Baadhi ya Viwanda vya kimkakati alivyoanzisha Mwl. Julius Kambarage Nyerere ambavyo ni magodauni na magofu

Baadhi ya Viwanda vya kimkakati alivyoanzisha Mwl. Julius Kambarage Nyerere ambavyo ni magodauni na magofu

umeleta historia nzuri kwa vizazi vya sasa....wazee wetu walifedheeka sana na kuuwawa kwa viwanda hizi kwa ukosefu wa uzalendo na ubinafsi wa walielimishwa na kuamniwa na taifa hili
Kweli kabisa !!
 
Kabla haujambebesha lawama Mh. Mkapa ni vyema ukaangalia sababu ambazo zilimfanya Mkapa kufikia hatua hiyo.

Iko hivi. Viwanda vingi havikuwa vinajiendesha kwa faida. Serikali ilikuwa ina vipa ruzuku ili viendelee kuwepo. Kuna sababu mbalimbali ambazo zilisababisha haya.
1. Management Mbovu. Wabongo tunajijua. Pamoja na kwamba Nyerere alijitahidi kusomesha watu na kuwapa nafasi..wengi walimuangusha.

2. Technolojia iliyopitwa na wakati. Baadhi ya viwanda alikuwa anapewa msaada...vilikuwa vimeshapitwa na wakati. Kumbe wale jamaa walikuwa wanatafuta sehemu ya kuvitupa. Wao wana move kwenye tech mpya ile ya zamani ndo wanawa wapa au kuwauzia. Hivyo ilikuwa gharama kubwa kuviendesha na havikuwa na ubora kama vya ulaya. Hivyo kufanya kutokuwa na ushindani katika soko. Maana una produce low quality at high cost.

So kipindi cha Mwinyi vingi ya hivyo viwanda vilifungwa. Hali ilikuwa mbaya sana. Watu walikaa nyumbani huku wakiendelea kulipwa mishahara.

Mkapa alipokea nchi ikiwa namna hiyo. Yaani una watu wako nyumbani wanalipwa mishahara. Una viwanda ambavyo havifanyi kazi na technolojia yake imepitwa na wakati.

Je utafanya nini.?

Mkapa aliamua kuvibinafsisha. Kwa sababu ni dhahiri serikali haiwezi kuendesha miradi ya kibiashara. Angali tu kwa mfano Mabasi ya Mwendo kasi, Angalia Tanesco etc..zote zinaendeshwa kwa ruzuku.

Sasa kwa nini uchukue gela ya walipa kodi uvipe viwanda visivyoingiza faida.?

Hivyo Mkapa akaamua kuvibinafsisisha. Ili private investors waendeshe na watoe ajira. Akawapunguza wafanyakazi kwa kuwalipa haki zao ili wasiendelee kula mishahara bila kazi.

Kuna tuhuma kwamba Mkapa aliuza viwanda kwa bei rahisi bei ya kutupa. Ukweli ni kwamba ingawa vilikuwa vinaitwa viwanda...havikuwa viwanda kiuhalisia. Mitambo yake mingi ilikuwa ya kizamani na haifanyi kazi. Hivyo Mkapa aliuza vyuma chakavu na majengo.

Baadhi ya walionunua walifanya vizuri..Viwanda kama TBL vinafanya vizuri hadi sasa. Ila baadhi ya walio nunua walivigeuza ma godown na wao ukiwauliza kwa nini hawakuviendeleza wana sababu zao.
Hakuna sababu yeyote ya maana iliyokuwepo wakati ule !! Ndio maana yeye mwenyewe Mkapa alikiri kwamba kosa kubwa analolijutia zaidi katika utawala wake ni kuvibinafsisha viwanda hivyo !!
 
..kwa kiasi kikubwa viwanda vilikufa kwasababu ya tabia zetu za kijamaa-jamaa ktk kuviendesha.

..Viwanda vingi havikuzingatia kanuni za kibiashara ktk uendeshaji, na menejiment zilikuwa zikiingiliwa kimaamuzi na wanasiasa.

..kwa mfano, vipo viwanda ambavyo vilikuwa javizalishi ktk full capacity, lakini kwasababu ni kiwanda cha umma basi kililazimika kuajiri kana kwamba kinafanya kazi kwa asilimia 100.

..Mtu binafsi anapokuwa na biashara yake huajiri na kupunguza wafanyakazi kulingana na uzalishaji ktk mradi wake.

..Jambo lingine ni viwanda na mashirika kuwa na shughuli nyingi za ziada zisizohusiana na biashara husika. Kila chama kilipotoa tamko fulani viwanda na mashirika yalilazimika kuitikia au kutekeleza.

