Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Mwendazake alikuwa iblis
 
Haaaaaa
 
Hawezi kupata, unadhani manjagu na jeiwii wanakubali aiuze tanganyika, never. Ongea nao uwasikie
Walikuwa wapi wakati migodi na maziwa vinauzwa na mkapa!? Tz hamna jeshi ni midoli ya wanasiasa tu!
 
Tanzania hawashindi kwa Kura za masanduku.

Wanajisumbua tu
 
Napenda kukuita Rais Samia na si mama Samia.
Sakata la bandari si dogo kama linavyochukuliwa na baadhi ya wasaidizi wako pamoja na machawa wako.
Bado serikali haija li address kwa nidhamu na undani, zaidi ni blaa blaa tu.
Jambo hili la Bandari lipo kwenye mioyo ya Watanzania,usiwaone wapo kimya kwenye hadhara lakini mioyoni wamekunja ndita.
Maofisini,mtaani na makanisani ndiyo mjadala unaotawala kwasasa.
Mpaka vijijini kwasasa wanajua bandari imeuzwa. Wananchi hawatakuambia kwenye mikutano yako ya hadhara lakini amini vichwa vyao vimeinama.
Kama leo ikipigwa kura ya kupima namna unavyokubalika si ajabu kama haitafichwa basi unaweza kuwa na asilimia 40 tu ya kura zote.
Nini kinatafuna serikali unayoiongoza?
1. Unawasaidizi wengi waliojaa viburi Sana. Nadhani umemsikia kiongozi wa mbio za mwenge Taifa akilalamika kujibiwa kwa jeuri na mkurugenzi mmoja. Hebu fikiria kiongozi wa mbio za mwenge anajibiwa kwa jeuri. Mwenge upo kwenye itifaki ya Rais. Sasa kama yeye anakumbana na kadhia hiyo, mwananchi wa kawaida itakuwaje?
2. RUSHWA. Kwasasa hakuna ubishi. Jamaa Hadi wanasema ukishindwa kutoboa kwenye serikali hii basi wewe imeshindikana.
3. Serikali ya machawa. Hapa kazi ipo. Wanaokunadi ni wale ambao jamii imewadharau. Wananchi pia wanaelewa penye kazi inachapwa wanaona penye ubabaishaji wanaona.
4. Una mawaziri wengi mizigo. Sina haja ya kuwataja.
5. Huduma za kijamii zimelegea. Hospitali,shule( hapa kwenye shule kuna tatizo kubwa),pamoja na maeneo mengine.
Mwisho.
Usikubali kuitwa majina mazuri na pongezi hewa ili watu walinde vibarua vyao. Usipofanya maamuzi magumu ya kuondoa wasaidizi mizigo na wewe kuwa mtumishi wa watu ,ya 2015 yatajirudia na 2025 mtatafuta mtu wa kumvisha mabomu akakomboe chama
 
Samia inaonekana hajakua rais wa tanzania kwa bahati mbaya ila ni mpango wa uovu dhidi ya uhuru wa nchi yetu. Watanzania hawajawahi kuona ubabe kama ulivyoonyeshwa leo toka uongozi wa ccm. Kulazimisha kuendelea kutekelezwa mkataba wa kukabidhi bandari za tanzania bara kwa masharti kama kumilikishwa kampuni ya DPW mali ya sultani wa dubai. CCM isiyokua sikivu kwa wananchi lazima itang'olewa tu madarakani.

Mkataba wa kihuni na ufisadi wa serikali ya samia kukabidhi bandari za tanzania bara kwa usultani wa dubai kuzidhibiti kama milki yake ndio bila shaka itakua chachu ya kuhitimisha uongozi wa ccm tanzania. Samia mwanzo wa uongozi wake akihojiwa na shirika fulani la habari la magharibi alisema asingejali sana ccm kushindwa katika uchaguzi.

Bila shaka waarabu wakishapewa udhibiti wa bandari zetu watachafua hali ya kijamii kwa kuhonga kila mtu na hata chaguzi zitaharibika ili kutetea chama kitakachoendeleza ubeberu wa DPW tanzania. Ila watanzania wana sifa ya mshikamano mkubwa kukabiliana na mabwanyenye wa ndani na ubeberu wa nje.
Mungu ibariki tanzania. Tutashinda tu.
 
2025 mbali hivyo? Ona hii July iishe, save hii comment
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…