DOKEZO Angalizo: Utapeli na wizi kwenye maduka ya Pharmacy/ biashara ya dawa za binadamu

DOKEZO Angalizo: Utapeli na wizi kwenye maduka ya Pharmacy/ biashara ya dawa za binadamu

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Mimi nina mfano halisi sababu chaka langu la tonge la kila siku napatia kwenye afya za watu,kuna hizi dawa kama antibiotics ambazo sio common mtaani bei ya hasa amoxclav huwa tuchukua 4000 ila tunaipiga 12 maeneo yetu japo na mimi kuna sehem nilibamizwa kuna changamoto ya afya ilinikumba ni dawa ya kutuma muda mrefu kidogo nilitumia kidonge kimoja kila siku karibia miaka mitatu sasa nilikuwa mkoa wa katavi kidonge ilikuwa 150 sasa nikasafiri kwenda musoma huko nikiamini bei ni moja nitachukuwa huko basi kufika musoma mjini kabla ya kwenda kijijini nakuoelekea basi kupitia famacy moja nauliza wanauza mia sita kidonge kimoja na wanatoa kwa kibali cha dakitar na wanaangalia kaandika za miezi mingapi nikiangalia nimeambiwa nimeze kwa miezi mitatu kabla ya kurudi kwa tabibu kupiga hesabu ni 54000 du nilikacha na nikasema japo dawa ina withdral side effects nyingi nitakaza hadi nirudi mpanda kule pa 150 na vidonge kumi wanakupa kwa hiyo huku nako ni jipu,tangu kikwete airuhusu afya kuwa biashara huria basi ni kujipigia tu,ila wakuu sijui hii hela ni ya laaana maana ningumu kumwona jamaa kwenye afya kuwa na ukwasi wa kutisha labda wale wenye hospital zenye majina
 
Mimi nina mfano halisi sababu chaka langu la tonge la kila siku napatia kwenye afya za watu,kuna hizi dawa kama antibiotics ambazo sio common mtaani bei ya hasa amoxclav huwa tuchukua 4000 ila tunaipiga 12 maeneo yetu japo na mimi kuna sehem nilibamizwa kuna changamoto ya afya ilinikumba ni dawa ya kutuma muda mrefu kidogo nilitumia kidonge kimoja kila siku karibia miaka mitatu sasa nilikuwa mkoa wa katavi kidonge ilikuwa 150 sasa nikasafiri kwenda musoma huko nikiamini bei ni moja nitachukuwa huko basi kufika musoma mjini kabla ya kwenda kijijini nakuoelekea basi kupitia famacy moja nauliza wanauza mia sita kidonge kimoja na wanatoa kwa kibali cha dakitar na wanaangalia kaandika za miezi mingapi nikiangalia nimeambiwa nimeze kwa miezi mitatu kabla ya kurudi kwa tabibu kupiga hesabu ni 54000 du nilikacha na nikasema japo dawa ina withdral side effects nyingi nitakaza hadi nirudi mpanda kule pa 150 na vidonge kumi wanakupa kwa hiyo huku nako ni jipu,tangu kikwete airuhusu afya kuwa biashara huria basi ni kujipigia tu,ila wakuu sijui hii hela ni ya laaana maana ningumu kumwona jamaa kwenye afya kuwa na ukwasi wa kutisha labda wale wenye hospital zenye majina
Hujawaona sekta ya afya wenye hela? Nimesoma nao na nilitakiwa niende sekta hiyo, ninao wengi wenye hela ninawaona. Wamiliki wa huduma/biashara sio wafanyakazi.
 
Hawa wanaoshangaa hapa wajichanganye waende Dubai sijui kutembea umeandaa bajeti ya nauli go & return 1.5M na malazi kule lets say 1M vichochoroni umepanga ukae siku 6. Fika uko uumwe malaria tu uone moto wake.

Au jichanganye pewa mwaliko Marekani si unakuwa mtumishi kanisani kwenu, fika uko usikate Visitor Health Insurance alafu umwa ndio utajua dunia duara.

Watu wanaenda nje na mlundikano wa madawa just in case. Malaria, painkillers, minyoo, mafua na kikohozi. Ukijifanya kwenda uko utalipia dawa zao bill inakuja kuja kuliko bajeti nzima ya kukaa uko.
Ujerumani hawana kabisa dawa za Malaria.

Sitasahau.
 
