Askofu Emaus Mwamakula akamatwa na Polisi kwa kuhamasisha Maandamano ya kudai Katiba Mpya

Askofu Emaus Mwamakula akamatwa na Polisi kwa kuhamasisha Maandamano ya kudai Katiba Mpya

Kumbe huyu aanejiita askofu ni mpinzni wa kisiasa na alikuwa pia mshauri wa Lisu wakati wa kampeni?

Alafu mnalaumu kwanini mmeshindwa uchaguzi?

Imagine Mwamakula ndio mshauri wa mgombea urais katika harakati za kwenda ikulu katika nchi kama tz!

Yani huko chadema hakuna watu wenye akili kabisa?
 
Ule muujiza wa mtu mmoja aliouahidi Mungu kabla ya 2023 utatikisa nchi! Na baada ya huo, wengi watatoka mapangoni kudai katiba iandikwe upya. Hata hawa wanaomkamata Askofu leo mtawasikia!
 
Huyu Askofu ndiyo ali organize matembezi ya hiyari kudai Katiba mpya?

Nadhani angejikita kwenye kuchunga kondoo wa bwana tu, utawala uliopo huwa haupendi kufosiwa kufanya mambo. Mambo yanafanyika pale mwenye nyumba atakapoamua.

Hata kama aliwahaidi Katiba mpya -mpaka apende mwenyewe

Milioni 50 kila Kijiji - mpaka apende

Nyongeza ya mishahara - mpaka apende

You mention...
Atawachungia wapi hao kondoo na kanisa lilimfukuza?
Hana kanisa, kiufupi ni mkorofi kiasili, huwa hawezi kutulia
 
View attachment 1703071


View attachment 1703070



View attachment 1703379


====

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
KUKAMATWA KWA ASKOFU EMMAUS BANDEKILE MWAMAKULA
KWA KOSA LA KUHAMASISHA MAANDAMANO HARAMU

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Polisi Dar es Salaam leo tarehe 15.02.2021 limefanikiwa kumkamata anayejiita Askofu EMMAUS BANDEKILE MWAMAKULA wa kanisa la Uamsho la Moravian kwa kosa la kuhamasisha maandamano nchi nzima kwa njia ya ujumbe wa maneno katika mitandao ya kijamii. Taarifa ilikuwa ikihamasisha wananchi wajitokeze kwa wingi ili kuandamana wakishinikiza na kudai katiba mpya jambo ambalo ni kinyume na taratibu na sheria za nchi.

Aidha awali Jeshi la Polisi kupitia idara ya upelelezi kanda Maalum Dar es salaam walifanikiwa kupata taarifa hiyo na kumkamata Askofu huyo kwa ajili mahojiano kwa jambo hilo ambalo lilileta taharuki kwa umma katika mitandao ya kijamii.

Jeshi la Polisi linatoa onyo kwa yeyote ambaye ameshawishika na kupanga kuandamana kuahirisha mara moja nia hiyo ovu ambayo iko kinyume na sheria.

Pia ifahamike ni kosa kufanya maandamano bila kuwa na kibali cha Polisi ili kupewa ulinzi, na atakayejaribu kuandamana atashughulikiwa kwa mujibu wa sheria. Hivyo wananchi wote wa jiji la Dar es salaam waendelee na shughuli zao za kukuza uchumi na kujipatia vipato vyao vya kila siku.


LAZARO B. MAMBOSASA– SACP
KAMANDA WA POLISI KANDA MAALUM
DAR ES SALAM.
15.02.2021

Zaidi, soma:


Sikujua kama matembezi ya hiari ni kosa la kisheria.Kama ni kosa,chombo gani kinapaswa kusaidia kupatakatiba mpya?
 
Sasa kama amekamatwa si muandamane mwende mkamtowe.
Si mlimuahidi kwamba mko nae bega kwa bega.
Hapa ndo makamanda wa malalamiko hua siwaelewi. Mi nadhani wawe wanawaweka wazi hawa waanzisha maandamano kwamba tutakupa support ila ya mitandaoni tu, barabarani hatuingii. Huenda itawafanya hawa waanzisha maandamano watuluze vichwa
 
Tafadhari naombeni CV yake. Kazaliwa wapi, kasoma wapi na ana elimu kiasi gani. Naona mtandaoni siioni CV iliyoshiba ila atakuwa ana akili sio kama kina Askofu Rashid
Nacho f
Tafadhari naombeni CV yake. Kazaliwa wapi, kasoma wapi na ana elimu kiasi gani. Naona mtandaoni siioni CV iliyoshiba ila atakuwa ana akili sio kama kina Askofu Rashid
Nachofahamu Askofu Mwamakulah alisoma Azania High school. Na alikuwa mchapuo wa PCM.
Pia alikuwa ni Headboy. Inasemekana alikuwa na uwezo mkubwa darasani. Na alikuwa kiongozi mzuri alie heshimika kwa wanafunzi, walimu na hata Mkuu wa shule alimpenda sana. Wakati huo Mkuu wa shule alikuwa Bwana Kwayu.
Mwamakulah alifaulu vizuri kwa kiwango cha juu katika mtihani wa Taifa kidato cha Sita. Nasikia aliendelea na masomo ya chuo kikuu.
 
Watu wenye mawazo kama yako ndo wamefanya watanzania kuchezewa kama watoto wadogo nasi kukubali kufyata mkia! Kazi ya mchungaji ni pamoja na kulinda usalama wa kondoo wake! Watanzania wameuawa, wamepigwa, wamebambikiwa kesi za uongo, nasi tuko kimya tunaendelea kutoa macho tu na kuandika kama uliyoandika hapa!
Mkuu Watanzania nawajua, ni waoga kupitiliza. Kile kizazi cha akina Samwel Sitta hakipo, fikiria mtu anahamasisha mgomo hadi kufikia Mwl Nyerere kutoka Ikulu kwenda Chuo Kikuu na Kumchapa viboko.

Hakuna Mtu alijua kuwahamasisha Watanzania kama Tundu Lissu, lakini uliona walivyom disapoint.

Fikiria kuna kundi la vijana zaidi ya laki 5 wame graduate na hawana ajira, lakini hata kusema waandame kuhamasisha utatuzi wa kilio chao.

Imagine watumishi ambao hawajaongezewa mishahara tangu alipowaongezea JK 2014 lakini hakuna anayetoka kulalamika.

Imagine wanufaika wa bodi ya mikopo walioongezewa riba kutoka 8% ya JK hadi 15% za Magufuli na wamekaa kimya

Imagine wakulima wa Korosho kule kusini walipokopwa Korosho zao na Serikali 2018 lakini hakuna aliyethubutu kupanua kinywa chake kulalamika

Fikiria kikokotoo alichosema kitaanza kutumika 2023, kuna aliyesema chochote

Watanzania wangekuwa wadudu tungesema wanadamu ya Kunguni, unamjua kunguni Mkuu 😀😀

Kwahiyo wakati naandika vile, nawajua Watanzania, ndivyo tulivyo.

Imagine bei za vifaa vya Ujenzi ilivyopanda hadi kujenga tumepunguza alafu hakuna anayelalamika, ndiyo kwanza wanasema tumewaachia kujenga Matajiri.

Ingekuwa Nchi nyingine kitendo cha Tundu Lissu kupigwa zile Risasi Serikali yote ingekuwa imeondolewa madarakani lakini wapi bwana, ndiyo kwanza imeanza kampeni ya kuomba aongezewe miaka mingine 10, ujinga tupu
 
Back
Top Bottom