Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Kwa maneno kama hayo tu kwenye hiyo comment yako...INAONYESHA WAZI KUWA WEWE NI MWEPESI SANA KWENYE UJENGAJI WA HOJA.

Sawa sikatai naweza kuwa Mjinga lakini wewe mwerevu mbona unakimbilia kejeli?...

kwa staili hii...endelea tu kutumia kichwa chako kama kabati la kuhifadhia Meno na sio vinginevyo.

Unadiriki kuuliza kuwa "NCHI HII KUNA RAIS ALIYEFANYA MAPYA KATIKA AWAMU YAKE?"...hivi ni miradi mingapi mipya ambayo Magu aliifanya na haikuwepo awamu za nyuma??...(kwa hiyo SGR, Stiegler's Gorge kule mto rufiji sio vipya vilivyoletwa na magu katika awamu yake ya tano)

Acheni, blah...blah...blah!...tuambie miradi mipya aliyoianzisha yeye Rais samia kipindi cha hii awamu yake mpya anayosema ya.6. Na ni Kwanini hamusemi ukweli kuwa mama ameanzisha mfumo wake mpya wa kukusanya mapato kupitia miamala ya kifedha kielektronik yaani TOZO?...au haya si maendeleo tumepigwa jamani😂😂😂

USHA PANIC WEWE...
 
Women empowerment
 
Na wala sikumaanisha eti kupata ajira kwa uyo mtu...kuzuie rais samia asitoe ajira kwa wengine.

Na hakuna niliposema Magufuli alikuwa mgombea binafsi SOTE TUNAFAHAMU alikuwa ni wa CCM, Na maana ya kwamba miradi ya maendeleo iliyowepo katika ilani ya CCM awamu ya tano tunaifahamu. Na hadi ivi sasa tupo ndani ya miaka miwili ya awamu mpya ya sita...semeni kipi kipya ambacho hakijaachwa na hayati Magu kimefanywa na mama samia???

Maana itakuwa ni upumbavu leo hii Stiegler's Gorge ikamilike alafu tuseme MAMA SAMIA AMEJENGA KATIKA AWAMU YAKE YA 6. Wakati inafahamika kuwa mradi uliletwa na magu akauwacha ukiendelea kutekelezwa na bajeti yake ikiwa ilishapangwa kabisa. Tokea awamu ya tano.
 
Wewe kipi umefanya kumsaidia mumeo na watoto wako
 
Sijacomment tangia jana baada ya kuusoma huu uzi bado naendelea kutafuta.

Nikipata nitacomment.
 
Kwani mwendazake alifanya nn cha maana?
 
Kwani magufuli alikubalika na nani kiufupi hakuna raisi aliyekubalika akiwa madarakani ngosha mpaka amekufa ndo watu wanajifanya alikuwa jembe watanzania kwa unafiki
 
Kwani mbolea haujaona namna zilivyopungua Bei? Japo Sina uhakika Kama hata unafahamu habari za kilimo maana katika kusoma maelezo yako nimeona Ni mtu ambaye huna taarifa nyingi Sana juu ya yanayoendelea hapa nchini katika secta nyingi tu,Sasa Kama hufahamu ni kuwa mbolea zilipaa Sana Bei na siyo hapa tu Bali maeneo mengi tu katika Bara la afrika, lakini mh Rais wetu mpendwa mama Samia kwa umadhubuti na ushupavu wake kiuongozi akaamua kuwaokoa wakulima kwa kuamua kutoa Ruzuku ya billion Mia moja hamsini Hali iliyopelekea kushuka kwa Bei ya mbolea zaidi ya nusu ya Ile ya msimu uliopita sokoni,

Sasa je hapa wewe huoni kuwa mh Rais amewagusa wananchi moja kwa moja? Huoni kilimo Ni pumzi ya watanzania wanyonge walio wengi? Huoni hapa Ni Kama mama Amewapa pumzi mpya na Safi mamilioni ya wakulima? Huoni ameleta matumaini kwa watanzania? Unajuwa athari ya mtu kuishi bila matumaini wewe?

Vipi kuhusu bajeti ya kilimo? Unajuwa mama aliikuta Ni shilingi ngapi na kwa Sasa Ni shilingi ngapi? Unajuwa Ni vipi kilimo kwa Sasa kimekuwa na tija kutokana na juhudi za mh Rais wetu kutilia mkazo?

Najuwa huwezi ukayaelewa haya maana akili yako imefubazwa na chuki zilizojaa katika akili na moyo wako juu ya Rais wetu mpendwa, lakini utake usitake huyu ndiye Rais wako mwenye kibali Cha watanzania na ambaye amepewa baraka zote na watanzania kutuongoza Hadi 2030

Pia lazima ufahamu kuwa Ni utaratibu wa Rais yoyote Yule katika nchi yetu kufanya Kama ambavyo baba wa Taifa amewahi kutuasa kuwa unaanzia alipoishia mwenzio katika Yale mema na kurekebisha Yale yenye kasoro, huuwi ulivyovikuta Wala huviharibu ulivyovikuta Bali unakamilisha,kuendeleza na kukamilisha vilivyokuwa katika mipango na mikakati ikiwa tu vitaonekana vina faida pale vitakapokamilishwa na hapo ndipo hatua zako zinapoanza katika kuibua au kuanzisha na kutekeleza miradi mingine,mikakati mingine kulingana na bajeti itakavyoruhusu na uchumi wa wakati huo,

