Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Anayejua Rais Samia Suluhu anatupeleka wapi atuambie, naona kama tunapotea

Unafiki wake nini, mbona hayati nae alikuwa hivo hivo wakati anamuambia JK asafir tu ili alete mahela, alivoingia unakumbuka akasemaje na akatendaje?

Mtateseka sana, nchi imechukuliwa na CDM kiulaini bila hata push up yani.
Wacha uchonganishi CDM wametoka wapi? Nchi ni ya CCM ila imepata Rais mwenye Busara sana
 
Hata huyo Jpm wakati "tukiibiwa mmno" kama alivyodai yeye alikuwa waziri!! Mbona hakujiuzulu? Ngoma inachezwa kuendana na mdundo!! Ukishindwa kabisaaa ndo unajitoa sio kila mkitofautiana unazirazira kazi!!
Tatizo katiba imemfanya raising asiweze kupingwa hasa akiwa mkatili atakuita kibaraka was mabeberu mwisho atasema unasaliti vita vyakiuchumi hapo yatakukuta makubwa yalisu chamtoto!!
Ndio mimi nkawauliza wameshawahi kushika hata nyadhifa ndogo tu katika jamii??

Eti wanaleta mambo ya kufkirika hapa ya kwanini hakujiuzulu. Wanadhani unajiuzulu tu simple simple???
 
Kifo cha huyu mh kimenifikirisha sana...

1.afya yake ilienda inadhoofika kadri mda unavyoenda..ukiangalia sura yake katika picha tangu december hadi feb siku ile amesimama kanisani st peter utaona mabadiliko makubwa..wenye jicho la tatu tulijiuliza kulikon mh anazid kudhoofika kila kukicha na waliomzinguka hawaoni hali hii?...siku ile anamuaga kijazi alipoingia pale kalimjee nikamwbia rafiki yangu mmoja kuwa pamoja na msiba huu mzee hayuko sawa iko shida kubwa inamsumbua..kwa nini wasaidiz wake waliacha hali hii huku wakijua kuwa huyu Mkuu wa nchi..kama walimshaur akatibiwe akakataa kwa nini hawakutumia utaratibu unaofaa kumfanya akatibiwe?..mana watu baki tulikiwa tunaona kabisa mzee hayuko sawa..lakini pia kingine yeye mwenyewe kwa nini hakujali afya yake wakat hali halisi ilikiwa inajionyesha?..aliweka nchi mbele kuliko afya yake..ona sasa kabla hajafika chato kuzikwa tayari kiti kilikuwa kimeshapata mtu wa kukali!!!...je walikiwa wanamuogopa kumwambia ukweli..hawakujua shida iliyokuwa mbele yake?...shida ya moyo kwa zaidi ya miaka kumi bila checkup!

