Asiyoyajua Yericko Nyerere katika utafiti wa historia ya Mapinduzi ya Zanzibar

Asiyoyajua Yericko Nyerere katika utafiti wa historia ya Mapinduzi ya Zanzibar

Hao CCM siyo wazanzibar?


Ccm si wazanzibari. Ni mabolozi wa Tanganyika ndani ya Zanzibar. Hawana uwezo hata wakushinda majimbo ma 10 bila ya nguvu ya dola. Na maeneo yenye nguvu ya CCm nimeonea ya wahamiaji kutoka bara.
Hebu zitizame izo sherehe uwanjani kuna wananchi waliohudhuria? majukwaani mumejazwa JKU na KVZ. Watumishi wa serekali na wanafunzi wa skuli za serekali hulizimishwa kwa nguvu kuhudhuria. Mapambo ya sherehe utayakuta kwenye maskani za CCm na ofisi za serekali tu. Bado Picha hupati. Nenda mwenyewe ukajionee alafu ndo uzungumze.
 
Pamoja na ukweli wa hoja zako lkn unaonekana ww ni mbinafsi,mchoyo na mwenye wivu wa dhahiri...na unanisononesha zaidi kwa kua umri umeshakwenda,laiti ungelikua kijana ningesema maneno mabaya zaidi.

Mara nyingi unapoteza nguvu nyingi kubishana na kazi za Yericko kwa nukta nukta za ukweli unaoujua.
Ombi langu kwako kusanya kila unachokijua halafu tuandikie kitabu ukisambaze na tukisome kama alivyofanya Yericko kuliko hili povu lako la kila mara.

Mm binafsi nimesoma historia ya mapinduzi ya Zanzibar ktk vitabu vitatu tofauti na vyote vina vitu vinakinzana na kingine..Lkn pia nimesoma historia ya Zanzibar kupitia makala za Joseph Mihangwa ktk gazeti la RAI .Na kwa kutumia akili yangu nimekubaliana na aliyoandika Mihangwa kwa 65% zaidi ya kwenye vitabu nilivyosoma.

Sasa baba ANDIKA ..ANDIKA baba tusome.

HUU UNAFIKI WA KUJUA VITU HALAFU UNAA NAVYO MPAKA UFE NAVYO UTATUSAIDIA NINI SISI WA KIZAZI HIKI.
BILA YERICKO KUANDIKA UNGELIBISHANIA WAPI.
Wewe pia unaonekana ni mvivu wa kusoma au wa kutafuta habari. umekurupuka ulipotoka kwasababu tu hukupendezwa na ukweli mchungu alioambiwa Yerricko Nyerere. Ungepata nafasi ya kusoma kitabu cha KWAHERI UKOLONI KWAHERI UHURU kilichoandikwa na Dr.Harith Ghassany ungeelewa vizuri alichokua anamaanisha Mohammed Said kwasababu ndo rejea aliyoifanya kuhusu uandishi makini wa historia, sasa sijui unataka akusanye kitu gani tena au aandike nini. Hivyo hivyo, ukisoma hata kitabu alichokiandika yeye mwenyewe cha MAISHA NA NYAKATI ZA ABDULWAHID SYKES utaona utafiti wa kina uliofanyika katika uandishi wa kitabu hicho. Kwahiyo,anachojaribu kutuelewesha Sheikh Mohammed, kwamba unapoandika kitabu (hasa vinavyohusu historia siyo riwaya) ni lazima ufanye utafiti tena ikiwezekana kufanya mahojiano na wahusika wenyewe waliokuapo kwa wakati huo ili kupata uhalisia wa mambo na hicho ndicho alichofanya Dr.Ghassany. Sasa Yerricko anavyoandika upupu wake anakua amemhoji nani au amefanya utafiti gani? hivyo ni haki kabisa mtu mwingine kusema anafanya ' Plagiarism'.
 
Yericko,
Haitapendeza kwangu mimi nishindane na wewe kuhusu kitabu chako.
Uungwana unanikataza.

Kitabu kipo na kama mimi nitafanya, ''critique,'' yoyote basi iwe ya kisomi
isiwe kuishambulia kazi yako.

