Ajabu na kweli: Padri wa kanisa katoliki kaoa mke na anavuta sigara kali!

Ajabu na kweli: Padri wa kanisa katoliki kaoa mke na anavuta sigara kali!

Ukistaajabu ya Musa hujaona ya Firauni. Hivi majuzi nilikuwa mitaa fulani nikapita karibu na maskani ya padre mmoja wa kanisa katoliki. Kwa mbali nikamuona mwanamke wa makamo anafanya usafi na kulisha mifugo. Haujapita muda mrefu nikakutana na kijana na kumuuliza kama padre yupo akanijibu padre katoka ila mke wake yupo. Nikamuuliza je, mke wake ni yule niliyemuona anafanya usafi pale nyumbani? Akajibu: NDIYO! Nilihisi kushikwa ganzi na kushindwa kusimama wima. Nikajifanya sijisikii vizuri nikawa nimechuchumaa chini nimeinamisha kichwa. Yule kijana kaniuliza: Vipi unaumwa? Nikamjibu najisikia vibaya.

Kwa mshtuko wangu nilihisi kabisa yule kijana ameunganisha hali yangu na tukio la mke wa padre kwa kuwa alikuwa akiniangalia kwa hofu iliyochanganyikana na wasiwasi. Kijana alionesha hofu ya kutoa siri za watu. Nikaanza kujilaumu kimoyomoyo kwanini nilishindwa kujikaza hadi kijana wa watu akahisi labda nitaenda kuvujisha hizi taarifa kwa viongozi wa kanisa. Nami wala sina nia hiyo na sijamwambia mtu yeyote hadi leo ninapoandika kuhusu jambo hili hapa JF.

Siku za nyuma kidogo (takribani miaka 3 iliyopita) niliwahi kumshuhudia padre mwingine wa kanisa katoliki akivuta sigara kali. Nikashangaa sana. Wavutaji wa sigra kali wanafahamu aina hii ya sigara. Hii sio sigara ya kawaida ndio maana ikapewa hili jina la kipekee. Tangu siku hiyo nikagundua kwamba kumbe upadre wakati mwingine ni kazi tu kama kazi nyingine wala haina koneksheni na utakatifu au matendo mema. Kuna mapadre genuine ambao kweli wamejitoa kumtumikia Mungu kwa hali na mali na wengine ni wachumiatumbo tu.

MAONI YANGU
Ifike wakati sasa kanisa litambue umuhimu wa matamanio ya mwili kwa wanadamu na kusitisha mpango wake wa muda mrefu wa kuwazuia mapadri kuoa na kutumia vilevi vingine kama watu wa kawaida ilmradi hawavunji amri 10 za Mungu. Kitendo cha kulazimisha mapadri wasioe na kushiriki matendo mengine mema ya dunia sio jambo zuri.

ANGALIZO
Hii sio mada ya kidini bali ni habari mchanganyiko inayohusu maisha ya binadamu bila kujali imani, dini, rangi, jinsia, kabila au ukanda. Mods msiingie mkenge kuhamisha hii mada kwenda jukwaa la dini tafadhali.

Nawasilisha.
Unashangaa Padre kuvuta Sigara, nikiwa kijana mdogo nilikua natumikia Kanisani, Askofu wa zamani wa jimbo kuu la Mwanza sasa Marehemu, alikua akivuta Sigara, na haikua Siri, ila hakua akivuta Mbele za Watu, Sigara sio Dhambi.... Kama ilivyo Pombe.
 
Unashangaa Padre kuvuta Sigara, nikiwa kijana mdogo nilikua natumikia Kanisani, Askofu wa zamani wa jimbo kuu la Mwanza sasa Marehemu, alikua akivuta Sigara, na haikua Siri, ila hakua akivuta Mbele za Watu, Sigara sio Dhambi.... Kama ilivyo Pombe.
Mkuu sigara ni kileo kama zilivyo pombe na vilewo vingine. Usitetee dhambi kwa mifano rahisi. Kwa hiyo padre kuvuta bangi au sigala kali wewe unaona sawa tu?
 
Ukistaajabu ya Musa hujaona ya Firauni. Hivi majuzi nilikuwa mitaa fulani nikapita karibu na maskani ya padre mmoja wa kanisa katoliki. Kwa mbali nikamuona mwanamke wa makamo anafanya usafi na kulisha mifugo. Haujapita muda mrefu nikakutana na kijana na kumuuliza kama padre yupo akanijibu padre katoka ila mke wake yupo. Nikamuuliza je, mke wake ni yule niliyemuona anafanya usafi pale nyumbani? Akajibu: NDIYO! Nilihisi kushikwa ganzi na kushindwa kusimama wima. Nikajifanya sijisikii vizuri nikawa nimechuchumaa chini nimeinamisha kichwa. Yule kijana kaniuliza: Vipi unaumwa? Nikamjibu najisikia vibaya.