Amefanya hivyo Samia ,alifanya hivyo Hayati Magufuli na atafanya mwingine pia miaka ya mbele huko, kwa hiyo acha ushamba wa kiuongozi, nchi ina utaratibu wake wa kimaendeleo, chama ni kimoja kilichoongoza nchi hii na kitakachoendelea kuongoza nchi hii, kwa hiyo hakuna anayekuja kuongoza nchi utazaninmgombea binafsi, Soma uelewe , siyo kuandika tu utazani mtu alikuwa peke yake katika kwenda kufanya vibarua na kuleta hela za kujengea nchi yetu,Urais Ni Taasisi siyo mtu binafsi
 
Hayo ni mawazo ya inferiority complex, badilika uende na wakati
 
Rais Samia yupo pale kwenye nafasi ki mkakati. Naweza sema anafanya kitu tunaita katika utawala ni ku turn around nchi, kutoka kwenye mkakati wa siasa za ndani kurudi siasa za nje. Kitu alichokifanya mpaka sasa siyo kibaya ni kizuri na miaka inayokuja hata watu wenye kipato kidogo watafurahia matunda ya Rais Samia. Hivyo tunajua wanyonge hawampendi kabisa Rais Samia ila tunajua sababu kuu ni mabadiliko. Tunaamini ndani ya miaka miwili uchumi wa juu utawagusa hata hawa wa chini na watafurahia. Tuzidi kumuombea Rais Samia aendelee kutuongoza kwa vipindi vingi zaidi.
 
Hahaha!...mbona huelewi ndugu, NAULIZA HIVII KATIKA MAZINGIRA YOYOTE YALE HAKUNA MTU DUNIANI ANAYEPEWA MAMLAKA NA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YA RAIS BILA KUAPISHWA/KIAPO...AU wewe uliona wapi hii??...toa mfano hapa.

Na hakuna mahali nimesema rais samia sio RAIS KAMILI, Bali naungana nawewe kabisa hapo kusema ni rais kamili na ana mamlaka yote ya kiutendaji kama amiri jeshi na maamuzi yote ndani na nje ya nchi kwa niaba yetu watanzania(Maana ata akienda kukopa mikopo hakopi kwa jiani lake bali jina la TZ)

Mbona katiba ilishaweka wazi hili ndugu...
"Kwa mujibu wa kifungu cha 37 (5) cha Katiba ya nchi hiyo iliyotungwa mwaka 1977, nafasi ya urais inapokuwa wazi kwa sababu yoyote ikiwemo kifo, viongozi watatu wameorodheshwa na ni Makamu wa Rais, na endapo hatakuwepo atachukua Spika wa Bunge na kama hayupo atachukua Jaji Mkuu"

Hivyo "
endapo kiti cha Rais kitakuwa wazi kutokana na Rais kufariki dunia, kujiuzulu, kupoteza sifa za uchaguzi au kutomudu kazi zake kutokana na maradhi ya mwili au kushindwa kutekeleza kazi na shughuli za Rais, basi Makamu wa Rais ataapishwa na atakuwa Rais kwa muda uliobaki katika kipindi cha miaka mitano..." inaeleza katiba ya Tanzania katika kifungu cha 37 (5).

KWA MUJIBU WA MANENO HAYO HAPO MWISHONI(atakuwa Rais kwa MUDA ULIOBAKI katika kipindi cha miaka mitano..). HIVYO YEYE ATAMLIZIA TU KIPINDI KILICHOBAKIA KATIKA HIYO MIAKA MITANO ILIYOSALIA YA AWAMU HUSIKA NA NDIO MAANA NIKASEMA BADO TUPO AWAMU YA TANO...HAISTAHILI KUWA AWAMU YA SITA. Na ndio maana hana/hakuna ilani/Dira ya awamu ya sita Kama mpango wa utekelezaji miradi na Vipaumbele vya Maendeleo kwa awamu yake mpya ya.6.

Na ukiulizwa hapa Vipaumbele vya maendeleo katika awamu ya sita ni vipi utasemaje?...na vimeainishwa wapi??...kama unavyo viweke hapa tafadhali.
 
Ukitoa wafanyabiashara ,wanasiasa na watumiaji wa uma utabaki na wakulima na wafugaji+ wanafunzi. Hao wote wanamkubali kinyama.
 
V
Vipo katika ilani aliyoinadi na kuipigia kampeni,
 
Hayo kweli yamemgusa mwananchi...
 
Kalynda E commerce ,NA HILI NALO MKALITAZAME
 
Rais wa kugusa watu wa Chini kwa kupora watu wa juu kwa kulazimisha makosa ya kubambikiana hatotokea tena Tanzania katika miaka ya karibuni

ni bora watu wabaki kuwa maskini kuliko kuwapunguzia umaskini wa kuumiza wengine
Rudia ulicho kiandika, utajigundua wewe una matatizo kidogo.
Ama labda uwe mnufaika katika mgawo wa keki ya Taifa.
 
Hayo ya dini yamekujaje tena?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…