Kama kweli ''umechimba,'' historia ya mapinduzi hilo ni jambo jema na
wa kulisemea hilo si mimi na wewe bali ni wasomaji wa kitabu chako na
watakaokufanyia ''book review.''

Nasubiri kusoma ''reviews,'' za kitabu kama ninavyongoja kuona na kusoma
habari mpya za mapinduzi ambazo unasema Dr. Ghassany hakuziona katika
utafiti wake.

Ghassany alikuja na Mohamed Omari Mkwawa na Victor Mkello na kina
Lumumba, Aboud Mmasai na hawa wote picha zao na sauti zao zipo katika
Maktaba kwa ajili ya rejea kwa watafiti wengine siku za usoni.

Ghassany kaja na Kipumbwi, kambi ya askari mamluki waliovushwa kuingia
Zanzibar kusaidia mapinduzi.

Habari hii ya Wamakonde kutoka mashamba ya mkonge ya Sakura ambayo
haikufahamika toka mwaka wa 1964 ikaja kusomwa mwaka wa 2010 katika
kitabu cha Dr. Ghassany baada ya miaka 46 kupita.

Vumbi la habari hizi kila msomaji wa kitabu kile analijua.

Ikiwa wewe kitabu chako kina mambo zaidi ya hayo utakuwa umefanya kazi
kubwa sana ya kupigiwa mfano na itasaidia sana kukitangaza kitabu chako
kama utaeleza haya yakafahamika.

Nakushauri usiache kuonyesha na kueleza mambo kama haya ili wasomaji
wavuitiwe na ukweli uliokujanao katika kitabu chako hiki.

Itakuwa vizuri sana kama hawa wasomi wanaopendekeza utunukiwe shahada
kwanza kabla ya hayo wao kwa usomi wao ungewaomba waandike ''review,''
ya kitabu chako ili wasomaji wajue nini umeeleza katika kazi hii yako.

Nionavyo mie si busara mathalan kwa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam au chuo
chochote kile kuanza kukupa shahada kabla ya kuonyesha kwanza uzito wa kazi
yako au hata kabla kitabu hakijaandikiwa, ''reviews'' na kuchapwa katika majarida
kama Cambridge Journal of African History.

Kweli unastahili sifa kubwa sana kuwa kitabu ni cha Kiswahili lakini kinasomwa
dunia nzima na watu ambao hawajui Kiswahili.

Unastahili sifa sana kwani hiki ulichofanikiwa wewe si kitu kidogo.

Nakueleza haya kutoka moyoni kwangu kwani mimi kama mtu wa vitabu naujua
vizuri ugumu uliopo katika biashara ya vitabu hasa kitabu kilichoandikwa na
mwandishi ambae hajawahi kuandika kitabu.

Umenishauri niandike kitabu nipinge kitabu chako.
Sidhani kama hili ni jambo la busara kwani huwezi kuandika kitabu juu ya kitabu.

Hakuna ''publisher,'' atakaegusa mswada kama huo kwa kuwa somo nimeshaliandika
na kitabu kipo.

Kitabu chako wewe kimekuja nyuma ya kitabu changu kwa takriban miaka 20.

Ninachoweza kufanya ni mimi kufanya ''book review,'' ya kitabu chako.

Hili ndilo muhimu na nitakuwa khasa mtu ninaestahili kufanya "review" kwa kuwa
hili somo la mapinduzi na uhuru wa Tanganyika nalijua vyema.

Hivi ndiyo baadhi ya vitu mwandishi anatakiwa awe anavijua kuepuka makosa ambayo
si ya lazima.

Umenishambulia kwa kuniita mvivu na mtu mwenye wivu.
Sidhani kama hizo sifa zinanienea mimi.

Ama hili la ''porojo,'' waliokuwa katika haya mambo ya utafiti na uandishi na baadhi ya
vyuo vikuu na taasisi nyingine za elimu ambao tumefanyakazi pamoja aidha kwa kuhariri
au kuandika au nilkopita na kufanya mihadhara kwenye vyuo vyao nadhani wananijua
kuwa mimi si mvivu wala si mpiga porojo.

Lakini akutukanae hakuchagulii tusi.

Inawezekana nina kasoro kama ilivyo kawaida ya binadamu yoyote, kakini hii sifa ya uvivu
si sifa yangu.

