Baada ya Humphrey Polepole kuteuliwa kuwa Mbunge. Je, nani kuchukua nafasi ya Katibu wa Itikadi na Uenezi ndani ya CCM?

Ni wakati sasa wanawake wakapewa nafasi muhimu katika sekretarieti ya CCM, hivyo napendekeza nafasi hiyo safari hii iwaangalie zaidi dada zetu.

Kama vipi yule mwenezi wa CCM Zanzibar apandishwe cheo awe wa taifa ama DC Jokate aliyewahi kuwa Katibu wa uenezi na hamasa UVCCM atatosha kuvaa viatu vya Polepole.

Maendeleo hayana vyama!
 
Nilihisi tu, makonda au Abdallaah Bulembo
 
Pendekezo zuri. You never know mkuu. Anaweza kuwa hata dada yako.
 
Labda Pascal atakumbukwa. Maana anavyojipendekeza siku hizi mpaka imekuwa kero. Anafuata nyayo za yule jamaa yetu wa mkoani Singida aliyejipendeza mpaka akapata uwaziri dakika za mwisho kabla ya bunge kuvunjwa. Yetu masikio na wa kujipendekeza wataanza.
 
Makonda anapewa uenezii subiri uonee
 
Mwanamke atakuwa na ujasiri wa kuratibu wizi wa kura na utekaji wa wagombea wa upinzani wakati wanarudisha NEC fomu za uteuzi? Sifa moja kuu kwenye hiyo nafasi uwe na roho ngumu ikiwezekana kuuua kwa ajili ya ushindi kwa chama😜😜😜
 
Sauti ya zege?!
 
Anarudi mpiga gitaa maarufu kwa jina la bao la mkono!
 
Apewe inginia isack kamwele...
Aliyekuw waziri wa ujenzi na miundombinu
 
Paul Makonda.
Ukisoma nyendo zake za siku za karibuni utaona kuna kitu kinakuja!!
 
Sifikiri kama CCM watataka kuweka mtu ambaye sio smart. HP ni smart hata kama wengine hatumpendi. PM sioni kama ni smart kutosha kuvaa viatu vya HP. Maoni yangu tu.
CCM hamna mtu smart.
CCM akili hazitakiwi kwani hazitumiki.
CCM kikubwa ni kujua wizi/ufisadi, uchawi, unafiki, uongo na kusifu.
 
WanaJf ni lazima tupendane.

Kwa namna mkuu Pascal Mayalla anavyoipigania CCM na kwa taaluma yake ya uandishi wa habari na sheria, ninamuona kama mtu sahihi katika nafasi iliyoachwa wazi na Polepole.

Wanaccm wenye mapenzi mema maoni yenu Tafadhali.

Maendeleo hayana vyama!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…