Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Kikwete mlisema mkatili anatoa watu kucha,Magufi dikteta na huyu naye kashakuwa muonevu,sasa naanza kuamini maneno ya hayati Mwl.J.k.Nyerere kuwa ikulu ni pagumu...
 
Uchaguzi wa 2025 hashindi hata akiiba kura. Watu watadhibiti wakurugenzi na tume.
Kuna wimbo moja maarufu ambao unaimbwa wakati wa mchakamchaka una maneno yafuatayo;

"Kibwagizo: Jua lile literemke mama"
Kiitikio: Jua lile literemke mama"

Mkuu, kamwe jua haliwezi kuteremeka.
 
Timu Mwendazake mmeshikwa pabaya na mama!
 
Fedha za umma zinachotwa na majizi bila huruma ARUSHA ni mfano mzuri mbunge wa Arusha mjini MRISHO GAMBO alijitoa mhanga na kuwataja hadharani baadhi ya viongozi wa CCM na mkurugenzi wa jiji la Arusha kuwa wamechota fedha za miradi mkoani hapo na kujiwekea katika account zao hakuishia hapo alusema kuwa wengine aliamua kutowataja kwa sababu ya kutodhalilisha serikali.

Ndugu wana jamvi hilo lilitokea Arusha mbunge aliyeapa kuwa yupo tayari kuwataja na atapambana nao je kwa wabunge ambao ni waoga je fedha huko kwenye halimashauri siwanajichotea bila huruma! Niwaambie ukweli ipo halmashauri ilipewa fedha kiasi cha tsh bilion tatu ijenga shule mkoa flani hadi sasa mradi huo haujakamilika na pesa zilishatolewa.

Nimefatilia kwa ukaribu juzi walivyosikia rais anafanya ziara mkoan kagera waliwaita mafundi haraka sana walijua anaweza kupita katika mkoa huo na kuwaletea matatizo! Je hii ni sawa katika utendaji?

Rais wangu mama SAMIA SULUHU HASSAN anza kufanya ziara kila mkoa ulipopeleka fedha kwenye miradi mbalimbali ujionee madudu vijana wako wanakula hadi wamekata kamba wanajuwa hufatilii wanaona wewe niwakukuandalia safari za kila mara huku wanapiga fedha za umma, jaribu kukaa hata mwezi na kufanya ziara utanishukuru ninayokwambia! Vijana wako wanakula hadi wamepitiliza miradi haiendi.
 
Ana kwama wapi sema siyo uje na kauli mama anakwama kisa tu mzee wako amestaafu anasubilia kinua mgongo mda bado kupewa na wewe una hesabu nazo unaona mama anakuchelewesha as if mama ndio yupo uko hazina
 
Tunaishi kwenye nchi yenye kanchi kadogo ndani yake!
 
Hata asinge safiri ukosefu wa Dawa na Maji ungekuepo tu.
Safari haikusababishi ukose Dawa na Maji Mkuu,hayo matatizo yapo toka awamu zilizo pita.
Hayati Magufuli aliwafunga midomo kukataa ujinga kama huu.

Sent from my SM-J500F using JamiiForums mobile app
 
Ujinga wa wafuasi wa jiwe unaendana na roho ya kwanini. Wanafurahia watu kuishi maisha magumu! Akitumbua,akisema siongezi mishahara,hakuna posho nk hapo roho zenu zitakuwa kwatuu!

Ada ya kidato Cha sita imefutwa....hio ndilo la msingi sasa hivi.
 
Ujinga wa wafuasi wa jiwe unaendana na roho ya kwanini. Wanafurahia watu kuishi maisha magumu! Akitumbua,akisema siongezi mishahara,hakuna posho nk hapo roho zenu zitakuwa kwatuu!

Ada ya kidato Cha sita imefutwa....hio ndilo la msingi sasa hivi.
Wengi ni kama huyu muuza kangala, hoja zao ni malalamiko tu. Watu wanaoamka asubuhi na machungu na kwenda kulala jioni wakiwa na machungu mengi tu.
 
Tangu ameingia madarakani nimeona ziara nyingi anazifanyia nje ya nchi na katika ziara hizo tulichokipata ni mikopo mbalimbali kwa ajiri ya miradi mbalimbali ! Kuhusu kukaa nchini na kufanya ziara katika mikoa mbalimbali kujuwa kero za wananchi hili naona hili halifanyi kabisa kwa asilimia kubwa, hata akikaa nchini mara nyingi ana kaa ikulu na kusubilia taarifa za viongizi wake wa chini na akikaa zaidi ya miezi miwili basi ujue kuna mtu atapata teuzi hayo ndiyo nayoyaona anayoyafanya.

ziara kubwa nchini ya kwanza kumbukumbu ya mwalimu nyerere iliyofanyika mkoa wa mara na akaambiwa kero za mkoa huo

Ziara ya pili mkoa wa mwanza sikukuu ya wafanyakazi

Ziara ya tatu mkoani pwani

Ziara ya nne daresalaam kukagua soko la kariakoo

Ziara ya tano mkoa wa tabora kuzindua barabara.


Ziara ya sita mkoa wa kagera wilaya ya chato kuzindua shule mgeni alikuwa MSEVENI.
 
 

Attachments

  • IMG_4664.MP4
    3.7 MB
Kwaio unataka kusema ubao unasona 18-6?basi hatari sana hii
 

Duh mipasho hatari
Mama yupo kikaangoni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…