Napenda kuhitimisha kuwa kusema kuwa umeifanyia nchi yetu hisani kubwa kwa kuandika
historia ya TANU na mchango wa Jesuits katika historia hiyo.

Sasa tuna historia tatu za TANU.

Historia ya Chuo Cha Kivukoni, historia hiyo yako ya Jesuits na historia mnayoijua ya TANU
na uhuru wa Tanganyika niliyoandika
kama nilivyopokea kutoka kwa wazee wangu.
Kwanza nakushukuru kwa kujibu kwa ADABU tofauti na maandishi yaliyomo kwenye uzi wako namba moja...

Umeonesha kujutia vizuri kile ulichokiandika awali, huu ni uungwana mkubwa...


Lakini nikusihi tena na tena, kitabu changu kina rejea (reference's) zote, na zaidi nyaraka muhimu zote...

Ninaamini kabisa kitabu changu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi wewe mzee hujakiona hata kwa macho ya karibu tu, achilia mbalikukisoma.. Maana ungekuwa umesoma bila shaka kila rejea ungeona... Kwa kukusaidia tu rejea zote zipo mwishoni mwa kitabu achilia mbali zilizowekwa ndani ya maandishi.......

Screenshot_20180117-104639.png
Screenshot_20180117-104700.png
 
Yericko,
Vizuri ujifunze lugha za kistaarabu.

Unaposema, "wewe mzee," ni tofauti na "mzee wangu."

Mfano wa kwanza ni kukosa adabu na wa pili ni staha ingawa maana ni moja.
 
Yericko,
Waamuzi wa hadhi ya kitabu kwanza huwa "reviewers," hawa ni wataalamu wa somo lililoandikiwa kitabu na hawa ndiyo huwafanya watu wakakisoma kitabu.

Kama ipo "review," yoyote tuwekee hapa tuwasikie nini maoni yao kuhusu kitabu chako.
 
Nilimwambia yeriko hakuna cha maana alichoandika ila ukiandika wewe wanasema ni muongo,mdini,mkabila ila wao ni kukopi tu ndo wanachoweza
 
Pamoja na ukweli wa hoja zako lkn unaonekana ww ni mbinafsi,mchoyo na mwenye wivu wa dhahiri...na unanisononesha zaidi kwa kua umri umeshakwenda,laiti ungelikua kijana ningesema maneno mabaya zaidi.

Mara nyingi unapoteza nguvu nyingi kubishana na kazi za Yericko kwa nukta nukta za ukweli unaoujua.
Ombi langu kwako kusanya kila unachokijua halafu tuandikie kitabu ukisambaze na tukisome kama alivyofanya Yericko kuliko hili povu lako la kila mara.

Mm binafsi nimesoma historia ya mapinduzi ya Zanzibar ktk vitabu vitatu tofauti na vyote vina vitu vinakinzana na kingine..Lkn pia nimesoma historia ya Zanzibar kupitia makala za Joseph Mihangwa ktk gazeti la RAI .Na kwa kutumia akili yangu nimekubaliana na aliyoandika Mihangwa kwa 65% zaidi ya kwenye vitabu nilivyosoma.

Sasa baba ANDIKA ..ANDIKA baba tusome.

HUU UNAFIKI WA KUJUA VITU HALAFU UNAA NAVYO MPAKA UFE NAVYO UTATUSAIDIA NINI SISI WA KIZAZI HIKI.
BILA YERICKO KUANDIKA UNGELIBISHANIA WAPI.
Na ni yapi maoni yako juu ya huyo anaelalamikiwa?
 
BB,
Nina uzoefu mkubwa katika haya.
Naingia Maktaba In Shaa Allah nitakuwekea hapa stori ina zaidi ya miaka 30.
 
