Upo serikalini Tena kwenye nafasi ya uteuzi,unapopinga Yale yanayosimamiwa kupitia sera na miongozo ya serikali,huo ni utovu wa nidhamu,kama hukubaliani nao,Kaa kimya,toa maoni jinsi ya kuboresha lakini sio kukosoa kwa kuonyesha jinsi viongozi wako wa juu wanavyokosea,uwezi kumkosoa boss wako harafu akuache tu,hii ni logic simple kabisa.
Viongozi wa kisiasa wanapo amua mwelekeo wa jambo fulani kupitia sera,sheria miongozo au maagizo,mtumishi wa umma ni kutekeleza tu,huwezi kutumia nafasi hiyo kupinga,na kuleta upinzani,hii sio Sawa,lazima utekeleze Yale wakubwa wa kisiasa wanataka serikali ifanye kwa niaba ya wananchi,sio jukumu lako kusema hiki hakifai!wewe hujachaguliwa na wananchi,waliochaguliwa ndio Wana haki na uwezo wa kutenda kwa niaba ya wananchi.
Sasa fikiria Dakitari wa hospitari ya umma,wakati waziri na nchi wanahamasisha chanjo ya COVID,yeye apite kimya kimya chini chini anawashawishi watu wasipime kwa vile ina madhara!!sasa serikali haiwezi kufanya kazi na mtu asiyekwenda na miongozo inayoitoa,lazima upigwe chini.