Baada ya TPA kutangaza tenda kuhusu uwekezaji Terminal 2, Bado mnaamini Bandari zote zimeuzwa?

Baada ya TPA kutangaza tenda kuhusu uwekezaji Terminal 2, Bado mnaamini Bandari zote zimeuzwa?

Kwa wachache tuliobarikiwa kuielewa vizuri nchi hii na jamii yake pamoja na siasa zake tunaposimamia jambo kwa maslahi ya taifa naomba tuheshimiwe na tueleweke vizuri.

Kwa miezi 2 sasa kuna kikundi cha wanasiasa na viongozi wa dini, kwa maslahi binafsi na kutumiwa na watu ambao kila siku wamekuwa wakineemeka kwa michezo yao michafu wanayoifanya kwenye njia zetu kuu za uchumi walianzisha maneno kuwa Bandari zote za Maziwa na Bahari ikiwemo Bandari ya Dar es Salaam zimeuzwa kwa waarabu.

Kikundi hichi cha watu kilisambaza maneno haya nchi nzima huku kikisema kuwa Bunge letu limeshurutishwa na Rais Samia kuuza Bandari zetu na hivyo linauza nchi.

Kwa wachache tunaowajua vizuri tulisema kuwa haya maneno ya hawa watu hayana ukweli wowote ule ila ni hila za watu ambao wamekuwa wakineemeka kwa kuifisadi nchi yetu kupitia Bandari ambao wanatunga maneno ili ku sabotage nia nzuri ya Rais katika kuleta mapinduzi ya kiuchumi kupitia njia zetu kuu za kiuchumi ikiwemo Bandari.

Tuliosimamia ukweli huu na kukataa upotoshaji wa kundi hili la wanasiasa na viongozi wachache wa kidini tuliitwa majina yote eti tumehongwa, mara sisi ni chawa wa Rais Samia.

Kuna mzee mmoja aliwahi kuniambia kuwa, ukweli una tabia moja, unatembea taratibu sana ila uzuri wake ni lazima tu ufike mahali pake.

Baada ya Mamlaka ya Bandari kutoa tangazo la kukaribisha maombi ya uwekezaji katika Terminal 2 ya Bandari yetu ya Dar es Salaam sasa nimeamini rasmi maneno ya yule mzee.

Kilichonifurahisha ni kwamba, baada ya tangazo hili la Bandari, Sijasikia maneno yale ya wale wanasiasa pamoja na wale viongozi wa dini hasa TEC kuwa Rais kauza Bandari ya Dar es Salaam au Bandari zote kwa waarabu!


Wale watu waliokuwa wanasema kuwa Bandari zetu zimeuzwa wameufyata kimyaaaaaa na siwasikii wakisema neno lolote lile zaidi ya kuhamisha magoli saivi wameanza kuzungumzia kampuni ya Adani.

Wale waliokuwa wanasema tumeondoa our National Sovereignty kwa kuwapa Bandari yetu Dubai ndo siwasikii kabisa sasa sijui wamelala usingizi wa pono hawajaona hili tangazo la TPA?

Napenda kumaliza kwa kusema
Tanzania kuna kundi maslahi ambalo limekuwa likinufaika kwa ujinga wa Watanzania. Kundi hili ni zito na lina wanasiasa na watu wa dini pia.

Endapo msiposimama na Serikali kuiunga mkono katika kuleta mapinduzi ya kweli ya kiuchumi, nchi yetu itakuwa maskini hadi ukamilifu wa dahali.

Tumsifu Yesu Kristo!

Nakala kwa
The Boss FaizaFoxy GUSSIE
Usilete mambo ya kijinga kwenye jukwaa tukufu. Hilo tangazo mlilotoa mnafikiri Watanzania ni wajinga? Hiyo kampuni ya Adan Group mliyoipa mktaba kinyemela walikuwa vibarua kusafisha gati?

Mmeuona mziki wa Watanganyika wasiopenda masihala ulivyowachezesha dansi mkaona hili likija kugundulika tutakatwa shingo ndio mnajifanya kutangaza tenda?

Lazima serikali itamke hadharani na kwa maandishi kwamba mkataba na DP World umefutwa ndio Watanganyika wataamini kinyume na hapo hakuna wa kudanganywa tena.
 
Usilete mambo ya kijinga kwenye jukwaa tukufu. Hilo tangazo mlilotoa mnafikiri Watanzania ni wajinga? Hiyo kampuni ya Adan Group mliyoipa mktaba kinyemela walikuwa vibarua kusafisha gati?

Mmeuona mziki wa Watanganyika wasiopenda masihala ulivyowachezesha dansi mkaona hili likija kugundulika tutakatwa shingo ndio mnajifanya kutangaza tenda?

