Masterplaner
Senior Member
- Jul 30, 2020
- 121
- 184
Mkuu, siupingi mradi wa Bagamoyo, siupendi kwa ninayosikia yakisemwa kwamba yamo ndani ya mkataba wa ujenzi huo. Kama ni kweli, nitaendelea kuupinga sana.Bandari ya Bagamoyo ita complement ya Dar sio kuiua kwa sababu service sector itapanuka sana na faida yake itakua zaidi hata ya mapato ya bandari yetu kwa mwaka. Embu fikiria makampuni mangapi ya logistics, Bima,ndege,Marine, n.k yatakua pale Bagamoyo huoni yatachochea uchumi na hta kuchochea operation za Air Tanzania/SGR?
Mbunge wa Ilala ameomba muongozo leo Bungeni Dodoma kuhusu mpango wa Serikali kuanzisha mazungumzo tena ya bandari ya Bagamoyo kutokana bandari ya Dar es Salaam kuzidiwa na kutokuwa na uwezo wa kuingiza meli kubwa. Zungu amesema bandari ya Bagamoyo itapelekea kuanzisha viwanda, kuleta ajira na gateway kwa Bagamoyo.
Zungu amesema ulikuwa mpango wa Serikali kuanzisha Industrial Park Bagamoyo lakini wakapata mgogoro wa kimkataba.
Hakuna Jambo limetokea likakubaliwa na wote au kukataliwa na wote,hata ukioneshwa huo mkataba unaweza ukaukubali Mimi nikaukataaSuala la kujenga bandari sio baya, ila waweke mkataba hadharani watu wote wausome kama alivosema Prof Assad.
😊Wewe ulitakaje? Ongeza na mambo mengine mengi aliyofanya ndani ya siku 100
Kama mradi wa Trilioni 20 utashindwa kufikisha maximum capacity kwa miaka 33 basi unapaswa kukimbiwa kama ukiwa. Dar port na madhaifu yake ukiangalia record zake imeweza kufikisha zaidi ya Trilioni 20 miaka 15 tu iliyopita, sasa kwa vipi Bandari ya Bagamoyo ihitaji zaidi ya miaka 33? Tena kwa sifa yake kedekede ya kuingiza mimeli mikubwa ya mizigo!!Sheria ya Ardhi inaruhusu hilo hta wakatoliki maeneo yote walionunua walipewa hizo 99 Years.
Mradi wa trillion 20+ mpaka ufike maximum capacity unadhani miaka 33 inatosha? Ukubwa wa mradi ndio una determine urefu wa umiliki wa ardhi husika kwa uwekezaji.
Kwahiyo tunaweza kupinga mradi ila kuhusu 99 years hiyo sio hoja kabisa.
Tanga na Mtwara mbona zinapanuliwa kitambo tu lakini ujenzi unaenda taratibu sana sababu bajeti ipo stretched sana.Mkuu, siupingi mradi wa Bagamoyo, siupendi kwa ninayosikia yakisemwa kwamba yamo ndani ya mkataba wa ujenzi huo. Kama ni kweli, nitaendelea kuupinga sana.
Nimenukuu hayo maneno yako hapo juu kuhusu manufaa yatakayotokana na mradi huo.
Hivi Tanga na Mtwara haiwezekani nako tukahimiza manufaa haya yawepo? Kuna vizuizi gani!
Mtaji wa Trillion 20 sio mapato usichanganye.... Yaani unasema bandari ya Dar imewekeza mtaji wa trillion 20 ndani ya miaka 15??? Unaweza nipa source ya hiki?Kama mradi wa Trilioni 20 utashindwa kufikisha maximum capacity kwa miaka 33 basi unapaswa kukimbiwa kama ukiwa. Dar port na madhaifu yake ukiangalia record zake imeweza kufikisha zaidi ya Trilioni 20 miaka 15 tu iliyopita, sasa kwa vipi Bandari ya Bagamoyo ihitaji zaidi ya miaka 33? Tena kwa sifa yake kedekede ya kuingiza mimeli mikubwa ya mizigo!!
Kalagabaho
Inaiuaje? Btw ukarabati wa Tanga ushafanyika na Mtwara pia unafanywa kitambo sasa so ni Bagamoyo ndio haina serious investment mind you ilani ya CCM imeahidi hili sio kwamba Bila china kusingekua na port development hapo.
Bandari ya Bagamoyo ita complement ya Dar sio kuiua kwa sababu service sector itapanuka sana na faida yake itakua zaidi hata ya mapato ya bandari yetu kwa mwaka. Embu fikiria makampuni mangapi ya logistics, Bima,ndege,Marine, n.k yatakua pale Bagamoyo huoni yatachochea uchumi na hta kuchochea operation za Air Tanzania/SGR?
