Atakayenionesha andiko linalosema mke na mume walifungishwa ndoa na kiongozi wao wa dini nampa laki 1 akale sikukuu

Atakayenionesha andiko linalosema mke na mume walifungishwa ndoa na kiongozi wao wa dini nampa laki 1 akale sikukuu

Wakuu kwema,

Kuna laki moja hapa nataka nimpe mtu akale na wana wake. Ili uipate nahitaji uniwekee aya, mstari au sura ndani ya Quran au Biblia inayoonesha mke na mume walifungishwa ndoa na kiongozi wao wa dini au walifungishwa ndoa na Mtume, nabii au Kuhani?

Sihitaji Hadithi au andiko lisiloonyesha ninachokizungumza moja kwa moja.
Nimesema nukuu itoke kwenye Biblia au Quran si kwamba siheshimu dini zingine hapana, hivi vitabu ndivyo navifahamu.

Asante.

Sio lazima kufungisha Ndoa Kanisani.

Kufungia ndoa Kanisani ni mbinu ya kudhibiti waumini(Wateja) waendelee kusali hapo ili Watoto wakizaliwa nao wawe Wateja hapo
 
Huo sio utaratibu. Utaratibu lazima ufuatwe. Haiwezekani kiongozi wa dini yupo. Uamue kufanya huduma bila ruhusa yake. Ukitaka kufanya hivyo fungua dini yako isiokuwa na utaratibu. Kwamba mtu akikurupuka anawezafanya lolote as long as ni muumini.
Utaratibu na uheshiwa liliofungwa duniani (maamuzi) kwa kibali cha Mungu au uongozi wa wa roho wa Bwana linakuwa lishapata kibali kutoka kwa Mungu..

Hatuongozwi na maneno ya vijiweni.
Tupe Andiko au sheria zilizopo kwenye Biblia/Torati.
 
Andiko kama halipo watu wanatumia dini kuwa control watu kama kulikuwa na ulazima mungu angesema
Yesu alikuwa anapenda sana kwenda katika harusi kuna harusi moja alikwenda kama ingekuwa lazima viongozi wa dini kuwafungisha watu ndoa ndio mungu akubali basi siku ile Yesu angefungisha lakini alifanya jambo alilopenda mwenyewe walimuuliza mama ake aliwaambia atakalofanya msikilizeni basi akageuza maji kuwa pombe hapa inaonyesha jamaa kwenye mambo ya pombe yupo poa na itakuwa alikunywa tu

Muhamad alimuoa Khadija mwanamke tajiri kama Leo tunasema zali la mental kwa maana muhamad alikuwa kapuku hana hata hela unaambiwa iyo hela ya mahari katoa khadija je huyo aliefungisha ndoa yake alikuwa sheikh gani?

Ukija kuangalia hayo matukio utakuja kugundua hakuna ya haja ya mchungaji au sheikh au padri au kiongozi yoyote wa dini kuwafungisha watu ndio maana Yesu mwenyewe kaenda katika harusi hakufungisha watu ndoa sana sana kageuza maji kuwa pombe na Muhamad kama mwenyewe kiongozi hajafungishwa na sheikh hakuna ulazima wa sheikh kutaka kufungisha watu ndo nyie wakristo na waislam mumepata wapi huo utaratibu ?

Hakuna ulazima wa kufungisha Ndoa Kanisani.

Ndoa ni kwenda Kwa Wazazi wa Binti ukiwa na mshenga wako au Ndugu zako, ukikubali kumchukua Binti. Imeisha hiyo. Hiyo ndoa
 
Imeandikwa alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.
Sasa hapo mtu asie wa dini anawezafunganisha? Na ni nani alie mkuu katika taasisi za kidini ki Mungu?
Hujajibu,mbona akili yako inakuwa biased kuwa alichounganisha Mungu wewe unajua kuwa Ni ndoa tu ndio akaunganisha ama mnakuwa manipulated na viongozi wa kusini ili muwe mateka wao mtoe hela ya kufungia ndoa kanisani kwake.

Sema Sasa alichounganisha pia jikite kabisa kujibu swali alilouliza mleta maada
 
Yaani kitu ambacho watu wengi hawajui Ni kuwa Kuna watu wanataka kuwatawala wengine kupitia nguvu ya jeshi na wengine kupitia neno kujumlisha na hofu kuwa Kuna kifo huko mbinguni,so ili wafuate matakwa yao.