Kwa mshtuko wangu nilihisi kabisa yule kijana ameunganisha hali yangu na tukio la mke wa padre kwa kuwa alikuwa akiniangalia kwa hofu iliyochanganyikana na wasiwasi. Kijana alionesha hofu ya kutoa siri za watu. Nikaanza kujilaumu kimoyomoyo kwanini nilishindwa kujikaza hadi kijana wa watu akahisi labda nitaenda kuvujisha hizi taarifa kwa viongozi wa kanisa. Nami wala sina nia hiyo na sijamwambia mtu yeyote hadi leo ninapoandika kuhusu jambo hili hapa JF.

Siku za nyuma kidogo (takribani miaka 3 iliyopita) niliwahi kumshuhudia padre mwingine wa kanisa katoliki akivuta sigara kali. Nikashangaa sana. Wavutaji wa sigra kali wanafahamu aina hii ya sigara. Hii sio sigara ya kawaida ndio maana ikapewa hili jina la kipekee. Tangu siku hiyo nikagundua kwamba kumbe upadre wakati mwingine ni kazi tu kama kazi nyingine wala haina koneksheni na utakatifu au matendo mema. Kuna mapadre genuine ambao kweli wamejitoa kumtumikia Mungu kwa hali na mali na wengine ni wachumiatumbo tu.

MAONI YANGU
Ifike wakati sasa kanisa litambue umuhimu wa matamanio ya mwili kwa wanadamu na kusitisha mpango wake wa muda mrefu wa kuwazuia mapadri kuoa na kutumia vilevi vingine kama watu wa kawaida ilmradi hawavunji amri 10 za Mungu. Kitendo cha kulazimisha mapadri wasioe na kushiriki matendo mengine mema ya dunia sio jambo zuri.

ANGALIZO
Hii sio mada ya kidini bali ni habari mchanganyiko inayohusu maisha ya binadamu bila kujali imani, dini, rangi, jinsia, kabila au ukanda. Mods msiingie mkenge kuhamisha hii mada kwenda jukwaa la dini tafadhali.

Nawasilisha.
Sasa nawewe ulienda kuungama dhambi zako au ulienda kufanya nini kwenye nyumba za watu? Unatakiwa kwenda kanisani si kwenye makazi yao.
 
Sasa nawewe ulienda kuungama dhambi zako au ulienda kufanya nini kwenye nyumba za watu? Unatakiwa kwenda kanisani si kwenye makazi yao.
Mkuu usijadili nje ya mada.....jikite kwenye mada mahsusi (theme) ya uzi.
 
Mkuu sigara ni kileo kama zilivyo pombe na vilewo vingine. Usitetee dhambi kwa mifano rahisi. Kwa hiyo padre kuvuta bangi au sigala kali wewe unaona sawa tu?
Nasema hivi, Sigara, Pombe si dhambi, Dhambi ni matokeo....!

Kama nikivuta Sigara, Sizurumu cha mtu, Sizini, Siibi, wewe ambaye huvuti, ni mwizi, mzumaji, Mzinzi...!

Unadhani nani atakutana na mkono wa Mungu....!?

Ukristo ni Ndani ya Moyo.,..
 
Naunga mkono hoja, nilipandisha bandiko kushauri mapadri wa Katoliki waoe, lilifutwa fasta!.
P

Ni maoni yako na ni sawa kibiblia ila hakuna mtu anaelazimishwa kuwa padre, wote wanakula kiapo wakiwa watu wazima. Sasa kwa nini mtu aingie ndio aone umuhimu wa kuzaa na kuwa na familia??..

Kama anataka kumtumikia Mungu, mbona kanisa lina levels nyingi za kutumikia pasipo kujiingiza kwenye utawa au upadre

Kwa nini mtu awiwe kuwa padre na vipi kama hao wanaofanya maovu hawakuwa na wito zaidi ya kutaka benefits za upadre

Je, hiyo level ikirahisishwa, huoni kama hali itakuwa mbaya zaidi maana barrier waliyowekewa imepunguza mamluki kuliko waliopo sasa

Je, mkuuu pascal wewe kama muandishi wa habari, ulishawahi kufanya uchunguzi wa kina kuhusu hizi story ili ujue faida ya hii system lakini pia perspective ya watawa wenyewe katika hili kuliko kutegemea nadharia za jamii ya kawaida

Faida na hasara ni zipi ili kabla kulishauri kanisa kuruhusu mapadre waoe ili uwe na informed contribution
 
Nimefuatilia comments zenu moja baada ya nyingine nimegundua jamii imekengeuka sana. Eti badala ya kuona kitendo kibaya alichokifanya padre na kukemea, wengi wenu mnasapoti na kujifaharisha kuwa padre kafanya kitendo cha kishujaa!!! Hivi ukengeufu wa jamii kumbe umefikia kiwango hiki cha kutisha? Mungu Baba atusamehe🙄 😳 🙄 😳
 
Ukistaajabu ya Musa hujaona ya Firauni. Hivi majuzi nilikuwa mitaa fulani nikapita karibu na maskani ya padre mmoja wa kanisa katoliki. Kwa mbali nikamuona mwanamke wa makamo anafanya usafi na kulisha mifugo. Haujapita muda mrefu nikakutana na kijana na kumuuliza kama padre yupo akanijibu padre katoka ila mke wake yupo. Nikamuuliza je, mke wake ni yule niliyemuona anafanya usafi pale nyumbani? Akajibu: NDIYO! Nilihisi kushikwa ganzi na kushindwa kusimama wima. Nikajifanya sijisikii vizuri nikawa nimechuchumaa chini nimeinamisha kichwa. Yule kijana kaniuliza: Vipi unaumwa? Nikamjibu najisikia vibaya.

