisa Elimu wa wapi hilo lizee?
ngebe
 
Inawezekana ni mpango mkakati wa serikali maana hata madame boss alifanyaga hivyo hivyo,
Pia hiyo clip haijakamilika hatuwez kujua alieisambaza kwanini kaamua kuifupisha ,
Also hao watu wakipoteza vibarua vyao wewe utajisikia burudani?
Hitimisho: usiamini sana kila kitu unachokiona mitandaoni
 
Tuwashukuru sana hawa watu,kwani wanazidi kuthibitisha ya kwamba chanjo hii haifai kwa matumizi ya binadamu.
 
Hapo kosa ni la Muuguzi, kashindwa kuvaa uhusika.
Inawezekana muuguzi ni mmoja wa watu wanaotaka ukweli ujulikane na ndio maana amefanya hivyo. Big up sana muuguzi chukua soda nitakuja kulipa
Nalog off
 
ukifa kwa korona ni familia yako ndiyo inaumia sio viongozi so tumia akili usiwe na akili fupi kama kinjekitile.
 
huu ni udhahidi kuwa, kuna watu hawachomi chanjo wanahadaa umma,
hv hapa amechoma kweli? ni nini hiki walichokua wanafanya?

nina wasiwasi huwenda na Rais hakuchanjwa na hakuna waziri wala mkuu wa mkoa aliyechanjwa yote ni maigizo!

msituone sisi ni wapumbavu kiasi hicho

wizara ya Afya huyu muuguzi anafanya nini? hii hospitali inauza vyeti vya chanjo?

View attachment 1882300
Nilivyoelewa ni kuwa hakuchomwa kwa sababu kuna kitu kakosea.
 
Hili wanatakiwa wajibu waliolileta maana pamoja na yule daktari bingwa aliyehojiwa na TBC na kueleza wazi hakuna chanjo ya muda mfupi hivyo, madhara ya muda mrefu waliyafanya lini majaribio,wakati chanjo haijatimiza hata miaka 2?.wao wamekomaa kusema iko salama bila justifications.
Leo nimeuliza swali hilo: Nami nikaulizwa swali: Unajua kwa nini inaitwa Corona Virus Disease 19? Wakasema kirusi cha korona sio kipya kiligunduliwa zamani kwa hiyo research na trials zimekuwa zikifanyika. Ndiyo sababu kirusi hiki kimeitwa #19.
Je kuna usahihi kwenye hili?
 
Kwenu Wizara ya Afya na mamlaka husika,

Huu sasa umekua ujinga, tumejitahidi sana kutoa elimu ya kuhimiza chanjo ya Covid-19, binafsi mimi nimetia elimu sana
halafu anakuja mtu wanafanya upuuzi huu video inatrend, watu wanakata tamaa kabisa ya kwenda kwenye chanjo, Wizara ya afya mko wapi huyu nesi asimamishwe kazi.

Mkuu wa Mkoa pia huyu Afisa elimu hapaswi kuwa kazini mpaka muda huu, waondolewe mara moja.
wanaihujumu serikali juu ya mapambano dhidi ya Covid-19

View attachment 1882372
TBC Kutwa nzima wanatueleza chanjo ni hiari. Kwa nini ukereke na clip hii!?
 
Leo nimeuliza swali hilo: Nami nikaulizwa swali: Unajua kwa nini inaitwa Corona Virus Disease 19? Wakasema kirusi cha korona sio kipya kiligunduliwa zamani kwa hiyo research na trials zimekuwa zikifanyika. Ndiyo sababu kirusi hiki kimeitwa #19.
Je kuna usahihi kwenye hili?

19 ni mwaka amao ugonjwa uliibuka mkuu 2019.
 
Hajachomwa kaigiza baada ya kuigiza kapewa pole nesi akimaanisha zoezi tayari. Tukiwaambia viongozi wote duniani hawachanjwi hizi chanjo za majaribio kuna watu wanakuwa wabishi.
Nani amewarecord? Kwasababu ipi?
Alijuaje kutakuwa na udanganyifu? Nani amesambaza mitandaoni?
Any chance ikawa internet manipulation?
Kama ni kweli, huyo jamaa na nurse wake hawakutakiwa kuwepo kazini.
 
Leo nimeuliza swali hilo: Nami nikaulizwa swali: Unajua kwa nini inaitwa Corona Virus Disease 19? Wakasema kirusi cha korona sio kipya kiligunduliwa zamani kwa hiyo research na trials zimekuwa zikifanyika. Ndiyo sababu kirusi hiki kimeitwa #19.
Je kuna usahihi kwenye hili?
Corona virus ni jamii ya virus ambao tunao miaka mingi---Tukumbuke kuwa hawa wadudu ndani ya jamii moja but wapo wa aina tofauti tofauti.. Huyu ameitwa 2019 kwasababu aina yake imegunduliaka 2019. But ipo iliyosababisha SARS 2002, ipo iliyosababisha MERS 2009, huyu SARS-CoV-2 (COVID-19), na wataendelea kuja wengine
 
Back
Top Bottom