Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Samahani wewe ni MJINGA, yaan samahani sana. NCHI HII KUNA RAIS ALIFANYA MAPYA KAMA SIO MWENDELEZO WA YALIYOPITA? Hivi huwa mnafikirikia kwa kutumia makalio au akili??

Mmetaka alichofanya mmewekewa sasa mnaanza kubishia nini?? Huyo boya wenu MAGUFULI alifanya nini lenye manufaa kwa watu wa CHINI??
Kwa maneno kama hayo tu kwenye hiyo comment yako...INAONYESHA WAZI KUWA WEWE NI MWEPESI SANA KWENYE UJENGAJI WA HOJA.

Sawa sikatai naweza kuwa Mjinga lakini wewe mwerevu mbona unakimbilia kejeli?...

kwa staili hii...endelea tu kutumia kichwa chako kama kabati la kuhifadhia Meno na sio vinginevyo.

Unadiriki kuuliza kuwa "NCHI HII KUNA RAIS ALIYEFANYA MAPYA KATIKA AWAMU YAKE?"...hivi ni miradi mingapi mipya ambayo Magu aliifanya na haikuwepo awamu za nyuma??...(kwa hiyo SGR, Stiegler's Gorge kule mto rufiji sio vipya vilivyoletwa na magu katika awamu yake ya tano)

Acheni, blah...blah...blah!...tuambie miradi mipya aliyoianzisha yeye Rais samia kipindi cha hii awamu yake mpya anayosema ya.6. Na ni Kwanini hamusemi ukweli kuwa mama ameanzisha mfumo wake mpya wa kukusanya mapato kupitia miamala ya kifedha kielektronik yaani TOZO?...au haya si maendeleo tumepigwa jamani😂😂😂

USHA PANIC WEWE...
 
Mnaweza kunambia ni kipi cha maana alichokifanya rais Samia hadi sasa ambacho kimegusa raia wa kawaida au kumsaidia??

Nambieni ni kipi kakifanya ambacho kinaweza kuwa sababu ya yeye kusema amefanya kazi ya kusaidia wananchi wake

Nataka kimoja tu ambacho kakifanya ambacho tunaweza kusema kimemgusa mtu wa chini tokea awe Rais
Women empowerment
 
Wewe unamatatizo kichwani, kwani Hayati Dr Magufuli Alikuwa Ni mgombea Binafsi? Kwani Hakuwa na chama? Kama alikuwa na chama ni chama gani? Halafu hata bila aibu unajenga hoja kwa kusema mdogo wako alipata ajira 2018,swali je kupata ajira kwa mdogo wako ndio kulizuia ajira zisitoke kipindi hiki Cha mama Samia? Au mdogo wako kupata kazi ndio ajira zikafungwa serikalini mpaka leo? Au ulitaka kuleta ujumbe gani hapa kuhusu kuajiliwa kwa mdogo wako?

Alipofariki Dr Magufuli mama Samia alikuwa Ni Nani serikalini? Vipi mh kasimu majaliwa? Uliona uchaguzi mkuu ukiitishwa Tena? Unajuwa kwanini haukuitishwa kwa akili yako? Jibu Ni kuwa Ni kwa kuwa mh Rais wetu mpendwa kipenzi Cha watanzania Alipiga kampeni na aliinadi ilani ya CCM na alikuwa katika utekelezaji wake katika kipindi chote na hata alipofariki Hayati Magufuli na kuapishwa mama samia kwa mujibu wa katiba yetu alikuwa anajuwa kazi iliyopo mbele yake,

Mama Samia Rais wetu kafanya mambo makubwa Sana ndani ya muda mfupi Sana, mpaka amalize miaka yake hiyo 2030 hakika Tanzania itakuwa inapendeza sanaaa na kuvutia Sana, Hutaki unataka huyu ndio Rais Wako tuu labda uhame nchi, na kwa akili yako utaenda kuwa mtumwa ugenini
Na wala sikumaanisha eti kupata ajira kwa uyo mtu...kuzuie rais samia asitoe ajira kwa wengine.

Na hakuna niliposema Magufuli alikuwa mgombea binafsi SOTE TUNAFAHAMU alikuwa ni wa CCM, Na maana ya kwamba miradi ya maendeleo iliyowepo katika ilani ya CCM awamu ya tano tunaifahamu. Na hadi ivi sasa tupo ndani ya miaka miwili ya awamu mpya ya sita...semeni kipi kipya ambacho hakijaachwa na hayati Magu kimefanywa na mama samia???

