Asikudanganye mtu, vitabu ni chakula muhimu sana cha akili

Asikudanganye mtu, vitabu ni chakula muhimu sana cha akili

Nafikiri ni kwenye hicho, if I have not mistaken, Napoleon Hill kasimulia kisa kimoja cha mfungwa aliyekuwa amehukumiwa kifo, wanasaikolojia wakamfanyia jaribio la kumwua kwa maneno na wakafanikiwa. Unaweza ukashea kidogo? Nilikisoma siku nyingi, more than ten years ago.
Naaam ni hiki hiki Ila
Topic inaitwa pleasing personality
 
Kwa mnaosoma vitabu nashauri soft copy ziwe mfumo wa epub na si pdf . EPUB inakupa option nyingi na inakuwa kitabu kabisa tofauti na hizi pdf . EPUB ni kitabu halisi ingawa inahitaji application nzuri kuweza kuifungua. Kwa wanaotumia iPhone ipo app ya books by default , Kwa android unaweza ingia play store.
 
Mkuu kama w
Sijasoma vitabu vingi sana, lakini alau nimevisoma soma kidogo.

Katika kipindi cha miaka kumi iliyopita, nimeweza kusoma Vitabu vichache, vikubwa kwa vidogo, vinavyozidi mia nne.

Nimeiona faida yake. Kuna faida sana. Ni CHAKULA muhimu sana cha akili, hakika!.

Mara tu baada ya kuianza hiyo tabia, nilijaribu kuwashawishi baadhi ya watu, hasa wasomi, kuiga hiyo tabia. Kuna siku, nafikiri nilikosea, nikaenda kumshawishi mtu aliyenizidi kitaaluma naye awe msomaji. Alichonijibu kilinifanya nisirudi kwake tena kwa sulala hilo. Niliamini, usomaji wa Vitabu ungweza kumwongezea mawazo ya kuboresha shughuli alizokuwa akizifanya.

Siku ya kwanza, pengine alinivumilia, hakunijibu chochote.

Nilipoamua kumpelekea orodha ya vitabu nilivyoamini kuwa vingemfaa, aliishia kunijibu, "hivyo Vitabu havifanyi kazi Tanzania"

Havifanyi kazi Tanzania? How? Kisa tu vilikuwa vimeandikwa na Wazungu? Iweje visifanye kazi Tanzania, wakati vingi ya Vitabu alivyovitumia Chuo Kikuu vilitoka kwa Wazungu?

Namshukuru Mungu sikutetereshwa na kauli yake, ila na mimi sikurudia kumshawishi katika hilo. Niliendelea kujisomea, na sasa imeshakuwa ni tabia yangu.

Nahisi, maarifa niliyoyapata kwa kujisomea mwenyewe vitabu nilivyojichagulia, yamenisaidia zaidia kuzidi maarifa niliyoyapata chuo kikuu.

Vitabu, hasa Vitabu vizuri, haviwezi kukuacha kama ulivyokuwa. Ila ukivisoma "visivyo" salama kwa akili, utakuwa hatarini pia.

Soma vitabu vizuri, hutajutia.

Wanasema, LEADERS ARE READERS!

Soma VITABU, Vitabu vizuri! Vina faidi tele!

Dhamini Vitabu kuliko unavyoldhamini chakula cha kawaida, ni CHAKULA muhimu sana cha akili ya
Mkuu kama ww umesoma vitabu huku hata kuandika kiswahili huwezi ni bora usiendelee kusoma!dhamini hapo imetumikaje?mbona sioni uhalali wa dhamini hapo!!
 
Kwa mnaosoma vitabu nashauri soft copy ziwe mfumo wa epub na si pdf . EPUB inakupa option nyingi na inakuwa kitabu kabisa tofauti na hizi pdf . EPUB ni kitabu halisi ingawa inahitaji application nzuri kuweza kuifungua. Kwa wanaotumia iPhone ipo app ya books by default , Kwa android unaweza ingia play store.
Ni browser am?
 
Mkuu kama ww umesoma vitabu huku hata kuandika kiswahili huwezi ni bora usiendelee kusoma!dhamini hapo imetumikaje?mbona sioni uhalali wa dhamini hapo!!
Mkuu, hata mimi nilihisi kuna makosa mengi sana, ila sikuwa na uhakika hasa ikizingatiwa kuwa mimi si mtaalam wa lugha. Almanusura hata niahirishe kupost humu jukwaani kwa kuhofia kuwa ujumbe niliotaka kuwasilisha usingeeleweka. Lakini nilipokumbuka kwamba anayetaka kuwa bora hapaswi kuogopa kukosea, nilijipiga moyo konde na kupost kama nilivyofanya.

Labda mkuu, unaweza ukanielekeza namna ambavyo nilipaswa kuandika?

Nashukuru kwa usaidizi wako.
 
Ni browser am?

