Hao CCM siyo wazanzibar?
Wewe pia unaonekana ni mvivu wa kusoma au wa kutafuta habari. umekurupuka ulipotoka kwasababu tu hukupendezwa na ukweli mchungu alioambiwa Yerricko Nyerere. Ungepata nafasi ya kusoma kitabu cha KWAHERI UKOLONI KWAHERI UHURU kilichoandikwa na Dr.Harith Ghassany ungeelewa vizuri alichokua anamaanisha Mohammed Said kwasababu ndo rejea aliyoifanya kuhusu uandishi makini wa historia, sasa sijui unataka akusanye kitu gani tena au aandike nini. Hivyo hivyo, ukisoma hata kitabu alichokiandika yeye mwenyewe cha MAISHA NA NYAKATI ZA ABDULWAHID SYKES utaona utafiti wa kina uliofanyika katika uandishi wa kitabu hicho. Kwahiyo,anachojaribu kutuelewesha Sheikh Mohammed, kwamba unapoandika kitabu (hasa vinavyohusu historia siyo riwaya) ni lazima ufanye utafiti tena ikiwezekana kufanya mahojiano na wahusika wenyewe waliokuapo kwa wakati huo ili kupata uhalisia wa mambo na hicho ndicho alichofanya Dr.Ghassany. Sasa Yerricko anavyoandika upupu wake anakua amemhoji nani au amefanya utafiti gani? hivyo ni haki kabisa mtu mwingine kusema anafanya ' Plagiarism'.Pamoja na ukweli wa hoja zako lkn unaonekana ww ni mbinafsi,mchoyo na mwenye wivu wa dhahiri...na unanisononesha zaidi kwa kua umri umeshakwenda,laiti ungelikua kijana ningesema maneno mabaya zaidi.
Mara nyingi unapoteza nguvu nyingi kubishana na kazi za Yericko kwa nukta nukta za ukweli unaoujua.
Ombi langu kwako kusanya kila unachokijua halafu tuandikie kitabu ukisambaze na tukisome kama alivyofanya Yericko kuliko hili povu lako la kila mara.
Mm binafsi nimesoma historia ya mapinduzi ya Zanzibar ktk vitabu vitatu tofauti na vyote vina vitu vinakinzana na kingine..Lkn pia nimesoma historia ya Zanzibar kupitia makala za Joseph Mihangwa ktk gazeti la RAI .Na kwa kutumia akili yangu nimekubaliana na aliyoandika Mihangwa kwa 65% zaidi ya kwenye vitabu nilivyosoma.
Sasa baba ANDIKA ..ANDIKA baba tusome.
HUU UNAFIKI WA KUJUA VITU HALAFU UNAA NAVYO MPAKA UFE NAVYO UTATUSAIDIA NINI SISI WA KIZAZI HIKI.
BILA YERICKO KUANDIKA UNGELIBISHANIA WAPI.
Kwanza nakushukuru kwa kujibu kwa ADABU tofauti na maandishi yaliyomo kwenye uzi wako namba moja...Yericko,
Haitapendeza kwangu mimi nishindane na wewe kuhusu kitabu chako.
Uungwana unanikataza.
Kitabu kipo na kama mimi nitafanya, ''critique,'' yoyote basi iwe ya kisomi
isiwe kuishambulia kazi yako.
Kama kweli ''umechimba,'' historia ya mapinduzi hilo ni jambo jema na
wa kulisemea hilo si mimi na wewe bali ni wasomaji wa kitabu chako na
watakaokufanyia ''book review.''
Nasubiri kusoma ''reviews,'' za kitabu kama ninavyongoja kuona na kusoma
habari mpya za mapinduzi ambazo unasema Dr. Ghassany hakuziona katika
utafiti wake.
Ghassany alikuja na Mohamed Omari Mkwawa na Victor Mkello na kina
Lumumba, Aboud Mmasai na hawa wote picha zao na sauti zao zipo katika
Maktaba kwa ajili ya rejea kwa watafiti wengine siku za usoni.