BB
Ofisi za Africa Events Banner Street, London alikuwapo Mohamed Mlamali Adam, Ahmed Saleh Yahya, Ahmed Rajab na Mlamali Adam. Alikuwapo na Abdullatif Abdallah huyu kutoka Mombasa. Waliobakia wote Wazanzibari. Hili gazeti lilifanya makubwa na Babu akiandika sana mle. Ikafikia serikali ikawa inalipiga vita chini chini kwa BoT kukataa kuwapa fedha za mauzo ya gazeti hadi yalipofanyika makubaliano maalum nayo ni kumtoa Mlamali kama Mhariri mkuu na kuzuia makala za Mohamed Said. Haya yalifanyika lakini baada ya miaka 3 Ahmed Saleh Yahya akanipa assignment juu ya Rais Mwinyi lakini by line jina langu halikuwekwa nikawa sasa ni Special Correspondent na malipo yakawa ki James Bond napigiwa simu nakutana na mtu ananikabidhi bahasha. Lakini tulimsaidia Mzee Mwinyi na yeye akaeleweka shida anazokutananazo kama Rais kutokea Zanzibar...
 
Ridhwani,
Umerudi mtu mwingine kabisa.
Nimefurahi.

Unaandika katika lugha ya kistaarabu na kwa adabu.
Ahsante sana.

Nakuwekea baadhi ya niliyoandika:
  1. PUBLICATIONS/RESEARCH PAPERS/ARTICLES
  2. The Life and Times of Abdulwahid Sykes 1924 –1968 The Untold Story of the Muslim Struggle against British Colonialism in Tanganyika, Minerva Press London, 1998 translated into Kiswahili as Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes 1924-1968 Historia Iliyofichwa Kuhusu Harakati za Waislam Dhidi ya Ukoloni wa Waingereza, Phoenix Publishers, Nairobi, 2002.
  3. The Torch on Kilimanjaro, Oxford University Press, Nairobi, 2006
  4. Contributing author for an African anthology: The Mermaid of Msambweni and Other Stories, Oxford University Press 2007, Nairobi.
  5. Contributing author Dictionary of African Biography (DAB), Oxford University Press 2011, New York.
  6. Uchaguzi wa Busara, Abantu Publications 2008, Dar es Salaam.
  7. In Praise of Ancestors (1987) Africa Events (London).
  8. Abdulwahid Sykes: Founder of Political Movement (1988) Africa Events (London).
  9. Islam and Politics in Tanzania (1989) Al Haq International (Karachi)
  10. The Plight of Tanzanian Muslim (1993) Change (Dar es Salaam).
  11. Tanzania - The "Secular" Unsecular State (1995) Change (Dar es Salaam).
  12. The Question of Muslim Stagnation in Education in Tanzania - A Muslim Riddle (Paper presented at the Conference of the Global World of the Swahili Intercultural Dialogue on the Indian Ocean Zanzibar, February 20 - 23, 2003).
  13. Islamic Education and Intellectualism in Eastern Africa ‘Themes from the Pulpit in Tanganyika (Tanzania Mainland) 1800 – 2000’ (Paper presented at International Symposium on Islamic Civilisation in Eastern Africa Kampala, Uganda organised by the Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA), Istanbul and the Islamic University in Uganda, Mbale December 15th – 17th 2003).
  14. Sheikh Hassan bin Ameir - The Moving Spirit of Muslim Emancipation in Tanganyika (1950 – 1968) (Paper presented at Youth Camp Organised by Zanzibar University, World Assembly of Muslim Youth (WAMY) and Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) 27th February – 4th March 2004).
  15. Islamic Movement and the Christian Lobby in Tanzania - the Experience of the late Prof. Kighoma Ali Malima (1938 – 1995) (Paper Presented to Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) Sokoine University of Agriculture (SUA) Morogoro 11th April 2004).
  16. Terrorism in East Africa the Tanzanian Experience (Paper Presented at the Conference on Islam, Terrorism and African Development University of Ibadan, Nigeria 8th - 10th February 2006).
  17. Al Marhum Sheikh Kassim bin Juma bin Khamis (1940 – 1994) and the Pork Riots of 1993. (Paper Presented at the Regional Conference on Islam in Eastern Africa: Islam Encounter with the Challenges of the 21st Century 1st - 3rd August 2006, Kenyatta University, Nairobi.
  18. 14. Muslim Bible Scholars of Tanzania – The Legacy of Sheikh Ahmed Deedat (1918 – 2005) Paper Presented at the International Symposium on Islamic Civilisation in Southern Africa Organised by The Organisation of Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA) The National AWQAF Foundation of South Africa (AWQAF SA 1 – 3 September 2006 University of Johannesburg.
  19. Tanzania: A Nation Without Heroes Seminar Organised by IFRA French Institute for Research in Africa and BIEA British Institute in East Africa 23rd and 24th September 2013 at IFRA Nairobi.
Ridhwani,
Mimi ni mhariri, mfasiri na pia ni ''publisher.''
Kusoma na kuandika ndiyo maisha yangu.