Kwa mshtuko wangu nilihisi kabisa yule kijana ameunganisha hali yangu na tukio la mke wa padre kwa kuwa alikuwa akiniangalia kwa hofu iliyochanganyikana na wasiwasi. Kijana alionesha hofu ya kutoa siri za watu. Nikaanza kujilaumu kimoyomoyo kwanini nilishindwa kujikaza hadi kijana wa watu akahisi labda nitaenda kuvujisha hizi taarifa kwa viongozi wa kanisa. Nami wala sina nia hiyo na sijamwambia mtu yeyote hadi leo ninapoandika kuhusu jambo hili hapa JF.

Siku za nyuma kidogo (takribani miaka 3 iliyopita) niliwahi kumshuhudia padre mwingine wa kanisa katoliki akivuta sigara kali. Nikashangaa sana. Wavutaji wa sigra kali wanafahamu aina hii ya sigara. Hii sio sigara ya kawaida ndio maana ikapewa hili jina la kipekee. Tangu siku hiyo nikagundua kwamba kumbe upadre wakati mwingine ni kazi tu kama kazi nyingine wala haina koneksheni na utakatifu au matendo mema. Kuna mapadre genuine ambao kweli wamejitoa kumtumikia Mungu kwa hali na mali na wengine ni wachumiatumbo tu.

MAONI YANGU
Ifike wakati sasa kanisa litambue umuhimu wa matamanio ya mwili kwa wanadamu na kusitisha mpango wake wa muda mrefu wa kuwazuia mapadri kuoa na kutumia vilevi vingine kama watu wa kawaida ilmradi hawavunji amri 10 za Mungu. Kitendo cha kulazimisha mapadri wasioe na kushiriki matendo mengine mema ya dunia sio jambo zuri.

ANGALIZO
Hii sio mada ya kidini bali ni habari mchanganyiko inayohusu maisha ya binadamu bila kujali imani, dini, rangi, jinsia, kabila au ukanda. Mods msiingie mkenge kuhamisha hii mada kwenda jukwaa la dini tafadhali.

Nawasilisha.
Hivi majuzi nilikuwa mitaa fulani nikapita karibu na maskani ya padre mmoja wa kanisa katoliki. Kwa mbali nikamuona mwanamke wa makamo anafanya usafi na kulisha mifugo.
 
Hivi majuzi nilikuwa mitaa fulani nikapita karibu na maskani ya padre mmoja wa kanisa katoliki. Kwa mbali nikamuona mwanamke wa makamo anafanya usafi na kulisha mifugo.
Mkuu usisome ukaishia hapa tu. Endelea mbele utapata content. That was just a preamble.
 
Kazowea hao ni mapapai, lazima azimie.

tpaul
Ningeshangaa sana FaizaFoxy aache kuandika kitu kwa mada kama hizi.

Mleta mada, haya uliyoyaona sio ajabu, na Kila Dini Lina vioja vyake. Binafsi nawajua Mashekhe wengi tu ambao ni wapiga tunguli.

YESU Kristo alisema "Jililieni nafsi zenu". Hakuna atakaye eenda peponi kwa nafsi ya Mtu mwingine, awe mzazi, padre, shekhe, askofu Wala Mtume.
 
Mkuu usijadili nje ya mada.....jikite kwenye mada mahsusi (theme) ya uzi.
Ndiyo maana tuna ambiwa tuwaombee nao ni binadamu si malaika, shetani hana mapembe ni binadamu sisi hawa hawa, na kwa taarifa yako wanawake wengi huwa wanajipeleka wenyewe kwao.
 
ukiristo siodini jamanii.situlisha kubaliana mbona mnakuwa wagumu kuelewa?☹️☹️☹️😕😕😕😕hadituwachape viboko au?
 
Unafahamu maana ya neno ndoa? Rudi shule ukasome ndipo ujue kitendo ulichofanya ni zaidi ya kuoa. Tamaa za mwili zitakupeleka jehanamu. Tii miiko na sheria za kanisa; punguza tamaa za mwili mkuu.
Kwamba wewe ndio wa kunifundisha mimi maana ya ndoa ?

Kwa sababu wewe ni malaya basi unafikiri kila mtu humu ni malaya kama wewe ?
 
Wewe unadhani hilo ni jambo la kawaida?
hapana kwakwel... Lakini nae ni binadam hajakamilika... Tujitahid kuwasitiri tuu... Mimi kuna sheikh huwa anakuja dukan kununua sigara anazunguuka nyuma ukutani anapiga sigara mbili chap anarud msikitini... Lakini huwa simsemi ndio nimesema leo... Inshort ni kujiepusha tu...
 
Back
Top Bottom