Afrika Kusini sio salama, kuna Watanzania wameuawa siku za karibuni

Afrika Kusini sio salama, kuna Watanzania wameuawa siku za karibuni

Kuna dogo mmoja nilikutana nae miaka ya nyuma nikamhoji akasema anatokea magomeni, sasa ilikua lusaka hapo kweli anapass ya kitabu lakini ndio anasafiri kwa kuungaunga hata hajielewi, tunavuka chirundu keshaishiwa kila kitu ikabidi nianze kusimamia show za misosi, kumuhoji sana alisema anaenda Durban mimi nilikua naishia harare, tukafika bus terminal Roadport ya zimbabwe nikaongea nae sana akasema anaenda kuuza madawa wenzake wamemwita, na nauli hana na simu za anaowafuata south hazipatikani ikabidi tumchangie nauli japo apande roli asogee hata mesina mimi na jamaa wa Mabasi ya taqwa alikua zimbabwe jina lake anaitwa S , sasa nikajisemea huyu kajipanga naenda kufanya issue za kihalifu, sikuwahi tena kujua yuko wapi maana ni miaka mingi sana imepita,
Bila shaka ni marehemu
 
Katika safari zangu watu nilioona wanakwenda kwa malengo japo nao nafahamu wengine baadhi yao ni wahalifu warundi, wasomali, wazimbabwe, wamalawi, wanigeria wao hata biashara kubwa wanamiliki na elimu wanayo kubwa tu, kwahivo nadhani ni muhimu kuangalia nini utaamua kufanya maana nikiangalia hata Bongo ukituliza kichwa ukajichimbia sehemu kutoboa kuko palepale sema tumekariri ujanja ni south ukanyoe viduku, uwe kinyozi, mwizi wa highway, madawa maana kiuhalisia wabongo ni wachache sana wenye investment kubwa south za kueleweka
 
Kuna dogo mmoja nilikutana nae miaka ya nyuma nikamhoji akasema anatokea magomeni, sasa ilikua lusaka hapo kweli anapass ya kitabu lakini ndio anasafiri kwa kuungaunga hata hajielewi, tunavuka chirundu keshaishiwa kila kitu ikabidi nianze kusimamia show za misosi, kumuhoji sana alisema anaenda Durban mimi nilikua naishia harare, tukafika bus terminal Roadport ya zimbabwe nikaongea nae sana akasema anaenda kuuza madawa wenzake wamemwita, na nauli hana na simu za anaowafuata south hazipatikani ikabidi tumchangie nauli japo apande roli asogee hata mesina mimi na jamaa wa Mabasi ya taqwa alikua zimbabwe jina lake anaitwa S , sasa nikajisemea huyu kajipanga naenda kufanya issue za kihalifu, sikuwahi tena kujua yuko wapi maana ni miaka mingi sana imepita,
Mkuu hiyo yote ni kwenye kustruggle tu maisha,unaweza wazuia wasiende huko au kwa mtu mwingine asiwaelewe nia yao ya kwenda huko,lakini yote ni maisha tu kila mtu anatafuta ajuavyo yeye

Ova
 
Sijawahi kufika south Africa lakini niulize, hao jamaa wanaua watu bila sababu? Yaani wakikutana na mbongo wanamuua? Nadhani hao waliopostiwa walikua wanafanya issue haramu, labda walizulumiana ndio impact ikawa hiyo.
Ndio issue zao hizo tu.
Bwana mdogo wangu mmoja mpaka namrudisha kashagongwa visu mara 4 kapona
 
Kuwa salama au kutokua salama kunategemea na mazingira ya shughuli zako. Hao wote ni kazi chafu.

Mimi nina mbwa nilimpeleka huko namuita mbwa kwa sababu kafanikiwa na amepata uraia, na maisha yamenyooka, lakini mbwa yule kasahau fadhila.
Ulitaka fadhila gani? Ulishakamilisha part yako, tulia.
 
Itakuwa walikuwa katika chain moja au gang flani, ki group flani cha chenye agenda flani either haramu ama vinginevyo, ao itakuwa labda waliingia kwenye ugomvi na gang nyingine n.k, haiwezekani wapotee wote kwa kwa tofauti ndogo ya muda.
 
Mkuu hiyo yote ni kwenye kustruggle tu maisha,unaweza wazuia wasiende huko au kwa mtu mwingine asiwaelewe nia yao ya kwenda huko,lakini yote ni maisha tu kila mtu anatafuta ajuavyo yeye

Ova

Hustle zipo na rough zipo na hakuna mtafutaji ambae hajawahi kucheza michezo mibovu, iwe hata wale wanaoleta mafuta ya kula toka dubai wanaoshushia zanzibar nao yakiwa kwenye meli yanapigwa nyoka lita moja moja kila dumu, iwe sukari ni hivo hivo, lakini cha msingi inabidi tutumie akili wakati mwingine, chora ramani, fanya tafiti ndio uingie rough zipo wenzetu wanfanya za akili lakini
 
Wewe sio mgeni wa majority ya wabongo wengi dizonga, wanaungaunga tu hasa usikie durban unapata picha gani? Walikojaa watoto wa kino, magomeni na tmk
Mpaka sasa na utuuxima wangu
Naweza kusema katika vijana wa mwanzo mwanzo enzi hizo kwenda
Huko tulikuwa sisi ,kutokea kinondoni
Wakiwwpo na wakina makumbi nk
Wazee wa Italy trans
Wengi ambao miaka hiyo tuliendaga huko wote wakabaki,wamekufa
Visu,shaba nk
Kundi letu tuliporudi sasa ndy kila mtu akawa naye anataka kwenda huko
Sema enzi hizo,walikuwa wanaingia kwa kubinjuka senyenge border
Crime rate huko iko juu siku zote
Sikatai faulo tumecheza sema ukiwa kwenye game hiyo maisha yako unayaweka kwenye high risk
Kwenda kwenda huko nkaja kutana na smbdy k.stander ambaye alikuwa mkur3genzi wa sea cliff Hotel kaburu huyu ,ahh alinibadikishaga sana mindset
Akaniambia a,b,c,d za huko

Ova
 
Hatupendani na n waogoa piaa,,,mtu kafa uwanja wa mapambano wanalaumuuu...walitakaa afe akiwa anakunywa [emoji485]...

Sent using Jamii Forums mobile app
Sema nchi zetu pia hazithamini sana maisha ya raia wake huko ugenini... Imagine ni raia wa nchi za Ulaya au USA ndio inaripotiwa hivi, si msala sana...
 
Hatusemi vibaya marehemu lakini sura tu zinawasaliti kwakweli.

Vijana tufanye kazi halali tuishi maisha yaliyo ndani ya uwezo wetu tuwe smart kimuonekano na zaidi kama hakuna ulazima tubaki tupambane tukiwa nyumbani

Ni hayo tu.
 
Hustle zipo na rough zipo na hakuna mtafutaji ambae hajawahi kucheza michezo mibovu, iwe hata wale wanaoleta mafuta ya kula toka dubai wanaoshushia zanzibar nao yakiwa kwenye meli yanapigwa nyoka lita moja moja kila dumu, iwe sukari ni hivo hivo, lakini cha msingi inabidi tutumie akili wakati mwingine, chora ramani, fanya tafiti ndio uingie rough zipo wenzetu wanfanya za akili lakini
Ila kwa SA issue za rough kufa dk tu
Wabongo wengi wame ubulewe

Ova
 
Back
Top Bottom