Maana itakuwa ni upumbavu leo hii Stiegler's Gorge ikamilike alafu tuseme MAMA SAMIA AMEJENGA KATIKA AWAMU YAKE YA 6. Wakati inafahamika kuwa mradi uliletwa na magu akauwacha ukiendelea kutekelezwa na bajeti yake ikiwa ilishapangwa kabisa. Tokea awamu ya tano.
 
Mnaweza kunambia ni kipi cha maana alichokifanya rais Samia hadi sasa ambacho kimegusa raia wa kawaida au kumsaidia??

Nambieni ni kipi kakifanya ambacho kinaweza kuwa sababu ya yeye kusema amefanya kazi ya kusaidia wananchi wake

Nataka kimoja tu ambacho kakifanya ambacho tunaweza kusema kimemgusa mtu wa chini tokea awe Rais
Wewe kipi umefanya kumsaidia mumeo na watoto wako
 
Sijacomment tangia jana baada ya kuusoma huu uzi bado naendelea kutafuta.

Nikipata nitacomment.
 
Mnaweza kunambia ni kipi cha maana alichokifanya rais Samia hadi sasa ambacho kimegusa raia wa kawaida au kumsaidia??

Nambieni ni kipi kakifanya ambacho kinaweza kuwa sababu ya yeye kusema amefanya kazi ya kusaidia wananchi wake

Nataka kimoja tu ambacho kakifanya ambacho tunaweza kusema kimemgusa mtu wa chini tokea awe Rais
Kwani mwendazake alifanya nn cha maana?
 
Kwani magufuli alikubalika na nani kiufupi hakuna raisi aliyekubalika akiwa madarakani ngosha mpaka amekufa ndo watu wanajifanya alikuwa jembe watanzania kwa unafiki
 
Kwani mbolea haujaona namna zilivyopungua Bei? Japo Sina uhakika Kama hata unafahamu habari za kilimo maana katika kusoma maelezo yako nimeona Ni mtu ambaye huna taarifa nyingi Sana juu ya yanayoendelea hapa nchini katika secta nyingi tu,Sasa Kama hufahamu ni kuwa mbolea zilipaa Sana Bei na siyo hapa tu Bali maeneo mengi tu katika Bara la afrika, lakini mh Rais wetu mpendwa mama Samia kwa umadhubuti na ushupavu wake kiuongozi akaamua kuwaokoa wakulima kwa kuamua kutoa Ruzuku ya billion Mia moja hamsini Hali iliyopelekea kushuka kwa Bei ya mbolea zaidi ya nusu ya Ile ya msimu uliopita sokoni,

Sasa je hapa wewe huoni kuwa mh Rais amewagusa wananchi moja kwa moja? Huoni kilimo Ni pumzi ya watanzania wanyonge walio wengi? Huoni hapa Ni Kama mama Amewapa pumzi mpya na Safi mamilioni ya wakulima? Huoni ameleta matumaini kwa watanzania? Unajuwa athari ya mtu kuishi bila matumaini wewe?

Vipi kuhusu bajeti ya kilimo? Unajuwa mama aliikuta Ni shilingi ngapi na kwa Sasa Ni shilingi ngapi? Unajuwa Ni vipi kilimo kwa Sasa kimekuwa na tija kutokana na juhudi za mh Rais wetu kutilia mkazo?

Najuwa huwezi ukayaelewa haya maana akili yako imefubazwa na chuki zilizojaa katika akili na moyo wako juu ya Rais wetu mpendwa, lakini utake usitake huyu ndiye Rais wako mwenye kibali Cha watanzania na ambaye amepewa baraka zote na watanzania kutuongoza Hadi 2030

Pia lazima ufahamu kuwa Ni utaratibu wa Rais yoyote Yule katika nchi yetu kufanya Kama ambavyo baba wa Taifa amewahi kutuasa kuwa unaanzia alipoishia mwenzio katika Yale mema na kurekebisha Yale yenye kasoro, huuwi ulivyovikuta Wala huviharibu ulivyovikuta Bali unakamilisha,kuendeleza na kukamilisha vilivyokuwa katika mipango na mikakati ikiwa tu vitaonekana vina faida pale vitakapokamilishwa na hapo ndipo hatua zako zinapoanza katika kuibua au kuanzisha na kutekeleza miradi mingine,mikakati mingine kulingana na bajeti itakavyoruhusu na uchumi wa wakati huo,

Amefanya hivyo Samia ,alifanya hivyo Hayati Magufuli na atafanya mwingine pia miaka ya mbele huko, kwa hiyo acha ushamba wa kiuongozi, nchi ina utaratibu wake wa kimaendeleo, chama ni kimoja kilichoongoza nchi hii na kitakachoendelea kuongoza nchi hii, kwa hiyo hakuna anayekuja kuongoza nchi utazaninmgombea binafsi, Soma uelewe , siyo kuandika tu utazani mtu alikuwa peke yake katika kwenda kufanya vibarua na kuleta hela za kujengea nchi yetu,Urais Ni Taasisi siyo mtu binafsi
Na wala sikumaanisha eti kupata ajira kwa uyo mtu...kuzuie rais samia asitoe ajira kwa wengine.