..Kwa mfano, baada ya chama / Ccm kutoa tamko kuhusu michezo na utamaduni makampuni ya mashirika ya umma yalianzisha timu za mpira, netiboli, bendi za muziki, vikundi vya ngoma, etc.

..Na shughuli zote hizo zilikuwa ni mizigo kwa mashirika na makampuni ya umma.

..Lingine ni mashirika na makampuni ya umma kushindana kutoa ufadhili kwa shughuli za chama/ Ccm. Kwa mfano, mashirika yalikuwa yanashindana kugharamia mkutano mkuu wa chama/Ccm, mkutano wa Nec, etc

..Jambo lingine lililoua viwanda ni URASIMU ktk uendeshaji wake. Kwa mfano kiwanda kilipohitaji kuagiza vipuli nje ya nchi kulikuwa na mlolongo mkubwa wa kiserikali kupata vibali na fedha za kigeni kuagiza toka nje. Mtu binafsi akihitaji kipuli cha kiwanda chake hufanya maamuzi ya haraka.
upo sahihi sana, ilifikia rasimali za viwanda kama magari, matrekta etc yanatumika kijamii zaidi yaani kulima kwenye masham,ba ya wafanyakazi, magari ya umma na dereva kuhudumia familia za mabosi muda wa kazi, viongozi wa mashirika walijilimbikizia mali kifisadi toka hayo SU, ajira za kindugu bila tija wala professional. u-god father ulitawala
 
Mwadui kulikuwa na lami na mabasi yalikuwa yanazunguka bila abiria kulipa nauli.
Kwa walioishi mgodini enzi hizo mgodi wa Mwadui ukiwa Mwadui kweli wanasema maisha yalikuwa kama Ulaya.

Hadi maziwa walikuwa wanaletewa kwenye chupa mlangoni kila siku kama London.
 
Kinachosikitisha sana ni kwamba vimekaliwa na Waasia na matajiri wengine wenye asili ya kiarabu wakitumia kama ma Godown ya kuhifradhia bidhaa wanazoagiza kutoka nje ambazo wala hazifikii ubora wa zile zilizokuwa zinazalishwa na hivyo viwanda. Kwa maksudi kabisa ya kulihujumu Taifa.

Haya mambo yako wazi kabisa, wanasiasa wakiamua kuyafanyia uchunguzi ukweli wote utabainika na hatua stahiki kuweza kuchukuliwa. Hapo ndiyo pale baadhi ya viongozi walijaribu kufahamu nini kilichoko nyuma ya huo uhujumu uchumi, lakini wakaishia kukiri kuwa makaburi mengine ni hatari kuyafukua.

Hapo ikimaanisha kuwa kuna baadhi ya watu hapa nchini ambao wako juu ya sheria na Hawagusiki!
Mwendazake wakati anazindua soko Morogoro alimuumbua Abood,alimwambia umepewa viwanda lakini umekaa navyo kwa miaka 24 na hujafanya lolote,si bora uvirudishe kama umeshindwa.
 
Mkuu Mkapa ndie alieuza NBC ikiwa ndio benki kubwa ya biashara.
Aliuza bank na majengo yake nchi nzima kwa bei ya kutupa,
Fedha kidogo iliyopatikana ndio iliyoanzisha NMB
Baba wa taifa alipinga sana lakini hakuwa na sauti tena, Mkapa allimweka mwenyewe, kibaya zaidi akawauzia makaburu ambao aliwapiga vita muda mrefu
Nasikis kwenye NBC,Mwakyembe alikuwa mmojawapo ya wanabodi,alipinga sana Bank isiuzwe,wakaamua kumtoa nje na kumfukuza
 
Vinaweza kurejea, iwapo watu wenye mitaji (matajiri) watakaa meza moja na wapanga sera.
 
umeleta historia nzuri kwa vizazi vya sasa....wazee wetu walifedheeka sana na kuuwawa kwa viwanda hizi kwa ukosefu wa uzalendo na ubinafsi wa walielimishwa na kuamniwa na taifa hili

..siasa za ujamaa.

..Urasimu wa serikali.

..uzembe wa wafanyakazi waliokuwa wakilindwa na viongozi wa Ccm viwandani na kwenye mashirika.
 
Shinyanga vilikuwepo viwanda vya kusindika pamba na kukamua mafuta vya SHIRECU ! Shinyanga region cooperative union !!

..vilishindwa kuzalisha ndio maana kulikuwa na uhaba wa bidhaa muhimu nchi nzima.