Lazima serikali itamke hadharani na kwa maandishi kwamba mkataba na DP World umefutwa ndio Watanganyika wataamini kinyume na hapo hakuna wa kudanganywa tena.
Umeishia darasa la ngapi? Kama unasubiri mkataba wq DP ufutwe mwambie Mungu akuchukue tu maana nakuhakikoshia haufitwi
 
Mngeendelea kuishupazia shingo TEC na ilivyojipanga ni zaidi ya ccm ya lowasa

Tundulisu mkatolic yule ,pangeiva
 
TPA wanatangaza kumtafuta mwekezaji wakati tayari kuna makubaliano na DPW? Kama makubaliano hayajavunjika, basi wenye dhamana katika nchi hii wanafanya issues muhimu za kitaifa katika kiwango kidogo sana cha kufikiri. Tangazo la kutafuta mbia na yale makubaliano ya IGA yanapikika chungu kimoja?
Fedheha ni kwamba makanisani waraka ulishapelekwa na hivi sasa tunaishi na gharama za kuitengeneza hiyo chuki kati ya serikali na ukatoliki.

Tulilishwa matango pori kwamba mwarabu anataka kuinunua nchi hivyo ule waraka ulikuwa na ujumbe wa siri wa kukataa kuiuza Tanzania kwa mwarabu haswa muislam.

Leo hii tangazo la TPA linamtaka mwekezaji mwenye uwezo ajitokeze na vigezo vyake vitazamwe kama vinakidhi mahitaji ya uendeshaji wa bandari kisasa, tangazo linasema hata wale wazalendo wenye uwezo wa kuendesha bandari kisasa na wao wanaalikwa pia.

Maana yake ni kwamba hata sisi walei wa kawaida tunaosali makanisani tunaalikwa kufanya biashara na serikali yetu kama vigezo vyetu vinatimia!, hii ni aibu kubwa sana ambayo maaskofu pengine kwa kutokujua walichokifanya waliamua kuitafuta wao wenyewe!.
 
TPA wanatangaza kumtafuta mwekezaji wakati tayari kuna makubaliano na DPW? Kama makubaliano hayajavunjika, basi wenye dhamana katika nchi hii wanafanya issues muhimu za kitaifa katika kiwango kidogo sana cha kufikiri. Tangazo la kutafuta mbia na yale makubaliano ya IGA yanapikika chungu kimoja?
Wewe ni mmoja wa wale waliopotoshwa. Mmemuogopa DP World bila ya sababu zozote za msingi. Eneo lake ndani ya JMT ni gati namba tano mpaka namba saba, ambayo ni asilimia nane tu ya eneo lote la bandari la Tanzania.
 
TPA wanatangaza kumtafuta mwekezaji wakati tayari kuna makubaliano na DPW? Kama makubaliano hayajavunjika, basi wenye dhamana katika nchi hii wanafanya issues muhimu za kitaifa katika kiwango kidogo sana cha kufikiri. Tangazo la kutafuta mbia na yale makubaliano ya IGA yanapikika chungu kimoja?
Mantiki ya huu uzi ni kuwapa elimu kuwa hakuna bandari iliyouzwa wala kugawiwa.

Makubaliana ya Tanzania na Dubai yanahusu uwekezaji katika Terminal 1 hasa gati 0-7. Hii ni sehemu ndogo sana ya Bandari ya DSM.

Ndo mana TPA amekaribisha uwekezaji mwingine katika Terminal 2

Waliowaambia sijui hakuna national sovereignty sijui bandari za maziwa na bahari zimegawiwa walikuwa wanawaokota na kuwadanganya vilaza nyie alafu mnapayuka tu
 
Wamesanda kwa wa-TEC.DP WORLD byebye.
 
Inabidi uje na uthibitisho wa kuthibitisha hizo kelele zako kwamba wanaopinga vipengele vya mikataba wamehongwa au wana maslahi binafsi, hilo halibadilishi ukweli kwamba bibi yenu anataka kugawa mali zetu kipumbavu kabisa
 
Kwa wachache tuliobarikiwa kuielewa vizuri nchi hii na jamii yake pamoja na siasa zake tunaposimamia jambo kwa maslahi ya taifa naomba tuheshimiwe na tueleweke vizuri.

Kwa miezi 2 sasa kuna kikundi cha wanasiasa na viongozi wa dini, kwa maslahi binafsi na kutumiwa na watu ambao kila siku wamekuwa wakineemeka kwa michezo yao michafu wanayoifanya kwenye njia zetu kuu za uchumi walianzisha maneno kuwa Bandari zote za Maziwa na Bahari ikiwemo Bandari ya Dar es Salaam zimeuzwa kwa waarabu.