Nimejifunza kusoma labda nina miaka sita na bado sijakwenda shule.
Nakueleza haya ili tuelewane na tuende vyema.
Hakika wewe ni MAHIRI katika UANDISHI .. Big up .. but nimevutika na title moja isemayo .... "THE MERMAIDS OF MSAMBWENI AND OTHER STORIES" .... hapoooooo penye MERMAIDS hapo ... yaani kila siku iitwapo leo niko CURIOUS kufahamu juu ya hao VIUMBE ... are they REAL or just IMAGINARY creatures ...?
 
BB,
Hiyo hapo juu ni stori ya 1988.

Chukua muda usome ujue tatizo la kuandika historia ya kweli katika nchi za Kiafrika.
 
kwa nini rubawa unaamini kuwa mzee said tu ndo anapaswa kumkosoa au kuwa ndo mwalimu wa yericko?unadhani umri ni kigezo cha kusema yeye yericko akubaliane na hata kile asichokiamini? si sawa. tukiamini hivi tutapelekana shimoni maana kipofu hawezi mwongoz akipofu mwenzie. simshauri yericko akubaliane na mzee said. namshauri apingane naye kwa hoja. hakuna mwenye hati miliki ya elimu au ufahamu.na hili halihusiani na dini wala mtizamo. nadhani ukaribu na imani uliyo nayo kwa mzee said kama unavyosema kuwa ulimpigia simu vinakufanya pengine utiwe upofu wa kufikiria kinyume na yeye...hivyo ukajikuta kila alisemalo wewe waitikia "hewalaah" au tawile. ashakum si matusi.sisi wazee wa siku hizi tunakataza sana ufuasi.
3c76fab69f297d7a1053e3c760e87c70.jpg
yericko nyerere sijui unakumbuka ulikuja kuniuzia hicho kitabu ilala amana ofisini kwangu na nikampigia mzee Mohamed Said ukaongee nae nia yngu kubwa nilikuwa nataka uende kuongeza elimu hakika unaitaji kuivishwa zaidi na magwiji km mzee Mohamed Said sio kukalia ubishi km ndugu zetu wa lumumba jaribu kumsoma vizuri mzee wetu utamuelewa nia yke kujaribu kutaka kkujenga zaidi kijana wake lkn naona unataka kuleta ushindani sio na sababu hakika ww ni Kichochi uwezi kuingia kwenye kundi la ninga jaribu kkubari kukoselewa...
 
nimemsoma rubawa anaonekana kuwa ni mfuasi mtiifu wa said mohamed kiasi kwamba kwa yeye haoni hata sababu ya kutafakari yale yanayosemwa na ustaadhi mzee wetu said mohamed. kitu ambacho naona ni kibaya sana kwa ustawi wa akili. yeye anachosisitiza ni kuwa fuata kile kinachosemwa na mzee said naye atafurahishwa nawe.

Unataka ushahidi wa kipi ikiwa kitabu hujakisoma?

Nimekufafanulia hapo kwamba marejeo yote yamewekwa wazi, au hujui maana ya marejeo?
 
nimemsoma rubawa anaonekana kuwa ni mfuasi mtiifu wa said mohamed kiasi kwamba kwa yeye haoni hata sababu ya kutafakari yale yanayosemwa na ustaadhi mzee wetu said mohamed. kitu ambacho naona ni kibaya sana kwa ustawi wa akili. yeye anachosisitiza ni kuwa fuata kile kinachosemwa na mzee said naye atafurahishwa nawe.
Msamehe huyo mzee ni rafiki yangu yupo Buguruni Malapa ni mfuasi mtiifu wa Mohamed Said....

Hawa wazee wote ni watu ninaowamudu vizuri, niliwahi kubishana nao hapa miaka miwili mfululizo usiku na mchana, wana chuki sumu ya koboko inasubiri...wadini hasaaaa
 
Back
Top Bottom