Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 28,297
- 68,017
Wakuu kwema,
Kuna laki moja hapa nataka nimpe mtu akale na wana wake. Ili uipate nahitaji uniwekee aya, mstari au sura ndani ya Quran au Biblia inayoonesha mke na mume walifungishwa ndoa na kiongozi wao wa dini au walifungishwa ndoa na Mtume, nabii au Kuhani?
Sihitaji Hadithi au andiko lisiloonyesha ninachokizungumza moja kwa moja.
Nimesema nukuu itoke kwenye Biblia au Quran si kwamba siheshimu dini zingine hapana, hivi vitabu ndivyo navifahamu.
Asante.
Huo sio utaratibu. Utaratibu lazima ufuatwe. Haiwezekani kiongozi wa dini yupo. Uamue kufanya huduma bila ruhusa yake. Ukitaka kufanya hivyo fungua dini yako isiokuwa na utaratibu. Kwamba mtu akikurupuka anawezafanya lolote as long as ni muumini.
Utaratibu na uheshiwa liliofungwa duniani (maamuzi) kwa kibali cha Mungu au uongozi wa wa roho wa Bwana linakuwa lishapata kibali kutoka kwa Mungu..
Injili ya Yohana sura ya 2 anzia mstari wa 2.
Yesu alihudhuria sherehe ya harusi kana sasa sijui hoja yako ni ipi.....hiyo harusi aliifungisha nani sasa wewe au😅😅😅
Andiko kama halipo watu wanatumia dini kuwa control watu kama kulikuwa na ulazima mungu angesema
Yesu alikuwa anapenda sana kwenda katika harusi kuna harusi moja alikwenda kama ingekuwa lazima viongozi wa dini kuwafungisha watu ndoa ndio mungu akubali basi siku ile Yesu angefungisha lakini alifanya jambo alilopenda mwenyewe walimuuliza mama ake aliwaambia atakalofanya msikilizeni basi akageuza maji kuwa pombe hapa inaonyesha jamaa kwenye mambo ya pombe yupo poa na itakuwa alikunywa tu
Muhamad alimuoa Khadija mwanamke tajiri kama Leo tunasema zali la mental kwa maana muhamad alikuwa kapuku hana hata hela unaambiwa iyo hela ya mahari katoa khadija je huyo aliefungisha ndoa yake alikuwa sheikh gani?
Ukija kuangalia hayo matukio utakuja kugundua hakuna ya haja ya mchungaji au sheikh au padri au kiongozi yoyote wa dini kuwafungisha watu ndio maana Yesu mwenyewe kaenda katika harusi hakufungisha watu ndoa sana sana kageuza maji kuwa pombe na Muhamad kama mwenyewe kiongozi hajafungishwa na sheikh hakuna ulazima wa sheikh kutaka kufungisha watu ndo nyie wakristo na waislam mumepata wapi huo utaratibu ?
Hujajibu,mbona akili yako inakuwa biased kuwa alichounganisha Mungu wewe unajua kuwa Ni ndoa tu ndio akaunganisha ama mnakuwa manipulated na viongozi wa kusini ili muwe mateka wao mtoe hela ya kufungia ndoa kanisani kwake.Imeandikwa alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.
Sasa hapo mtu asie wa dini anawezafunganisha? Na ni nani alie mkuu katika taasisi za kidini ki Mungu?
Kipaimara huo ni utaratibu wa makanisa 2 kama sijakosea Lutheran na RC na wakati wanaanzisha huo utaratibu Biblia ilishatungwa na kukamilika kitambo,Biblia inasema tu fulani alikuwa mke wa fulani au mume wa fulani taratibu za ndoa hazipo, pia hata taratibu za kipa imara sijui komunio pia hakuna hii kitu, only Jews follow the Bible by 100%
Ila katika vitabu hakuna sasa wachungaji mapadri na masheikh wamepata wapi lazima wao wafungishe ndoaHakuna ulazima wa kufungisha Ndoa Kanisani.
Ndoa ni kwenda Kwa Wazazi wa Binti ukiwa na mshenga wako au Ndugu zako, ukikubali kumchukua Binti. Imeisha hiyo. Hiyo ndoa
Si unajua zinakopatikana. Kasome Biblia Sheikh.Hatuongozwi na maneno ya vijiweni.
Tupe Andiko au sheria zilizopo kwenye Biblia/Torati.
Wewe kama umeamua akili yako iamini hivyo. Mimi siwezi kubadilisha. Mnajitoa ufahamu tu.Hujajibu,mbona akili yako inakuwa biased kuwa alichounganisha Mungu wewe unajua kuwa Ni ndoa tu ndio akaunganisha ama mnakuwa manipulated na viongozi wa kusini ili muwe mateka wao mtoe hela ya kufungia ndoa kanisani kwake.
Sema Sasa alichounganisha pia jikite kabisa kujibu swali alilouliza mleta maada
Sijaamua Ila iko huru,ujibu swali la jamaaWewe kama umeamua akili yako iamini hivyo. Mimi siwezi kubadilisha. Mnajitoa ufahamu tu.
Kwani ndoa zote zinafanyikia kanisani au msikitini? Ama zinafungwa na viongozi wa dini pekee?
Harusi sio ndoa ni shereheInjili ya Yohana sura ya 2 anzia mstari wa 2.
Yesu alihudhuria sherehe ya harusi kana sasa sijui hoja yako ni ipi.....hiyo harusi aliifungisha nani sasa wewe au[emoji28][emoji28][emoji28]
hahahahahaLaki imekuwa ngumu kuchukulika.. Hapa ni mwendo wa siasa tu na kulazimishana kuamini😀😀
Nani tena huyo?Shehe ubwabwa a.k.a shehe ambaye mungu wake alishakufa a.k.a shehe mpenda kupitia barabara za vumbi mmemuuliza?
Acha ujinga ...unataka kutuambia ndoa za wapagani siyo ndoa mbele za mungu mbona yusufu ana kataa kutembea na mke wa boss wake na kusema ni kumkosea mungu .. au amri inayo sema usimtamani hata mke wa jirani yako siyo sahihi hivyo unaweza kumtamani mke wa jirani yako ambao ni wapaganiImeandikwa alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.
Sasa hapo mtu asie wa dini anawezafunganisha? Na ni nani alie mkuu katika taasisi za kidini ki Mungu?
Wameshiba ubwabwa mpaka maandiko wameyasahauNaongeza laki moja mkuu, iwe laki mbili.
Wewe ndio uache ujinga. Sticky to the post.Acha ujinga ...unataka kutuambia ndoa za wapagani siyo ndoa mbele za mungu mbona yusufu ana kataa kutembea na mke wa boss wake na kusema ni kumkosea mungu .. au amri inayo sema usimtamani hata mke wa jirani yako siyo sahihi hivyo unaweza kumtamani mke wa jirani yako ambao ni wapagani