Na hakuna niliposema Magufuli alikuwa mgombea binafsi SOTE TUNAFAHAMU alikuwa ni wa CCM, Na maana ya kwamba miradi ya maendeleo iliyowepo katika ilani ya CCM awamu ya tano tunaifahamu. Na hadi ivi sasa tupo ndani ya miaka miwili ya awamu mpya ya sita...semeni kipi kipya ambacho hakijaachwa na hayati Magu kimefanywa na mama samia???

Maana itakuwa ni upumbavu leo hii Stiegler's Gorge ikamilike alafu tuseme MAMA SAMIA AMEJENGA KATIKA AWAMU YAKE YA 6. Wakati inafahamika kuwa mradi uliletwa na magu akauwacha ukiendelea kutekelezwa na bajeti yake ikiwa ilishapangwa kabisa. Tokea awamu ya tano.
 
Mama Samia anaandamwa zaidi na DINI yake, ila kwa kazi zenye manufaa na UWAZI amemuacha mbali sana MAGUFULI. Uongozi sio vitisho, ni kuongoza kwa taratibu na sheria, Haya Kabudi aliongea wazi kuwa ile ishu ya MAKINIKIA walitung uongo. Sasa ile ilitusaidia nini??

Mada nyingi za Mama Samia zimejificha kwenye CHUKI ZA DINI YAKE. Hali hii hata kwa KIKWETE. WAKRISTO mara zote huwa mnahisi mko njia sahihi, na huwa mna beba sana chuki za kipumbavu.

HAYA NIAMBIE WEWE KUNA JAMBO LINALOIGUSA JAMII MOJA KWA MOJA KUSHINDA AJIRA, UPANDIASHWAJI WA MADARAJA NA VYEO???

Magufuli aliwahi kufanya hayo??? Acha chuki, hazitokusaidia, and pata kujua hii nchi ni ya wote na kila mtu ana haki ya kuongoza.
Hayo ni mawazo ya inferiority complex, badilika uende na wakati
 
Kama kuna watu 1000 hapa Tz ambao sio wanasiasa wala watumishi wa umma wala wafanyabiashara wanaomkubali rais samia basi nipo tayari kutoa gari yangu

Wanaomkubali Samia kwasasa kati ya watu milioni 60 huku Bara basi hata 1000 hawafiki

Nimetafuta raia wa kawaida anayemuunga mkono huyu bibi hayupo hata 1000 hawafiki nchi nzima

Hakubaliki, hapendwi wala hakuna mwenye hamu ya kumsikia huo ndio ukweli, mtaani ni ngumu sana kumkuta mtu anamkumbali rais Samia ukiachana na watumishi wachache wa umma na wanasiasa, na wafanyabiashara baadhi.

Huo ndio ukweli, mwambieni Rais ukweli kuwa hakubaliki kabisa kwa upande wa Tanzania bara.
Rais Samia yupo pale kwenye nafasi ki mkakati. Naweza sema anafanya kitu tunaita katika utawala ni ku turn around nchi, kutoka kwenye mkakati wa siasa za ndani kurudi siasa za nje. Kitu alichokifanya mpaka sasa siyo kibaya ni kizuri na miaka inayokuja hata watu wenye kipato kidogo watafurahia matunda ya Rais Samia. Hivyo tunajua wanyonge hawampendi kabisa Rais Samia ila tunajua sababu kuu ni mabadiliko. Tunaamini ndani ya miaka miwili uchumi wa juu utawagusa hata hawa wa chini na watafurahia. Tuzidi kumuombea Rais Samia aendelee kutuongoza kwa vipindi vingi zaidi.
 
Sasa wewe unataka kusema huyu Ni Rais wa awamu ya tano , Hivi hata mtoto wako hapo nyumbani akikuuliza huyu Ni Rais wa awamu ya ngapi utamwambia awamu ya Tano? Akikwambia umuhesabie Marais utamwesabiaje mwanao Hadi mh mama yetu Samia Naye awe wa awamu ya Tano?