Japo sijaelewa exagualation ni kitu gani ila dunia ya sasa ipo kwenye fingertips kama una akili sawasawa ingia tu Google bila kudhalilisha mtu ujiridhishe, that simple! Nimeongelea biashara in general, ni sawa na kununua jezi ya simba kwa vunja bei kwa laki wkt China haizidi sh 3000 ni maamuzi tu, dunia ina kila aina ya choice kiongozi
😅😅 Ku exaggerate Jambo mfano wewe ni observer wa Jambo / tukio Fulani
Mfano umeenda chooni ukakutana na nzi wakubwa wakubwa
Akatokea mtu akakuuliza wewe ukasema umeona NZI WAKUBWA KAMA TEMBO CHOONI
Huko ndipo ku exaggerate Jambo 😅😀😂
 
Ujerumani hawana kabisa dawa za Malaria.

Sitasahau.
Kuna nchi zimefanya eradication of malaria ukienda uko kichwakichwa utajua hujui, tupe mrejesho ilikuwaje mkuu.

Alafu afya ni biashara kama biashara nyingine, sasa wabongo ujima na ujamaa umewalemaza wao wanataka ununue dawa kwa 40,000 uuze kwa 60,000 wakati ina expire, inaweza sababisha kesi, kusoma mpaka upate kibali ni mbinde, regulations za duka la dawa ni ngumu. Wao wanataka biashara ya nihurumie.
 
Habari za wakati huu ndugu zanguni.

Kama ilivyo ada na kawaida kuhabarishana habari mbali mbali zenye manufaa kwa ajili ya kuepushana na mambo yanayoonekana kutuathiri kwenye jamii na familia hii kwa ujumla wake.

Nimepata bahati mbaya ya kumuuguza mgonjwa hapa nyumbani kwangu mwenye ugonjwa wa muda mrefu anayelazimika kutumia dawa fulani kwa kila wiki.

Hali hiyo ilipelekea kuwa na bajeti ya kiasi cha Elfu 20 kila wiki ili kukidhi mahitaji ya mgonjwa wangu kimatibabu kwa maelekezo ya Daktari wake.

Nilikuwa navichukua kwenye pharmacy za mitaani wakinihakikishia kuwa dawa za namna hiyo ni adimu sana na hivyo ni ghali.

Walikuwa wananiuzia kila kidonge kiasi cha Elfu mbili.

Kuna siku ikatokezea pale wakawa hawana zile dawa, nikaona anamuita kijana wa boda boda ingawa walitaka kufanya siri lakini niliibahatika kunasa maongezi yao na kujua anapomuelekeza kwenda kuchukua.

Nikasikia jina la duka kubwa la pharmacy kubwa hapa Dar es salaam ambapo mimi mwenyewe nalijua lilipo.

Nikafanya maamuzi ya kwenda kununua huko nikamwambia basi siku nyingine nikamuona akawa mbishi kidogo lakini nikakomaa.

Kufika kule( huko kwenye hilo duka kubwa maarufu) nikakuta kule vile vidonge vinauzwa 6,000/= vyote kumi nilishtuka sana kutoka 20,000/= mpaka 6,000/= lakini ndio basi tena ikawa nimeshapigwa, yule binti mpaka leo ananionea haya.

NB: Nawasihi ndugu zanguni kama una uhitaji au matumizi ya dawa fulani wa muda mrefu jitahidi walau uzungukie maduka matano makubwa kujiridhisha maana hawa ndugu zetu wanaouza madawa wamepanga kuwa matajiri kupitia afya zetu na wapendwa wetu tunao wauguza.
Kwani wewe hujui Daslade Kila kitu Kiko Exaggerated and total manipulated? Kama tu mfano gharama ya kitu kama Cake ambayo mikoani inauzwa 20K Dar wanauza 50k ukiuliza kwa nini wanadai Decor Pumbavu Kwani watu wanaenda kula hayo Marangi rangi ya Urembo na Ukiharisha infact Dar Kila kitu Kiko
 
Nilichojifunza kwa hapa dar kama ni mtumiaji wa dawa endelevu jaribu sana kununua kwenye maduka wanayouza madawa kwa jumla na rejareja.

Bi. Mkubwa ni mgonjwa wa sukari na kuna dawa anatumia kila siku. Nilikuwa nanunua pharmacy moja tabata ambapo kuna dawa walikuwa wananiuzia dozi moja laki na 15.

Siku moja nikiwa katika mizunguko yangu nikakumbuka dawa zinakaribia kuisha, nikaingia Mdee Pharmacy Mnazi Mmoja, dawa zile zile nilizinunua 45,000. Kuuliza utofauti mkubwa wa bei wakasema wao wanauza bei ya jumla sababu wananua bohari kuu moja kwa moja.