2..Magufuli alikiwa anaongoza watu amabo yeye akiwaangaloa machoni anawaona kama ni watu watiifu sana wenye kutii kila asemacho..lakini ukweli ni kwamba waliokiwa karibu nae na wengi waliokuwa wakiimba mapambio ya kumsifu na kumuabudu wengi walikuwa wameshamuasi kifikra..wengi walikuwa upande wake kulinda maslah yao na hili linaonekana wazi hasa wiki mbili hiI baada ya kuzikwa...wengi hawakupenda sera zake na namna anavyoongoza nchi bila kujali kujali katiba
Mzee wangu mmoja alinipa lift kwenye gari yake akaniambia jambo ambalo nimelitafakari baada ya kifo chake..mzee alisema magufuli ni kiongozi anayejenga nchi na sio taifa..iko tofauti kubwa kato ya nchi na taifa akaemdelea kusema ..hii itampa kazi sana katika kujenga nchi hii na akumbuke kuwa nchi hii hakuikuta ikiwa jangwa kwamba yeye ndie anaanza kuijenga kana kwamba wenzake waliotangulia hawakufanya kitu..nikamuuliza kwa vipi baba..mzee akasema kwa sasa huwez kujua ila utajua baadae ila nachokwambia anachokijenga hakitamfikisha popote..mzee akaishia hapo
Lakini pia magufuli hakuwa anazijua beacon za nchi hii..wapo wanaojua beacon za nchi hii yawezekana wako ndan au nje ya nchi..aproach nyingi za magufuli hazikiwavutia wengi kwenye inner cycle...maneno mengi ya kunanga watanguliz wake ,lugha za kibabe na kibaguzi(mfano mkichagua wa chama kile sileti maji..sikuleta maana hapa mlichagua wa chama kile nk)..waliompandisha kufika hapo wengi aliwakanyaga na kuwatupa nje..lakin pia wasaidizi wake wa karibu walikuwa nakaz ya ziada...njoo kwenye hili la corona alitumia ligha za hovyo wakat mwingine na kukatisha tamaa..watu nyeti sana wamepukutika..huko jeshin na ndan ya Tiss wazee kibao wamekifa na corona lakin yeye kama mkuu wa nchi hakutaka kutoa kauli yenye uelekeo..jana samia kachukua point tatu muhim..ubabe ubabe wake haukuwa na tija..
Siku ile mwaka jana amekufa mkapa kuna kitu nilijiuliza sana...maana nadhan fomula iliyotumika ni kumpiga mchungaji na kondooo watanyike ili tuwapate kirahisi.sasa angalia trend tangu amekufa mkapa..lakini pia vifo vya hawa wasaidizi wake waliotangulia kufa kwa kufatana sana na mwisho akafa yeye..binafsi nimekataa kuwa ni corona iliwaondoa wale kwa haraka haraka au corona ilitumika kama cover...vile vifo vya wasaidizi,wake na jamaa zake vilimpa wakat mgumu sana..sijui kama kuna mwingine aliyekuwa karibu nae atakufa baada ya kufa yeye akitokea hapo ikulu...deep state wanajua namaanisha nini..ila sisi wengine tunaoishi kwenye hii dunia ya chai na sukar hatuwez kujua lolote..so huenda akawa fixed maana sasa unaweza kuona kwa haraka kabla ya 40 sera zake zikibadilishwa..watu wakionyesha wazi waz alivyokuwa hayuko fair katika kaz zake..full ubabe..kuna kauli ameitoa Mh.Rais wa sasa jana iliyoonyesha huko ndan wakat wa hayati akiwa kwenye kiti mambo hayakuwa shwari..huwez kuendesha nchi kwa misingi ya kidikteta wakat umeshika madaraka toka kwenye sanduku la kura..ingekuwa kashika madaraka kwa mtutu kidogo ingesaidia..he was not safe...
Mienendo yake ya uongoz haikuashiria mwisho mzuri na ndio maana hata humu jf kuna thread ziliwekwa mwaka 2017,2018,2019 zote kutabiri kiwa huyu mwamba asingetoboa miaka 10 ya uongoz..

3..mataifa ya nje ushirika wao sidhan kama upo sana japo wengi hawakupenda sera zake...na kama upo basi wamewatumia watu wake wa karibu walioasi kifikra ili kumpata ila binfsi naona uhusika mkubwa wa humu ndan na yeye mwenyewe kutokisoma alama za nyakati na kutokujali afya yake..huwez kuwa na maradhi ya moyo halafu unakuwa mtu wa dizaini ile halafu uaeme utaishi maisha marefu yenye fanaka...
Ninarudi pale pale kwa yule mzee wangu..huwez kujikita kujenga nchi badala ya kujenga taifa halafu ukawa salama..taifa hili lina misingi yake..
 
Mama Samia ndio mwokozi, Watanzania walikuwa wanamsubiria. Praise team mtahama nchi.

Mnafiki ni yule aliyekuwa anajifanya mtetezi wa wanyonge kumbe hana lolote.

Eti tunajenga kwa fedha zetu za ndani, kumbe ni fedha za mikopo.

Akwende zake huko akaongoze malaika.
Nikuulize jomba kwa uelewa tu...fedha za mkopo huwa zinatokea wapi..kwanza wewe bado unasoma au umemaliza...nadhan hujitambui...jukwaa hili sio saiz yako..fedha za mkopo Ni nani anatakiwa kulipa mikopo...hizo hela za kulipa mikopo zinatokea ndani au zinatoka nje ya nchi..labda tuanzie hapa...wenye kutokuwa na akili za uelewa mpo wengi kumbe..ndio maana nchi yetu inapata shida kuendelea
 
Mfano wa kuacha kukusanya kodi kwa mabavu na kutumia akili

Ni pale tulipoachana na kodi ya kichwa, na kuingia kwenye kodi kwa mfumo wa VAT

Na mapato yaliongezeka maradufu
 
Sidhani kama unasema ukweli kuwa VP wa wakati huo na sasa Ras wetu ni mnafiki kwasababu yeye alipoanza ziara ya TANGA; mwendazake alikuwa mahututi lakini anazungumza hivyo hizo salaam alimpa kweli, wanafiki ni wale waliotoa salaam na wengine hata kudiriki kusema kuwa walizungumza nae kwa simu huku wakijua aliisha kufa!!! Kumuweka kundi moja na hao wanafiki sio sawa. Wanafiki kati ya hao mawaziri wake wanajulikana kwani wao cha msingi ni kujaza matumbo yao tu na sio kuwatumikia wananchi.
 
