Nipo serious mkuu, ukute alifananishwa au labda ni yeye, ndo maana nikasema, ni vema angetiwa nguvuni, halafu afikishwe mbele ya vyombo vya sheria, haki itendeke. Hiyo mob justice, ingekuwa vema ikaelekezwa kwa wezi wa mali za umma, ambao wanajulikana na karibia kila mtanzania, ila sheria hazichukui mkondo wake, jamii ingeheshimika kuliko kumuua mtu tena yawezekana hakupewa hata nafasi ya kusikilizwa lakini ndo hivyo.
Kuna habari za watu wengi tu kuuawa kwa kuitiwa mwizi huku si kweli na watu kuua bila kumhoji wala kumsikiliza, siyo fair kabisa. Anyway ndiyo umma wetu huu.