EPUB ni format tu Kama unavyoona word pdf n.k

 
Kwa mnaosoma vitabu nashauri soft copy ziwe mfumo wa epub na si pdf . EPUB inakupa option nyingi na inakuwa kitabu kabisa tofauti na hizi pdf . EPUB ni kitabu halisi ingawa inahitaji application nzuri kuweza kuifungua. Kwa wanaotumia iPhone ipo app ya books by default , Kwa android unaweza ingia play store.
🙏🙏🙏 Shukran mkuu. Nimeshaipata.
 
Ndiyo, kama ni story nzuri za kujenga. Lakini Mimi binafsi, kwa upande wangu, non fiction vinaweza vikawa ni vizuri zaidi.

Vitabu siyo chakula cha ubongo bali akili. Mimi siyo mtaalam wa Saikolojia lakini nafahamu kuwa ubongo siyo akili na akili siyo ubongo.

Ubongo ni kama hardware na akili ni software.

Unaposoma, yale maneno yanayoingia kwenye akili yako huweza kuathiri na utendaji kazi wa ubongo wako.

Ndiyo, maneno huweza hata kumwua mtu, ikiwa hayo maneno yataielekeza akili kufanya hivyo. Akili itakachofanya ni kuiamuru ubongo kusitisha utendaji kazi wake, na ubongo ukiacha kufanya kazi matokeo yake yanafahamika, kifo.

Lakini yakiwa chanya, yanaweza kumletea mtu manufaa makubwa sana.

Ndiyo maana ni muhimu sana kuwa makini na unachokidoma. Kitakubadilisha bila wewe kujua, sana sana ni watu wanaokufahamu ndiyo watakaobaini mabadiliko yako.

I tell you the truth, vitabu vinaweza kuathiri hata mwonekano wako wa nje. I know what I am talking about. Sijasimuliwa. Nimeiona kwa macho yangu.

Maneno humjengea mtu taswira fulani akilini mwake, na hiyo taswira hutawala matendo yake.

Maneno yanayoingia kwa wingi kwenye ufahamu wako hatimaye yatatafuta jinsi ya kujithihirisha kwa vitendo.
Ili usome vitabu na uelewe unapaswa usiwe na stress.
Ili ufanye mazoezi unapaswa usiwe na stress
Ili ule na ushibe unapaswa usiwe na stress
Ili unywe na ufurahi unapaswa usiwe na stress
Unadaiwa ada za watoto, pesa ya kujikimu huo muda wa kuupa ubongo chakula unapata wapiii?
 
Ili usome vitabu na uelewe unapaswa usiwe na stress.
Ili ufanye mazoezi unapaswa usiwe na stress
Ili ule na ushibe unapaswa usiwe na stress
Ili unywe na ufurahi unapaswa usiwe na stress
Unadaiwa ada za watoto, pesa ya kujikimu huo muda wa kuupa ubongo chakula unapata wapiii?
Ukiwa na stress ni sahihi kufa njaa?

Kama hata mtu akiwa na stress bado anahitajika kula, ndivyo ilivyo pia na usomaji.

Ukiwa na stress, unaweza usiwe na muda wa kula na kunywa kwa anasa, lakini lazima kula chakula na kunywa maji kwa ajili ya kuendelea kuishi.

Ndivyo ilivyo na vitabu. Ni sehemu ya maisha ya akili yako. Isitoshe, stress inaweza kuchangiwa na upungufu wa lishe sahihi kichwani.

Kusoma Vitabu sahihi kutakusaidia ama kuepuka stress, kuishinda, au kuimanage.
 
Ili usome vitabu na uelewe unapaswa usiwe na stress.
Stress inachangiwa na aina ya taarifa uliyoilisha ufahamu wako. Kwa kusoma vitabu sahihi, unaulisha ufahamu wako taarifa chanya chanya. Taarifa chanya zinapokuwa nyingi akilini mwako huzifisha taarifa hasi zisababishavyo stress.
 
Ukiwa na stress ni sahihi kufa njaa?

Kama hata mtu akiwa na stress bado anahitajika kula, ndivyo ilivyo pia na usomaji.

Ukiwa na stress, unaweza usiwe na muda wa kula na kunywa kwa anasa, lakini lazima kula chakula na kunywa maji kwa ajili ya kuendelea kuishi.

Ndivyo ilivyo na vitabu. Ni sehemu ya maisha ya akili yako. Isitoshe, stress inaweza kuchangiwa na upungufu wa lishe sahihi kichwani.

Kusoma Vitabu sahihi kutakusaidia ama kuepuka stress, kuishinda, au kuimanage.
Embu tuwe realistic. Huna hata pesa y nauli ya daladala kitabu cha 50000 utanunua ukianzia wapi?
 
Ili ule na ushibe unapaswa usiwe na stress
Ili unywe na ufurahi unapaswa usiwe na stress
Usipokula kwa sababu ya stress utakufa. Stress ikikufanya ushindwe kusoma Vitabu vizuri, itakufanya "udumae" kiakili na kuendelea kuendelea kutawaliwa na stress.
 
Back
Top Bottom