Biashara ya dawa za binadamu ina upigaji na uchakachuaji mkubwa sana.
Sasa hapo umepigwaje na wakati wao wamekuambia wanachukua moja kwa moja BOHARI KUU
 
Kuna nchi zimefanya eradication of malaria ukienda uko kichwakichwa utajua hujui, tupe mrejesho ilikuwaje mkuu.

Alafu afya ni biashara kama biashara nyingine, sasa wabongo ujima na ujamaa umewalemaza wao wanataka ununue dawa kwa 40,000 uuze kwa 60,000 wakati ina expire, inaweza sababisha kesi, kusoma mpaka upate kibali ni mbinde, regulations za duka la dawa ni ngumu. Wao wanataka biashara ya nihurumie.
Mwaka 2015 nilibahatika kwenda Frankfurt bana.
Nilitoka na Malaria huku Tz, nilikuwa sijui.

Ilibaki kidogo nikate moto.

Kuna Mtumishi mmoja alijiongeza kuniagizia mseto kutoka Moshi ndio ikawa pona yangu!!

Siendi tena Ulaya bila kuwa na dawa, zile muhimu muhimu.
 
Wizi tu

Juzi nimeenda kununua vidongea vya kuzuia Allergy

Nimepigwa vibaya Sana

Nadhani hawafikirii Mbali hawa wadada wa pharmacy
 
Kama wauzaji wa Misoprostol wanapiga bei kinyama kuanzia elfu 30 hadi 60 kwa vidonge vinne wakati wao wananunua kwa 500 mpaka 1500 kidonge kimoja. Sema huku nilipo kuna duka nimeliotea wananiuzia buku 12 tu ila maduka mengine kuanzia 20 na kuendelea
 
Kuna pharmacy nilienda Sina hamu, nilinunulishwa dawa Aina 2 tofauti zote zinafanya kazi moja, nilivyotumia nikaanza kuzidiwa, nilipomuona doctor akaniambia nilipaswa kunywa Aina moja tu na sio zote kwa pamoja.
 
Habari za wakati huu ndugu zanguni.

Kama ilivyo ada na kawaida kuhabarishana habari mbali mbali zenye manufaa kwa ajili ya kuepushana na mambo yanayoonekana kutuathiri kwenye jamii na familia hii kwa ujumla wake.

Nimepata bahati mbaya ya kumuuguza mgonjwa hapa nyumbani kwangu mwenye ugonjwa wa muda mrefu anayelazimika kutumia dawa fulani kwa kila wiki.

Hali hiyo ilipelekea kuwa na bajeti ya kiasi cha Elfu 20 kila wiki ili kukidhi mahitaji ya mgonjwa wangu kimatibabu kwa maelekezo ya Daktari wake.

Nilikuwa navichukua kwenye pharmacy za mitaani wakinihakikishia kuwa dawa za namna hiyo ni adimu sana na hivyo ni ghali.

Walikuwa wananiuzia kila kidonge kiasi cha Elfu mbili.

Kuna siku ikatokezea pale wakawa hawana zile dawa, nikaona anamuita kijana wa boda boda ingawa walitaka kufanya siri lakini niliibahatika kunasa maongezi yao na kujua anapomuelekeza kwenda kuchukua.

Nikasikia jina la duka kubwa la pharmacy kubwa hapa Dar es salaam ambapo mimi mwenyewe nalijua lilipo.

Nikafanya maamuzi ya kwenda kununua huko nikamwambia basi siku nyingine nikamuona akawa mbishi kidogo lakini nikakomaa.

Kufika kule( huko kwenye hilo duka kubwa maarufu) nikakuta kule vile vidonge vinauzwa 6,000/= vyote kumi nilishtuka sana kutoka 20,000/= mpaka 6,000/= lakini ndio basi tena ikawa nimeshapigwa, yule binti mpaka leo ananionea haya.

NB: Nawasihi ndugu zanguni kama una uhitaji au matumizi ya dawa fulani wa muda mrefu jitahidi walau uzungukie maduka matano makubwa kujiridhisha maana hawa ndugu zetu wanaouza madawa wamepanga kuwa matajiri kupitia afya zetu na wapendwa wetu tunao wauguza.

Nafahamu magonjwa ni faragha ya mhanga, lakini kama ulitaka kutusaidia ukataja ni vidonge vya kaswende sugu, nani jamvini angekujua Kikulachochako amepata kaswende ?
 
Back
Top Bottom