CCM Siyo ya kuiamini tena, laiti ningekuwa mmojawao baada tu ya matamshi hayo ningejiuzulu maana UNAFIKI ndio umethibitika rasmi hata kama kwa sasa wanajidai kutaka kujisafisha wameshaharibu taswira ni bora chama cha ADC kishike dola. Yuko wapi mama Sendiga?

Watu walikuwa wanawashambulia wanaharakati fulani kuwa ni wasaliti kumbe hao hao waliokuwa wakipiga kelele hizo ndio wasaliti na wanafiki namba moja.
1. Viongozi wa chama anachotoka hayati sio waungwana, wanafiki na inawezekana walidhamiria kumkatilia mbali kwa sababu wanazozijua bila kutafakari athari za muda mrefu ambazo kwa vyovyote vile haiwezekani kuzitibu na huenda kanda atokapo hayati ikaamua kukisurubu na kukifutilia mbali chama hicho huko na kwamba ni bora kurejea kwenye vyama mbadala. Hao watu ni wakimya, wapole, wanajulikana kama washamba na waliochelewa lakini wafuatilie ni kitu gani walifanya kwa Wajerumani, Waarabu wakaishia Kayenze, Nyerere alifanyiwa nini uwanja wa Nyamagana, Tabora, Shinyanga na Mara.
2. Wasaidizi wa Rais kuhusu usalama
3. Daktari maalum wa Rais
4. Wasaidizi na washauri wakuu wa Rais

Kwanza kitendo cha viongozi wa ngazi za juu kufanya ziara mikoani ndani ya muda ambao tetesi za hayati kuugua zikiwa zimeshika kasi ni uthibitisho kwamba ni sharti wawajibike kwa kuwahadaa waTanzania. Huwezi kumdanya Mtanzania eti Rais anawasalimia na anahimiza kuchapa kazi huku ukijua ukweli ni kinyume chake. Maana kila ukifanya ziara popote ndani ya eneo la utawala unatakiwa kuwa unampa taarifa mkuu wako wa kazi sasa ilikuwaje mmoja yuko huko Kaskazini kwa ziara ya siku sita na mwingine ziara huko Kusini huku kauli zikipishana? Wakato mmoja akiwaambia wananchi Rais anawasalimi lakini alipopewa kero za wananchi akadai atamtuma waziri husika kuja kufuatilia kero hizo kitu ambacho kwa miaka zaidi ya sita alikuwa hatoi kauli kama hiyo zaidi ya kusema atawakilisha kwenye mamlaka husika?

Taarifa tatu zinazokinzana zinatakiwa zitolewe ufafanuzi na uthibitisho ikielezea sababu za kitalaamu za kifo kwamba
1. Hayati aliugua ugonjwa wa moyo ghafla aina ya 'Atrial Fibrillation'
2. Hayati alishambuliwa na vimelea vya UVIKO (COVID-19) kama inavyodaiwa na mkosoaji wa hayati aliyeko huko Ubelgji
3. Hayati alifariki kati ya tarehe 6/3 na 9/3/2021 lakini ikafanywa siri hadi vuguvugu la mapinduzi lilipotaka kutumia nafasi hiyo kutwaa madaraka ndipo makamu wa Rais akaamuriwa sijui na nani kutangaza kifo akiwa ziarani huko mkoani Tanga wakato awali aliwaaminisha wananchi Rais ni mzima akiendelea na majukumu yake na kwamba aliwataka kuchapa kazi!!!

Wafuatao kwa namna yoyote wanawajibika kutoa wingu kwamba hawakujua kilichokuwa kinaendelea kuhusu ugonjwa, kupelekwa nje ya nchi na kurejeshwa kisirisiri pindi taarifa zilipovuja.
1. Makamu mwenyekiti wa chama tawala
2. Katibu mkuu wa chama tawala (kama yupo)
3. Katibu Itakadi na uenezi wa chama tawala
4. Makamu wa Rais (maana inasemekana wakati tetesi zimeanza mwanzo kabisa alifuatwa kutoka Zanzibar na akaongezewa ulinzi kisha yeye akaanza ziara mkoani Tanga wakati sintofahamu ikiiendelea)
5. Waziri mkuu ambaye mara kwa mara alikuwa akifanya ziara nyanda za juu Kusini na kukatishakatisha ziara hizo bila kuweka sawa kilichokuwa kikitolewa taarifa kutoka kwa Watanzania walioko nje ya nchi;
6. Mkurugenzi usalama

*Masuala yaliyopo hapo juu ni ya mhimu kuteguliwa sasa ili hali ya hewa iendane sawia na mabadiliko yanayoendelea hivi sasa kwa utawala ulipo madarakani ijapokuwa sio mpya (Chama kile kile chenye mjumuiko wa makundi yanayosigana kupambania madaraka chini kwa chini)

*The north exists in the presence of south whilst the west and east conveniently interacts with the former and latter steadhold polarized pillars.
 