Pili huyu siyo kaimu Rais Bali Ni Rais kamili wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, Ndio maana aliapa kiapo walichoapa Marais wengine walio mtangulia, Hakupewa kiapo Cha ukaimu Urais na Wala hakuna kitu Cha namna hiyo katika katiba yetu, Kama unacho tuwekee hicho kifungu kinachosema huyu Ni kaimu Rais,

Mama Samia Suluhu Hassan Ni Rais kamili wa jamhuri ya muungano wa Tanzania mwenye mamlaka kamili ya Urais na uamiri Jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama, Ni Rais kamili mwenye Amri zote na nguvu zote za Urais,
Hahaha!...mbona huelewi ndugu, NAULIZA HIVII KATIKA MAZINGIRA YOYOTE YALE HAKUNA MTU DUNIANI ANAYEPEWA MAMLAKA NA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YA RAIS BILA KUAPISHWA/KIAPO...AU wewe uliona wapi hii??...toa mfano hapa.

Na hakuna mahali nimesema rais samia sio RAIS KAMILI, Bali naungana nawewe kabisa hapo kusema ni rais kamili na ana mamlaka yote ya kiutendaji kama amiri jeshi na maamuzi yote ndani na nje ya nchi kwa niaba yetu watanzania(Maana ata akienda kukopa mikopo hakopi kwa jiani lake bali jina la TZ)

Mbona katiba ilishaweka wazi hili ndugu...
"Kwa mujibu wa kifungu cha 37 (5) cha Katiba ya nchi hiyo iliyotungwa mwaka 1977, nafasi ya urais inapokuwa wazi kwa sababu yoyote ikiwemo kifo, viongozi watatu wameorodheshwa na ni Makamu wa Rais, na endapo hatakuwepo atachukua Spika wa Bunge na kama hayupo atachukua Jaji Mkuu"

Hivyo "
endapo kiti cha Rais kitakuwa wazi kutokana na Rais kufariki dunia, kujiuzulu, kupoteza sifa za uchaguzi au kutomudu kazi zake kutokana na maradhi ya mwili au kushindwa kutekeleza kazi na shughuli za Rais, basi Makamu wa Rais ataapishwa na atakuwa Rais kwa muda uliobaki katika kipindi cha miaka mitano..." inaeleza katiba ya Tanzania katika kifungu cha 37 (5).

KWA MUJIBU WA MANENO HAYO HAPO MWISHONI(atakuwa Rais kwa MUDA ULIOBAKI katika kipindi cha miaka mitano..). HIVYO YEYE ATAMLIZIA TU KIPINDI KILICHOBAKIA KATIKA HIYO MIAKA MITANO ILIYOSALIA YA AWAMU HUSIKA NA NDIO MAANA NIKASEMA BADO TUPO AWAMU YA TANO...HAISTAHILI KUWA AWAMU YA SITA. Na ndio maana hana/hakuna ilani/Dira ya awamu ya sita Kama mpango wa utekelezaji miradi na Vipaumbele vya Maendeleo kwa awamu yake mpya ya.6.

Na ukiulizwa hapa Vipaumbele vya maendeleo katika awamu ya sita ni vipi utasemaje?...na vimeainishwa wapi??...kama unavyo viweke hapa tafadhali.
 
Kama kuna watu 1000 hapa Tz ambao sio wanasiasa wala watumishi wa umma wala wafanyabiashara wanaomkubali rais samia basi nipo tayari kutoa gari yangu

Wanaomkubali Samia kwasasa kati ya watu milioni 60 huku Bara basi hata 1000 hawafiki

Nimetafuta raia wa kawaida anayemuunga mkono huyu bibi hayupo hata 1000 hawafiki nchi nzima

Hakubaliki, hapendwi wala hakuna mwenye hamu ya kumsikia huo ndio ukweli, mtaani ni ngumu sana kumkuta mtu anamkumbali rais Samia ukiachana na watumishi wachache wa umma na wanasiasa, na wafanyabiashara baadhi.

Huo ndio ukweli, mwambieni Rais ukweli kuwa hakubaliki kabisa kwa upande wa Tanzania bara.
Ukitoa wafanyabiashara ,wanasiasa na watumiaji wa uma utabaki na wakulima na wafugaji+ wanafunzi. Hao wote wanamkubali kinyama.
 
V
Hahaha!...mbona huelewi ndugu, NAULIZA HIVII KATIKA MAZINGIRA YOYOTE YALE HAKUNA MTU DUNIANI ANAYEPEWA MAMLAKA NA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YA RAIS BILA KUAPISHWA/KIAPO...AU wewe uliona wapi hii??...toa mfano hapa.