No to Bagamoyo Port. Big NO! Bado hamjaweza kueleza kwanini mnafikiri bandari zetu 3 hazifai hivyo tuingie mkataba wa kuwapa watu wajenge bandari mpya ambayo siyo yetu. Magufuli alikuwa na mapungufu mengi sana lakini kwenye hili la bandari alikuwa sahihi mno. Huwezi kuipa nchi ya kigeni lango la kuingia kwenye nchi yako walimiliki. Ni hatari sana. Bandari tulizo nazo zikiboreshwa zitakuwa na manufaa mara milioni moja kuliko hili wazo la kuuza nchi.Mtaji wa Trillion 20 sio mapato usichanganye.... Yaani unasema bandari ya Dar imewekeza mtaji wa trillion 20 ndani ya miaka 15??? Unaweza nipa source ya hiki?
Wakati bado unatafuta source.... Sheria ndio inaruhusu mpaka miaka 99 na kuna wawekezaji wengi tu wanapewa hivyo sasa sielewi kwanini inageuzwa kma ni mara ya kwanza. Nmekueleza hapa hta wakatoliki wame lease ardhi kibao kwa hati za 99 years! Ila sioni mapovu kwamba nchi imeuzwa Vatican? It's really weird.
Mbona hili rahisi kueleweka, kama Trilioni 20 ni uwekezaji mwekezaji anategemea kuzirudisha na hazirudi kama mana toka juu, ni mapato. Sasa unampaje mwekezaji miaka 99 kuendesha mradi wa Bandari kwa kuzingatia mantiki hiyo hapo juu!Mtaji wa Trillion 20 sio mapato usichanganye.... Yaani unasema bandari ya Dar imewekeza mtaji wa trillion 20 ndani ya miaka 15??? Unaweza nipa source ya hiki?
Wakati bado unatafuta source.... Sheria ndio inaruhusu mpaka miaka 99 na kuna wawekezaji wengi tu wanapewa hivyo sasa sielewi kwanini inageuzwa kma ni mara ya kwanza. Nmekueleza hapa hta wakatoliki wame lease ardhi kibao kwa hati za 99 years! Ila sioni mapovu kwamba nchi imeuzwa Vatican? It's really weird.
Je, tulizonazo za mtwara, dar na tanga tumezu-utilize to the max mpk tuanze kuhangaika na bwagamoyo?Uchumi wa Singapore na Malaysia wanategemea bandari mkuu,kwa hiyo bandari ni mojawapo ya vyanzo vya mapato kwa asilimia kubwa vyenye uhakika kwa mwaka
Sasa hapo upigaji wake uko wapi?Mchezo Kama huo aliuufanya pia Manji huko Kigamboni, baada ya kustuliwa na watu wa ndani kuhusu Ujenzi wa Daraja la Kigamboni kupita,yeye Manji akawafuata Wakazi wa pale kwenye mradi na kuwarubuni kununua Viwanja vyao kwa M7 kwa kila mwenye kipande chake Cha Aridhi na kweli wengi walimuuzia maana walikuwa hawajui kuwa mradi tayari unakuja, na wale wachache waliojuwa walitishwa kuwa watanyanganywa Aridhi yao na Serekali,basi kwa haraka haraka nao wakakubali kumuuzia manji, japokua kuna wachache sana wao walichukua pesa kwa Manji na bado wakamkatalia, hao wengi wao walikua Wanajeshi wastaafu,
Sasa Mradi ulivyo kuja tu,ukakuta tajiri Manji ndiyo mmiliki wa eneo lile, Sasa ndiyo ikabidi wakae na Manji awauzie,Sasa hizo bei zilizopigwa hapo! Manji alipiga pesa ndefu sana,na ndiyo maana itachukua muda mrefu sana lile Daraja la Kigamboni kurudisha pesa zote za Mradi!! Matajiri wengi ni Wapigaji!!
Tanga na Mtwara mbona zinapanuliwa kitambo tu lakini ujenzi unaenda taratibu sana sababu bajeti ipo stretched sana.
Sababu kubwa ya Bagamoyo ni muwekezaji ndio ameonyesha opportunity hapo sio kwamba pesa ni yetu tunaweza amua wapi iwekwe. But maadam ni Tanzania hakuna hasara yoyote hta Gesi ipo mtwara but inachakatwa Dar!!
Bagamoyo kwa maoni yangu ipo karibu na social amenities nyingi kwa uwepo wa Dar tu mfano SGR, Airport kubwa, service sector karibu yote imejikita Dar (Bima,logistics etc) so Bagamoyo itakua kma extension tu ya jiji la Dar but kwa Mtwara inabidi mpka lami zijengwe, Airport zitanuliwe, mfumo wa Reli na vitu kibao vianze kujengwa upya so inakuwa disadvantage kwa uwekezaji mkubwa kama huo.