..watu walikuwa wanapanga foleni kwa ajili ya sukari, mafuta, mkate, sembe, mchele, ngano, etc halafu mnasema tulikuwa na viwanda?!

..Na iliwachukua miaka mingi kuuza viwanda na mashirika. Viwanda vingi viliuzwa miaka kadhaa baada ya kusimama uzalishaji au kufungwa.
 
Kabla haujambebesha lawama Mh. Mkapa ni vyema ukaangalia sababu ambazo zilimfanya Mkapa kufikia hatua hiyo.

Iko hivi. Viwanda vingi havikuwa vinajiendesha kwa faida. Serikali ilikuwa ina vipa ruzuku ili viendelee kuwepo. Kuna sababu mbalimbali ambazo zilisababisha haya.
1. Management Mbovu. Wabongo tunajijua. Pamoja na kwamba Nyerere alijitahidi kusomesha watu na kuwapa nafasi..wengi walimuangusha.

2. Technolojia iliyopitwa na wakati. Baadhi ya viwanda alikuwa anapewa msaada...vilikuwa vimeshapitwa na wakati. Kumbe wale jamaa walikuwa wanatafuta sehemu ya kuvitupa. Wao wana move kwenye tech mpya ile ya zamani ndo wanawa wapa au kuwauzia. Hivyo ilikuwa gharama kubwa kuviendesha na havikuwa na ubora kama vya ulaya. Hivyo kufanya kutokuwa na ushindani katika soko. Maana una produce low quality at high cost.

So kipindi cha Mwinyi vingi ya hivyo viwanda vilifungwa. Hali ilikuwa mbaya sana. Watu walikaa nyumbani huku wakiendelea kulipwa mishahara.

Mkapa alipokea nchi ikiwa namna hiyo. Yaani una watu wako nyumbani wanalipwa mishahara. Una viwanda ambavyo havifanyi kazi na technolojia yake imepitwa na wakati.

Je utafanya nini.?

Mkapa aliamua kuvibinafsisha. Kwa sababu ni dhahiri serikali haiwezi kuendesha miradi ya kibiashara. Angali tu kwa mfano Mabasi ya Mwendo kasi, Angalia Tanesco etc..zote zinaendeshwa kwa ruzuku.

Sasa kwa nini uchukue gela ya walipa kodi uvipe viwanda visivyoingiza faida.?

Hivyo Mkapa akaamua kuvibinafsisisha. Ili private investors waendeshe na watoe ajira. Akawapunguza wafanyakazi kwa kuwalipa haki zao ili wasiendelee kula mishahara bila kazi.

Kuna tuhuma kwamba Mkapa aliuza viwanda kwa bei rahisi bei ya kutupa. Ukweli ni kwamba ingawa vilikuwa vinaitwa viwanda...havikuwa viwanda kiuhalisia. Mitambo yake mingi ilikuwa ya kizamani na haifanyi kazi. Hivyo Mkapa aliuza vyuma chakavu na majengo.

Baadhi ya walionunua walifanya vizuri..Viwanda kama TBL vinafanya vizuri hadi sasa. Ila baadhi ya walio nunua walivigeuza ma godown na wao ukiwauliza kwa nini hawakuviendeleza wana sababu zao.
Hizi ni sababu za kuhalalisha hayo Angejenga discipline na uwajibikaji visingesimama?
 
Nimesema vingine vilikuwa na matatizo ya uongozi (Management), Vingine Technolojia na vingine yote mawili.

Ndo maana vipo ambavyo waliovinunua waliviendeleza kwa faida.

Vingine waling'oa vyuma chakavu wakabaki na magodown.