Sidhani kama ana vision

VISION YA RAIS NI KUWALETEA MAENDELEO WANANCHI KWA AMANI kwa kutumia vizuri rasilimali za chi yetu. Kumbuka vision ya mwendazake ndio hiyo hiyo ya Rais Samia kwani wote wanaongozwa na ILANI YA UCHAGUZI YA CCM!
 
Pole for your loss bro , jipange upya utafute kibarua ushiriki kwenye ujenzi wa taifa sasa zama za ujanjaujanja zimeshapita
"KAZI IENDELEE."
Zama za kusifia sifia na kuabudu ili upate uteuzi zimepitwa na wakati

😀😀😀😀

Kila milio itasikika
 
Mama Napwaya Sana.
Yaani Mama as if alikuwa sio sehemu ya Baraza la mawaziri.

Wacha tuone hii cheap popularity inako mpeleka.

Huyu ataishia kuwa omba omba huko ng'ambo.
Kwani rais gani wa nchi hakuwa hakuwa ombaomba?

cheap popularity? Mtu asifanye kazi kisa aogope maneno, henu tumia akili

waliopanguliwa hawakuwa good enough, amefanya immediate fix kwa kuwapangua ili apate quick results ila akipata muda atawaondoa wemgi sana.....

mridhike na uwanja wa ndege, hospital, ajira nyeti kwa ukanda na daraja vinatosha sana.
 
Madam yupo sawa
May Mosi anamaliza kabisa
Tulieni ni zamu yake chokochoko hazitatusaidia
Ni kazi kubwa! Wafanyakazi wanataka ongezeko la mishahara, wafanyabiashara wanataka mishahara ipungue (maana yake kodi ipunguzwe), kazi kwake SASHA.
 
Mama Samia achana na cheap popularity haitakusaidia lolote unatakiwa usiwe muongeaji sana maana naona unaanza kutoboa matundu ya hela wakati huo ukiwa umewekwa kwenye mtego mgumu na mzito sana wa ilani yenye kurasa 300 ya kutekeleza miradi yote iliyoko kwenye ilani

Yaani kumbuka sasa hivi hauko kwenye meli mpya uko kwenye meli ileile sema tu imepata mawimbi katikati ya safari

Mama nimekushangaa sana unaposema kuna miradi mingine iko kwenye makaratasi wakati wewe na Hayati Magufuli ndio mliotembea nchi nzima kuinadi kwa hiyo tunataka ahadi zilizoko kwenye ilani ya Chama cha Mapinduzi

Tofauti na hapo hatutakuelewa tutanyima kura 2025 kama ukitaka kuomba ridhaa ya kugombea tena

Jitahidi sana kwenye suala la kodi usiwalaumu tu TRA waonye hata wafanyabiashara pia maana ni wakorofi.
Mwendazake aliipeleka gari porini, mama anarudisha gari njia kuu.

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu watu ni wajinga sana..hawajui wananchi wanahitaji nini na mama nae kafuata huo huo mkumbo..sio kwa zile hotuba zake yaan hata kuziskiliza ni kero..anataka turudi enzi za kina jk.kuchekeana chekeana.. hatutaki uswahili kwenye masuala ya kulipa kodi kwenye masuala ya rasilimali za nchi..
Time will tell..JPM will never be forgoten.
Kwa hiyo ww unataka watu waendelee kutekwa Kama Zama zilizopita ? Wapi Ben saa nane , wapi azory , ?
 
Wee ukianza kutongoza Mwanamke kumuoa unaanza kumshawishi kwa kutaja furaha za ndoa au changamoto?

Sasa hivi tuna changamoto kubwa ya kurudisha Uwekezaji na njia bora ni kuwaaminisha mazingira kuwa yameboreshwa sio kuanza kuwapa maangalizo
Wawekezaji gani hao ambao Afrika hii huwa inalilia? JF nako tumeingia ujinga wa wansiasa waliofeli kugundua wapi wanakotupeleka? Hadi siku ya leo Samia hajasema ni wapi anataka kuipeleka nchi hii. Yuko bize kugeukia upande wa pili wa safari ya mwenzake bila kujua anaelekea wapi!
 
Back
Top Bottom