Kila mtu anataka kuwa na misukule itakayofanya wao wanachotaka Ni Nani ambaye hapendi kuwa na watumwa. Huku Kuna vat unalipa kwa lazima ,huku Kuna fungu sijui zaka ulipe 1/10 na unaaahidiwa kuwa ukilipa ndio unajaziwa so hapa unapewa hope tu ndio Imani yako. Cheki mwamposa ,gwajima, mwingira ,kakobe wanavyojikusanyia utajiri kisa Cha upofu wa watu wachache wajinga.


Bana Kuna jamaa alikuwa anahubiri dini akaja kwenye blocks za hostel enzi nikisomea Moscow,Sasa jamaa akapiga neno baadaye akasema kuwa fungeni tusali. Nilimsikia yule mrusi anamuiliza "ZA CHEMU?" yaani ili iweje yule mhubiri akakosa jibu ikawa imetoka ivyo.
 
Biblia inasema tu fulani alikuwa mke wa fulani au mume wa fulani taratibu za ndoa hazipo, pia hata taratibu za kipa imara sijui komunio pia hakuna hii kitu, only Jews follow the Bible by 100%
Kipaimara huo ni utaratibu wa makanisa 2 kama sijakosea Lutheran na RC na wakati wanaanzisha huo utaratibu Biblia ilishatungwa na kukamilika kitambo,
 
Hujajibu,mbona akili yako inakuwa biased kuwa alichounganisha Mungu wewe unajua kuwa Ni ndoa tu ndio akaunganisha ama mnakuwa manipulated na viongozi wa kusini ili muwe mateka wao mtoe hela ya kufungia ndoa kanisani kwake.

Sema Sasa alichounganisha pia jikite kabisa kujibu swali alilouliza mleta maada
Wewe kama umeamua akili yako iamini hivyo. Mimi siwezi kubadilisha. Mnajitoa ufahamu tu.
Kwani ndoa zote zinafanyikia kanisani au msikitini? Ama zinafungwa na viongozi wa dini pekee?
 
Wewe kama umeamua akili yako iamini hivyo. Mimi siwezi kubadilisha. Mnajitoa ufahamu tu.
Kwani ndoa zote zinafanyikia kanisani au msikitini? Ama zinafungwa na viongozi wa dini pekee?
Sijaamua Ila iko huru,ujibu swali la jamaa
 
Ndoa ya kiislamu hufungishwa na walii wa binti, ila kwasababu ya uchache wa elimu ndio utakuta baadhi ya vipengele kama utangulizi na nasaha baada ya ndoa vinasimamiwa na kiongozi wa dini, ila ndoa anafungisha mwenyewe mwenye binti yake au aliyekabidhiwa na wenye binti.

"...basi waoeni kwa idhini ya mawalii wao.."
Quran 4:25

Hapa utaona walii anamwambia bwana harusi nimekuozesha binti yangu fulani kwa mahari mliyokubaliana, na yule bwana harusi anajibu nimekubali kumuoa fulani binti fulani kwa mahari tuliyokubaliana..

Huu ndio utaratibu kwa mujibu wa uislamu.
 
Imeandikwa alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.
Sasa hapo mtu asie wa dini anawezafunganisha? Na ni nani alie mkuu katika taasisi za kidini ki Mungu?
Acha ujinga ...unataka kutuambia ndoa za wapagani siyo ndoa mbele za mungu mbona yusufu ana kataa kutembea na mke wa boss wake na kusema ni kumkosea mungu .. au amri inayo sema usimtamani hata mke wa jirani yako siyo sahihi hivyo unaweza kumtamani mke wa jirani yako ambao ni wapagani
 
Acha ujinga ...unataka kutuambia ndoa za wapagani siyo ndoa mbele za mungu mbona yusufu ana kataa kutembea na mke wa boss wake na kusema ni kumkosea mungu .. au amri inayo sema usimtamani hata mke wa jirani yako siyo sahihi hivyo unaweza kumtamani mke wa jirani yako ambao ni wapagani
Wewe ndio uache ujinga. Sticky to the post.
Kwani op kauuliza kuhusu ndoa za wapagani? Shawn.!
 
Back
Top Bottom