Hii ya kupeleka mitambo na mashine nje sina reference yoyote..hivyo siwezi kubiasha au kukataa. Lakini all in all watakuwa wameangalia mazingira ya biashara..maana at the end mwekezani anataka faida
Hapo ndipo kuna makosa makubwa kimtazamo wa sababu ya kuviuza, haikuwa eti ni kumnufaisha mnunuzi tu. Ni ili mnunuzi ahakikishe anavirekebisha viweze kuanza kuzalisha kwa manufaa ya Taifa, haswa kiteknologia. Sasa unapouza kiwanda cha serikali halafu hakuna kipengele kama hicho cha kuhakikisha kinabakia kuwa na manufaa kwa Taifa, then huo ni ubadhirifu wa mali ya umma.
Kitu kingine cha kuzingatia ni kwamba serikali yake ilitakiwa ijenge vipya vilivyo bora zaidi ndipo waviuze hivyo vilivyoundwa na Mwalimu, ili aonyeshe umahiri wake. Kama baba yako amejenga nyumba kwenye kiwanja cha familia ukaona si nzuri kipindi cha utu uzima wako, unatakiwa ujenge ya kwako iliyo bora zaidi na siyo kuibomoa aliyojenga Baba yako.
Leo hii ukiuliza fedha iliyopatikana kwa kuuza hivyo viwanda vyoote zimelinufaisha je Taifa kiuchumi haielezeki hata kidogo. Nina wasiwasi Mwalimu Nyerere alipata msongo wa mawazo kutokana na maamuzi haya ambao huenda ndiyo uliosababisha kifo chake. Hotuba ya Mwalimu Nyerere wakati wa kumteua inatosha kuthibisha hilo, it is beyond any reasonable doubt kwamba hili lilisababisha maumivu kwa Baba wa Taifa.
Ilikuwa ni muhimu maamuzi haya kujadiliwa kwa kina hata na Bunge. Vyuo vikuu tulikuwa navyo vilitakiwa vishirikishwe kufanya research ya nini kifanyike, vyuo kama UDSM, DIT, Arusha Tech, Sokoine University, Mzumbe, Chuo Cha Biashara DSM nk. walitakiwa wataalamu wapitie mkakati huo na kutoa ushauri. Unapokuwa kiongozi usiependa kushauriwa na unaishia kufanya maamuzi ya kubomoa uchumi wa nchi kiasi hicho, basi uwe tayari kushitakiwa kwa kosa la ufisadi na ubadhirifu wa mali za umma.
Kuna mtu amesema eti Baraza la Mawaziri halihusiki moja kwa moja kutokana na mfumo wetu. Kwanini basi hakuna hata mmoja wao aliyejiuzulu ili kujitoa kwenye huo ubadhirifu? Ina maana maadili ya uongozi hakuna.
Kitendo hicho kililirudisha Taifa miaka 40 nyuma kiuchumi.
 
Hapo ndipo kuna makosa makubwa kimtazamo wa sababu ya kuviuza, haikuwa eti ni kumnufaisha mnunuzi tu. Ni ili mnunuzi ahakikishe anavirekebisha viweze kuanza kuzalisha kwa manufaa ya Taifa, haswa kiteknologia. Sasa unapouza kiwanda cha serikali halafu hakuna kipengele kama hicho cha kuhakikisha kinabakia kuwa na manufaa kwa Taifa, then huo ni ubadhirifu wa mali ya umma.
Kitu kingine cha kuzingatia ni kwamba serikali yake ilitakiwa ijenge vipya vilivyo bora zaidi ndipo waviuze hivyo vilivyoundwa na Mwalimu, ili aonyeshe umahiri wake. Kama baba yako amejenga nyumba kwenye kiwanja cha familia ukaona si nzuri kipindi cha utu uzima wako, unatakiwa ujenge ya kwako iliyo bora zaidi na siyo kuibomoa aliyojenga Baba yako.
Leo hii ukiuliza fedha iliyopatikana kwa kuuza hivyo viwanda vyoote zimelinufaisha je Taifa kiuchumi haielezeki hata kidogo. Nina wasiwasi Mwalimu Nyerere alipata msongo wa mawazo kutokana na maamuzi haya ambao huenda ndiyo uliosababisha kifo chake. Hotuba ya Mwalimu Nyerere wakati wa kumteua inatosha kuthibisha hilo, it is beyond any reasonable doubt kwamba hili lilisababisha maumivu kwa Baba wa Taifa.
Ilikuwa ni muhimu maamuzi haya kujadiliwa kwa kina hata na Bunge. Vyuo vikuu tulikuwa navyo vilitakiwa vishirikishwe kufanya research ya nini kifanyike, vyuo kama UDSM, DIT, Arusha Tech, Sokoine University, Mzumbe, Chuo Cha Biashara DSM nk. walitakiwa wataalamu wapitie mkakati huo na kutoa ushauri. Unapokuwa kiongozi usiependa kushauriwa na unaishia kufanya maamuzi ya kubomoa uchumi wa nchi kiasi hicho, basi uwe tayari kushitakiwa kwa kosa la ufisadi na ubadhirifu wa mali za umma.
Kuna mtu amesema eti Baraza la Mawaziri halihusiki moja kwa moja kutokana na mfumo wetu. Kwanini basi hakuna hata mmoja wao aliyejiuzulu ili kujitoa kwenye huo ubadhirifu? Ina maana maadili ya uongozi hakuna.
Kitendo hicho kililirudisha Taifa miaka 40 nyuma kiuchumi.