Ghassany kaja na Kipumbwi, kambi ya askari mamluki waliovushwa kuingia
Zanzibar kusaidia mapinduzi.
Habari hii ya Wamakonde kutoka mashamba ya mkonge ya Sakura ambayo
haikufahamika toka mwaka wa 1964 ikaja kusomwa mwaka wa 2010 katika
kitabu cha Dr. Ghassany baada ya miaka 46 kupita.
Vumbi la habari hizi kila msomaji wa kitabu kile analijua.
Ikiwa wewe kitabu chako kina mambo zaidi ya hayo utakuwa umefanya kazi
kubwa sana ya kupigiwa mfano na itasaidia sana kukitangaza kitabu chako
kama utaeleza haya yakafahamika.
Nakushauri usiache kuonyesha na kueleza mambo kama haya ili wasomaji
wavuitiwe na ukweli uliokujanao katika kitabu chako hiki.
Itakuwa vizuri sana kama hawa wasomi wanaopendekeza utunukiwe shahada
kwanza kabla ya hayo wao kwa usomi wao ungewaomba waandike ''review,''
ya kitabu chako ili wasomaji wajue nini umeeleza katika kazi hii yako.
Nionavyo mie si busara mathalan kwa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam au chuo
chochote kile kuanza kukupa shahada kabla ya kuonyesha kwanza uzito wa kazi
yako au hata kabla kitabu hakijaandikiwa, ''reviews'' na kuchapwa katika majarida
kama Cambridge Journal of African History.
Kweli unastahili sifa kubwa sana kuwa kitabu ni cha Kiswahili lakini kinasomwa
dunia nzima na watu ambao hawajui Kiswahili.
Unastahili sifa sana kwani hiki ulichofanikiwa wewe si kitu kidogo.
Nakueleza haya kutoka moyoni kwangu kwani mimi kama mtu wa vitabu naujua
vizuri ugumu uliopo katika biashara ya vitabu hasa kitabu kilichoandikwa na
mwandishi ambae hajawahi kuandika kitabu.
Umenishauri niandike kitabu nipinge kitabu chako.
Sidhani kama hili ni jambo la busara kwani huwezi kuandika kitabu juu ya kitabu.
Hakuna ''publisher,'' atakaegusa mswada kama huo kwa kuwa somo nimeshaliandika
na kitabu kipo.
Kitabu chako wewe kimekuja nyuma ya kitabu changu kwa takriban miaka 20.
Ninachoweza kufanya ni mimi kufanya ''book review,'' ya kitabu chako.
Hili ndilo muhimu na nitakuwa khasa mtu ninaestahili kufanya "review" kwa kuwa
hili somo la mapinduzi na uhuru wa Tanganyika nalijua vyema.
Hivi ndiyo baadhi ya vitu mwandishi anatakiwa awe anavijua kuepuka makosa ambayo
si ya lazima.
Umenishambulia kwa kuniita mvivu na mtu mwenye wivu.
Sidhani kama hizo sifa zinanienea mimi.
Ama hili la ''porojo,'' waliokuwa katika haya mambo ya utafiti na uandishi na baadhi ya
vyuo vikuu na taasisi nyingine za elimu ambao tumefanyakazi pamoja aidha kwa kuhariri
au kuandika au nilkopita na kufanya mihadhara kwenye vyuo vyao nadhani wananijua
kuwa mimi si mvivu wala si mpiga porojo.
Lakini akutukanae hakuchagulii tusi.
Inawezekana nina kasoro kama ilivyo kawaida ya binadamu yoyote, kakini hii sifa ya uvivu
si sifa yangu.
Napenda kuhitimisha kuwa kusema kuwa umeifanyia nchi yetu hisani kubwa kwa kuandika
historia ya TANU na mchango wa Jesuits katika historia hiyo.