Na hakuna mahali nimesema rais samia sio RAIS KAMILI, Bali naungana nawewe kabisa hapo kusema ni rais kamili na ana mamlaka yote ya kiutendaji kama amiri jeshi na maamuzi yote ndani na nje ya nchi kwa niaba yetu watanzania(Maana ata akienda kukopa mikopo hakopi kwa jiani lake bali jina la TZ)

Mbona katiba ilishaweka wazi hili ndugu...
"Kwa mujibu wa kifungu cha 37 (5) cha Katiba ya nchi hiyo iliyotungwa mwaka 1977, nafasi ya urais inapokuwa wazi kwa sababu yoyote ikiwemo kifo, viongozi watatu wameorodheshwa na ni Makamu wa Rais, na endapo hatakuwepo atachukua Spika wa Bunge na kama hayupo atachukua Jaji Mkuu"

Hivyo "
endapo kiti cha Rais kitakuwa wazi kutokana na Rais kufariki dunia, kujiuzulu, kupoteza sifa za uchaguzi au kutomudu kazi zake kutokana na maradhi ya mwili au kushindwa kutekeleza kazi na shughuli za Rais, basi Makamu wa Rais ataapishwa na atakuwa Rais kwa muda uliobaki katika kipindi cha miaka mitano..." inaeleza katiba ya Tanzania katika kifungu cha 37 (5).

KWA MUJIBU WA MANENO HAYO HAPO MWISHONI(atakuwa Rais kwa MUDA ULIOBAKI katika kipindi cha miaka mitano..). HIVYO YEYE ATAMLIZIA TU KIPINDI KILICHOBAKIA KATIKA HIYO MIAKA MITANO ILIYOSALIA YA AWAMU HUSIKA NA NDIO MAANA NIKASEMA BADO TUPO AWAMU YA TANO...HAISTAHILI KUWA AWAMU YA SITA. Na ndio maana hana/hakuna ilani/Dira ya awamu ya sita Kama mpango wa utekelezaji miradi na Vipaumbele vya Maendeleo kwa awamu yake mpya ya.6.

Na ukiulizwa hapa Vipaumbele vya maendeleo katika awamu ya sita ni vipi utasemaje?...na vimeainishwa wapi??...kama unavyo viweke hapa tafadhali.
Vipo katika ilani aliyoinadi na kuipigia kampeni,
 
1. Tozo
2. Mgao wa umeme
3. Kenge road
4. Mabwana na Watwana
5. T..EAA kufika T..EAM ndani ya mwezi
6. Mchele kufika sh 4,000 kwa kilo
7. GSM kumleta Mayele
8. Uturuki
9. Chanjo
10. Uhuru wa reiniboo na elijibitii

Au mwananchi ulikuwa unamaanisha Uto? Mbona hayo yako wazi tu, yametugusa sisi uliotutaja!
Hayo kweli yamemgusa mwananchi...
 
Mnaweza kunambia ni kipi cha maana alichokifanya rais Samia hadi sasa ambacho kimegusa raia wa kawaida au kumsaidia??

Nambieni ni kipi kakifanya ambacho kinaweza kuwa sababu ya yeye kusema amefanya kazi ya kusaidia wananchi wake

Nataka kimoja tu ambacho kakifanya ambacho tunaweza kusema kimemgusa mtu wa chini tokea awe Rais
Kalynda E commerce ,NA HILI NALO MKALITAZAME
 
Rais wa kugusa watu wa Chini kwa kupora watu wa juu kwa kulazimisha makosa ya kubambikiana hatotokea tena Tanzania katika miaka ya karibuni

ni bora watu wabaki kuwa maskini kuliko kuwapunguzia umaskini wa kuumiza wengine
Rudia ulicho kiandika, utajigundua wewe una matatizo kidogo.
Ama labda uwe mnufaika katika mgawo wa keki ya Taifa.
 
1. Elimu bure hadi KIDATO CHA SITA

2. UJENZI WA MADARASA

3. KUPANDISHA MADARAJA YA WATUMISHI NA KUONGEZA MISHAHARA YAO.

4. KODI BILA MTUTU WA BUNDUKI NA DHULMA KWA WAFANYABIASHARA.

5. AJIRA SEKTA ZOTE (ELIMU, AFYA, ULINZI NA USALAMA, TAASISI ZOTE NK)

6. BARABARA NYINGI HASA ZINAZOSIMAMIWANA TARURA.

TUNAWEZA KUANDIKA MPAKA KESHO.

NB. CHUKI ZA DINI YAKE USILETE KWENYE MAISHA YA KAWAIDA NA KUTAKA WATU WENGINE WAMCHUKIA. ADUI WAKO SIO ADUI WETU SISI.
Hayo ya dini yamekujaje tena?
 
Back
Top Bottom