..serikali ya Raisi Mkapa ilikuwa haina fedha za kutoa huduma muhimu za jamii kama elimu, afya, etc sembuse kujenga viwanda vipya.

..Kulikuwa na ukata mkubwa wa fedha uliotokana na makusanyo madogo ya mapato ya serikali, pamoja na mzigo mkubwa wa madeni ya ndani na nje.

..Zaidi ya matatizo niliyoyaeleza hapo juu kulikuwa na tatizo la mzigo wa gharama za kuhudumia viwanda na mashirika ya umma ambayo yalikuwa hayawezi kujiendesha.

..Katika mazingira kama hayo nadhani sio sahihi kuilaumu serikali ya Raisi Mkapa kwa kutokujenga viwanda vipya, au kuvifufua vile vilivyokufa wakati wa awamu ya 1 na ya 2.
 
..serikali ya Raisi Mkapa ilikuwa haina fedha za kutoa huduma muhimu za jamii kama elimu, afya, etc sembuse kujenga viwanda vipya.

..Kulikuwa na ukata mkubwa wa fedha uliotokana na makusanyo madogo ya mapato ya serikali, pamoja na mzigo mkubwa wa madeni ya ndani na nje.

..Zaidi ya matatizo niliyoyaeleza hapo juu kulikuwa na tatizo la mzigo wa gharama za kuhudumia viwanda na mashirika ya umma ambayo yalikuwa hayawezi kujiendesha.

..Katika mazingira kama hayo nadhani sio sahihi kuilaumu serikali ya Raisi Mkapa kwa kutokujenga viwanda vipya, au kuvifufua vile vilivyokufa wakati wa awamu ya 1 na ya 2.
Hiyo siyo sababu ya kuua na kuuza viwanda vyoote hivyo. Wapi uliona upembuzi yakinifu uliotumika kufikia uamuzi huo? Huwezi kuamua kuua viwanda na mashirika mengi namna hiyo. Kwanini asitembee kutafuta ushauri wa kitaalam hata nchi za nje? Kwa nchi ni afadhali ku-negotiate mikopo yenye masharti nafuu kuliko kuzima uchumi wa nchi nzima. Unatetea nini Mkuu wakati yeye mwenyewe alifika mahali akakiri hadhani kuwa alifanya makosa? Ila inakubidi ukumbuke kuwa wakati anakiri hilo alikwisha kuwaita waliopinga maamuzi yake jina baya "Makanjanja" . Hakuna kitu kibaya kama ulevi wa madaraka.
 
Ni kweli kabisa. Mwalimu alijitahidi sana.. hata kama viwanda alivyopewa/uziwa vilikuwa tayari vimepitwa na wakati. Laiti kama Mwalimu angelijuwa kuwa alikuwa anaongoza watu wa aina gani, angeamua tu kula bata kama Mobutu

Mosi.. watz wa nyakati zile, kama walivyo wa sasa hawakuwa watu wa kupiga kazi.. walijaa uvivu tuuu, kulalamika na uzembe. Ili viwanda visonge mbele na kuzalisha faida, ilitakiwa mali ghafi. Katika sekta ya uzalishaji mali ghafi, mambo yaliharibika pindi mkoloni alipoondoka hususa baada ya Azimio la Arusha, 1967. Watz wakiwa na jembe la mkono huko mashambani na wengine wakiwa na elimu duni katika masuala mazima ya uchumi ea viwanda, hakuna cha maana ambacho kingefanýika. Ni uvivu kwa kwenda mbelee..
Baadaye ghafla chama kikashika hatam.. balaa la uharibifu likapanuka.. meneja wa kiwana cha Bucop anapewa amri ya kutoa milioni 30 kugharamia safari ya Kawawa mkoani Kagera, bila vielelezo wala nyaraka stahiki.. naye meneja anajiongezea zake milioni 5.. na kila mahala ilikuwa hivyo..
Kwa muktadha huo, uongozi wa wakati ule unapswa kulaumiwa sehemu kwa kushindwa kufuata miiko ya kiviwanda..
Ikawaje Waasia na waarabu wakavigeuza magodown? Ni uozo tu katika nchi.. Mh Ben (RIP) anarithi mahame/mapango wananchi waliopigika kisawa sawa.. wenye kaunafuu ni wahindi kwa vile wana uwezo wa kupata vijimikopo kutoka India.. ndo ikawa hivyo..

Kazi sana kuendeleza nchi ambako watu wake hawapendi kazi.. wanapenda kula kuliko kazi..
 
Back
Top Bottom