Sasa tuna historia tatu za TANU.
Historia ya Chuo Cha Kivukoni, historia hiyo yako ya Jesuits na historia mnayoijua ya TANU
na uhuru wa Tanganyika niliyoandika
kama nilivyopokea kutoka kwa wazee wangu.
Na ni yapi maoni yako juu ya huyo anaelalamikiwa?Pamoja na ukweli wa hoja zako lkn unaonekana ww ni mbinafsi,mchoyo na mwenye wivu wa dhahiri...na unanisononesha zaidi kwa kua umri umeshakwenda,laiti ungelikua kijana ningesema maneno mabaya zaidi.
Mara nyingi unapoteza nguvu nyingi kubishana na kazi za Yericko kwa nukta nukta za ukweli unaoujua.
Ombi langu kwako kusanya kila unachokijua halafu tuandikie kitabu ukisambaze na tukisome kama alivyofanya Yericko kuliko hili povu lako la kila mara.
Mm binafsi nimesoma historia ya mapinduzi ya Zanzibar ktk vitabu vitatu tofauti na vyote vina vitu vinakinzana na kingine..Lkn pia nimesoma historia ya Zanzibar kupitia makala za Joseph Mihangwa ktk gazeti la RAI .Na kwa kutumia akili yangu nimekubaliana na aliyoandika Mihangwa kwa 65% zaidi ya kwenye vitabu nilivyosoma.
Sasa baba ANDIKA ..ANDIKA baba tusome.
HUU UNAFIKI WA KUJUA VITU HALAFU UNAA NAVYO MPAKA UFE NAVYO UTATUSAIDIA NINI SISI WA KIZAZI HIKI.
BILA YERICKO KUANDIKA UNGELIBISHANIA WAPI.
Amemgusa "anaependwa" na haooooo ndo mana itambidi avumilie "mawe"Mzee wangu kwa jinsi baadhi ya watu humu wasivyokupenda itabidi uwe mvumilivu kweli kwa hili uliloandika.
Hakika wewe ni MAHIRI katika UANDISHI .. Big up .. but nimevutika na title moja isemayo .... "THE MERMAIDS OF MSAMBWENI AND OTHER STORIES" .... hapoooooo penye MERMAIDS hapo ... yaani kila siku iitwapo leo niko CURIOUS kufahamu juu ya hao VIUMBE ... are they REAL or just IMAGINARY creatures ...?Ridhwani,
Umerudi mtu mwingine kabisa.
Nimefurahi.
Unaandika katika lugha ya kistaarabu na kwa adabu.
Ahsante sana.
Nakuwekea baadhi ya niliyoandika:
Ridhwani,
- PUBLICATIONS/RESEARCH PAPERS/ARTICLES
- The Life and Times of Abdulwahid Sykes 1924 –1968 The Untold Story of the Muslim Struggle against British Colonialism in Tanganyika, Minerva Press London, 1998 translated into Kiswahili as Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes 1924-1968 Historia Iliyofichwa Kuhusu Harakati za Waislam Dhidi ya Ukoloni wa Waingereza, Phoenix Publishers, Nairobi, 2002.
- The Torch on Kilimanjaro, Oxford University Press, Nairobi, 2006
- Contributing author for an African anthology: The Mermaid of Msambweni and Other Stories, Oxford University Press 2007, Nairobi.
- Contributing author Dictionary of African Biography (DAB), Oxford University Press 2011, New York.
- Uchaguzi wa Busara, Abantu Publications 2008, Dar es Salaam.
- In Praise of Ancestors (1987) Africa Events (London).
- Abdulwahid Sykes: Founder of Political Movement (1988) Africa Events (London).
- Islam and Politics in Tanzania (1989) Al Haq International (Karachi)
- The Plight of Tanzanian Muslim (1993) Change (Dar es Salaam).
- Tanzania - The "Secular" Unsecular State (1995) Change (Dar es Salaam).