Kikundi hichi cha watu kilisambaza maneno haya nchi nzima huku kikisema kuwa Bunge letu limeshurutishwa na Rais Samia kuuza Bandari zetu na hivyo linauza nchi.

Kwa wachache tunaowajua vizuri tulisema kuwa haya maneno ya hawa watu hayana ukweli wowote ule ila ni hila za watu ambao wamekuwa wakineemeka kwa kuifisadi nchi yetu kupitia Bandari ambao wanatunga maneno ili ku sabotage nia nzuri ya Rais katika kuleta mapinduzi ya kiuchumi kupitia njia zetu kuu za kiuchumi ikiwemo Bandari.

Tuliosimamia ukweli huu na kukataa upotoshaji wa kundi hili la wanasiasa na viongozi wachache wa kidini tuliitwa majina yote eti tumehongwa, mara sisi ni chawa wa Rais Samia.

Kuna mzee mmoja aliwahi kuniambia kuwa, ukweli una tabia moja, unatembea taratibu sana ila uzuri wake ni lazima tu ufike mahali pake.

Baada ya Mamlaka ya Bandari kutoa tangazo la kukaribisha maombi ya uwekezaji katika Terminal 2 ya Bandari yetu ya Dar es Salaam sasa nimeamini rasmi maneno ya yule mzee.

Kilichonifurahisha ni kwamba, baada ya tangazo hili la Bandari, Sijasikia maneno yale ya wale wanasiasa pamoja na wale viongozi wa dini hasa TEC kuwa Rais kauza Bandari ya Dar es Salaam au Bandari zote kwa waarabu!


Wale watu waliokuwa wanasema kuwa Bandari zetu zimeuzwa wameufyata kimyaaaaaa na siwasikii wakisema neno lolote lile zaidi ya kuhamisha magoli saivi wameanza kuzungumzia kampuni ya Adani.

Wale waliokuwa wanasema tumeondoa our National Sovereignty kwa kuwapa Bandari yetu Dubai ndo siwasikii kabisa sasa sijui wamelala usingizi wa pono hawajaona hili tangazo la TPA?

Napenda kumaliza kwa kusema
Tanzania kuna kundi maslahi ambalo limekuwa likinufaika kwa ujinga wa Watanzania. Kundi hili ni zito na lina wanasiasa na watu wa dini pia.

Endapo msiposimama na Serikali kuiunga mkono katika kuleta mapinduzi ya kweli ya kiuchumi, nchi yetu itakuwa maskini hadi ukamilifu wa dahali.

Tumsifu Yesu Kristo!

Nakala kwa
The Boss FaizaFoxy GUSSIE
Kwa kweli nilijua unashusha vitu, kumbe umeandika kwa mapenzi yako.
Watanzania wameelimika miaka hii.
 
Kasome part II ya IGA, kama huna nikupatie, huwa unapoteza muda kuandika ujinga!

Bunge limeshakataa kupokea muswada wa mabadiliko ya sheria ya Maliasili na Ile ya mikataba ya Maliasili, ambayo ililenga kuaccommodate IGA,

Huoni kwamba sauti zimesikika kwamba Kuna uhovyo ulikua unafanyika?
Bado unaamini Rais ameuza bandari zote na bahari, mito na maziwa?
 
Kasome part II ya IGA, kama huna nikupatie, huwa unapoteza muda kuandika ujinga!

Bunge limeshakataa kupokea muswada wa mabadiliko ya sheria ya Maliasili na Ile ya mikataba ya Maliasili, ambayo ililenga kuaccommodate IGA,

Huoni kwamba sauti zimesikika kwamba Kuna uhovyo ulikua unafanyika?
Part 2 ya iga inahusu Terminal 1. Muswada wa Sheria ya Maliasilia hauhusiani na uwekezaji wa Bandari. Shida yako nini?
 
DP World bye bye kivipi?

Kwa ujinga wenu huo hata hamjui kusoma na kuelewa vitu ndo mana hao wanasiasa na maaskofu wanawapelekesha kama makaratasi
Kwahiyo DP world atafanya kazi nchini kinyume Cha sheria zetu? Kwa mujibu wa sheria yetu ya mikataba ya 2017 disputes zitaamuliwa na mahakama zetu, Kwa Mujibu wa IGA, zitaamuliwa Kwa sheria za Uingereza na center of abitration ni SA. Bunge limegoma kupokea mabadiliko ya Sheria ili kuweza kusuit mkataba na DP world. Ama Hilo hujui?
 
Back
Top Bottom