Baada ya TPA kutangaza tenda kuhusu uwekezaji Terminal 2, Bado mnaamini Bandari zote zimeuzwa?

Baada ya TPA kutangaza tenda kuhusu uwekezaji Terminal 2, Bado mnaamini Bandari zote zimeuzwa?

Wewe ndiye unayekariri mistari pasipo kuielewa vizuri, tena unafikia hatua ya kuuleta mkataba humu jukwaani.
1. Tanzania shall inform Dubai of any other opportunities relating to ports

2. Tanzania will inform Dubai of any other opportunities relating to ports

3. Tanzania may inform Dubai of any other opportunities relating to ports

Tutafsilie wanazengo tuelewe utofauti wa verb (Shall, Will na May)
 
Fedheha ni kwamba makanisani waraka ulishapelekwa na hivi sasa tunaishi na gharama za kuitengeneza hiyo chuki kati ya serikali na ukatoliki.

Tulilishwa matango pori kwamba mwarabu anataka kuinunua nchi hivyo ule waraka ulikuwa na ujumbe wa siri wa kukataa kuiuza Tanzania kwa mwarabu haswa muislam.

Leo hii tangazo la TPA linamtaka mwekezaji mwenye uwezo ajitokeze na vigezo vyake vitazamwe kama vinakidhi mahitaji ya uendeshaji wa bandari kisasa, tangazo linasema hata wale wazalendo wenye uwezo wa kuendesha bandari kisasa na wao wanaalikwa pia.

Maana yake ni kwamba hata sisi walei wa kawaida tunaosali makanisani tunaalikwa kufanya biashara na serikali yetu kama vigezo vyetu vinatimia!, hii ni aibu kubwa sana ambayo maaskofu pengine kwa kutokujua walichokifanya waliamua kuitafuta wao wenyewe!.
Inaruhusiwa kuwaza na kuelewa vyovyote inavyotaka iwe kwa mahaba yako,iwe kwa shinikizo au kwa maslahi ama yako ama ya kundi lako ama vyovyote iwavyo,kwa kuwa uko huru.
 
Chawa Lord denning haujawahi hata kuusoma ule mkataba wa IGA, ajabu una kiherehere kila siku kuutetea, uache ule mkataba ujitetee wenyewe.
IGA===Inter Government Agreement.
Whereas all contracts are agreements, not all agreement are contracts. An agreement is therefore, not necessarily a contract
 
DP ilishindanishwa na nani? Na kimsingi tunapinga aina ya mkataba wa kishenzi.

Hii spinning yenu imefeli, tunalikumbusha kanisa katoliki kuwakumbusha maparoko wote waraka uendelee kusomwa kwenye parokia zote kwa wiki tano mfululizo.
Warukeruke wee,ila kurukaruka kwa maharage ndio kuiva kwake.
 
Usikute TPA imekuwa dalali au wakala wa DP World, ya kwamba TPA wanafanya kazi za DP World kwa mlango wa nyuma.Hichi kinachofanyika(TPA kutangaza tenda), huenda ni kiini macho,kupunguza kelele za wanazengo 🤔
 
Sikia, hi hivi sisi hatumtaki DP World? yaani ni hivi ata alete mitambo yake ajue hatafanya kazi kwa amani
Naunga mkono hoja.. Tutamloga kwa mizimu ya kitanganyika hadi apagawe au hamjawahi kusikia greda limeshindwa kuvunja nyumba kupisha barabara........!!???
 
Mnajitahidi kupindua meza[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] waraka ndo umefanya tenda itangazwe unaisi Kila mtu ni mjinga sio kwani iga ilkua inasemaje?
Natamani nikupe hata likes 10. Wanajizima data ila wanajua kinachoendelea
 
Natamani nikupe hata likes 10. Wanajizima data ila wanajua kinachoendelea
Wana sahau watu wanauelewa wanakuja na hoja nyepesi utafikili tec ndo waliingia mkataba wa iga afu wao wamepindua
 
Back
Top Bottom