- The Question of Muslim Stagnation in Education in Tanzania - A Muslim Riddle (Paper presented at the Conference of the Global World of the Swahili Intercultural Dialogue on the Indian Ocean Zanzibar, February 20 - 23, 2003).
- Islamic Education and Intellectualism in Eastern Africa ‘Themes from the Pulpit in Tanganyika (Tanzania Mainland) 1800 – 2000’ (Paper presented at International Symposium on Islamic Civilisation in Eastern Africa Kampala, Uganda organised by the Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA), Istanbul and the Islamic University in Uganda, Mbale December 15th – 17th 2003).
- Sheikh Hassan bin Ameir - The Moving Spirit of Muslim Emancipation in Tanganyika (1950 – 1968) (Paper presented at Youth Camp Organised by Zanzibar University, World Assembly of Muslim Youth (WAMY) and Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) 27th February – 4th March 2004).
- Islamic Movement and the Christian Lobby in Tanzania - the Experience of the late Prof. Kighoma Ali Malima (1938 – 1995) (Paper Presented to Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) Sokoine University of Agriculture (SUA) Morogoro 11th April 2004).
- Terrorism in East Africa the Tanzanian Experience (Paper Presented at the Conference on Islam, Terrorism and African Development University of Ibadan, Nigeria 8th - 10th February 2006).
- Al Marhum Sheikh Kassim bin Juma bin Khamis (1940 – 1994) and the Pork Riots of 1993. (Paper Presented at the Regional Conference on Islam in Eastern Africa: Islam Encounter with the Challenges of the 21st Century 1st - 3rd August 2006, Kenyatta University, Nairobi.
- 14. Muslim Bible Scholars of Tanzania – The Legacy of Sheikh Ahmed Deedat (1918 – 2005) Paper Presented at the International Symposium on Islamic Civilisation in Southern Africa Organised by The Organisation of Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA) The National AWQAF Foundation of South Africa (AWQAF SA 1 – 3 September 2006 University of Johannesburg.
- Tanzania: A Nation Without Heroes Seminar Organised by IFRA French Institute for Research in Africa and BIEA British Institute in East Africa 23rd and 24th September 2013 at IFRA Nairobi.
Mimi ni mhariri, mfasiri na pia ni ''publisher.''
Kusoma na kuandika ndiyo maisha yangu.
Nimejifunza kusoma labda nina miaka sita na bado sijakwenda shule.
Nakueleza haya ili tuelewane na tuende vyema.
yericko nyerere sijui unakumbuka ulikuja kuniuzia hicho kitabu ilala amana ofisini kwangu na nikampigia mzee Mohamed Said ukaongee nae nia yngu kubwa nilikuwa nataka uende kuongeza elimu hakika unaitaji kuivishwa zaidi na magwiji km mzee Mohamed Said sio kukalia ubishi km ndugu zetu wa lumumba jaribu kumsoma vizuri mzee wetu utamuelewa nia yke kujaribu kutaka kkujenga zaidi kijana wake lkn naona unataka kuleta ushindani sio na sababu hakika ww ni Kichochi uwezi kuingia kwenye kundi la ninga jaribu kkubari kukoselewa...
Unataka ushahidi wa kipi ikiwa kitabu hujakisoma?
Nimekufafanulia hapo kwamba marejeo yote yamewekwa wazi, au hujui maana ya marejeo?
Msamehe huyo mzee ni rafiki yangu yupo Buguruni Malapa ni mfuasi mtiifu wa Mohamed Said....nimemsoma rubawa anaonekana kuwa ni mfuasi mtiifu wa said mohamed kiasi kwamba kwa yeye haoni hata sababu ya kutafakari yale yanayosemwa na ustaadhi mzee wetu said mohamed. kitu ambacho naona ni kibaya sana kwa ustawi wa akili. yeye anachosisitiza ni kuwa fuata kile kinachosemwa na mzee said naye atafurahishwa nawe.