Baba mzazi wa Askari Polisi anayedaiwa kujinyonga Mtwara adai kutoridhishwa na taarifa ya mwanae kujiua

Baba mzazi wa Askari Polisi anayedaiwa kujinyonga Mtwara adai kutoridhishwa na taarifa ya mwanae kujiua

Yaani mtu anakutuma kwenda kumuua mtu asiye na hatia na ww unaenda!!!!!
Hata kama mtu ni boss wako ndio akupe tu maagizo ya kipumbavu na ww unatii hata bila kufikiria mara mbili?!!!
Vilaza
Unadhani unavyotumwa utaambiwa hana hatia, si wanakwambia tu huyo ni jambazi sugu la kutumia silaha. Na wewe utaenda kuua kwa confidence ukidhani ni jambazi kweli
 
Hawa mbwa wanaoua raia wasio na hatia dawa yao ndogo sana.

Kama unajijua huna Nguvu za kupambana nao, kiserikali ama kifedha dawa ni moja tu.

Chukuwa nauli waendee kwa wazee, hakuna kupoteza muda, yaan watasambaratika kwanzia Master plan wa mchongo, mpaka machawa wao wote wa mpango haramu.

Muda mwngine hatuitaji kupoteza muda kujibizana na haya mashetan watu.
Asante mkuu[emoji24][emoji24]wkt mwingine inabidi kufanya visivyowezekana hawa matahira wanaboa Sana!!
 
Of course, hata kama ametumwa na wakubwa kuua, hilo bado lilikuwa ni kosa kwake, hautakiwi kuitii amri inayoenda kinyume na sheria. Cha kujiuliza? alijinyonganyongaje mahabusu, tena mahabusu ya polisi?

Tunazijua mahabusu ya polisi, wenzake walikuwa wapi? Alikuwa peke yake? Kwa jinsi zilivyojenga huwa hazionyeshi kama mtu anaweza kufanikiwa kupanda na kutundika nguo au kamba ajinyonge pale mahabusu. Ni ngumu.

Watueleze wazi tu, nani amemuua pale mahabusu ili kuficha ukweli wa hao wakubwa. Sisi tulitaka awe hai ili aende mbele ya mahakama asulubishwe kisheria, na pengine angefichua mengine mengi tu ya hao wakubwa. Tume iundwe, isipoundwa nakwambia hizo tabia zitaendelea kuwepo huko polisi.
 
Kama alitumwa kuuwa na akakubali huo ni upumbavu wake.
Kwani angegoma angefukuzwa Kazi?
Angeweza kupigwa risasi mzee. Ukiwa kwenye group la waovu wakajua wamepanga njama ya ajabu kama hiyo na wewe umekataa, that means unajua njama yao, huwa wanapoteza ushahidi kwa namna yeyote ile. Unatakiwa kuishi kwa hekima, utakuja kubugizwa risasi wakati ungepona.

Kama hujui hilo uliza wauza unga, wanajua unawafahamu wameleta unga, na hawana imani na wewe kama hauwezi kuwatolea siri, lazima walipe hata hela utolewe roho.

Sasa kama wakubwa zake walishatoa amri kikundi hicho kikafanye hivyo (kama ni kweli), wanajua jamaa anajua, na pengine ana misimamo ya ajabu, na pengine walipowakamata akatishia kuwa wamuachie la sivyo anaenda kusema ukweli, unategemea nini?
 
Nasema kutoka moyoni, sipendi hawa jamaa mapoti.. mapoti kuanzia mkoa wa Pwani, na huku Lindi sijui Mtwara..hao ni balaa mbele ya michongo ya fedhwa baba..wanakutoa upepo tu..wale wa Moshi na Arusha nadhani siku hizi wametulia ukiachana na wale wa genge la Sabaya
 
Akiongea na Azam News, Baba mzazi wa askari aliyejinyonga anasema hajaridhishwa na taarifa za kifo cha mwanae!

Anasema alipigiwa simu na kuambiwa mwanao tumpeleke akazikwe wapi? Akawaambia mleteni nyumbani kwangu Tabata, Dar Ea Salaam.
...
Kumekucha
 
Askari wamekuwa kivuli cha uhalifu na uporaji, hawana tofauti na raia waovu tu!!
 
Wamemuuwa polisi wenzake kwenye ili kupindisha kesi, safari hii jamuhuri isifanye uzembe wa Kama kesi ya zombe ambapo kwa kujua kesi itakavyokuwa walimtorosha SADI aliyeamuliwakupiga risasi wafanyabiashara na kupora pesa...
Huyo askari aliejinyonga, nae si ni boss? ACP si ni cheo kikubwa tu, nani anaweza ku comand aue ? Sio kwamba yeye ndo aliplan mchongo wote, so kaamua kujiondoa?
 
Hawa ndio polisi wetu.........mara nyingi polisi wetu ni wale walishindwa maisha.....so pale ndio kimbilio..... anaingia akiwa na tabia zile alizokuwa nazo......legelege, akili fupi...ubabe wa kijinga......haya ndio matokeo......baba mwanajeshi alifanya MCHONGO mwanae akaingia upolisi......keshampoteza mwana na aibu......
 
Utakuwa mchawi.Baba ana haki ya kujuwa ukweli kuhusu kifo cha mwanae

Sent from my Infinix PR652B using JamiiForums mobile app
Yule mdingi kwanza yeye ni mwanajeshi mstaafu. inasikitisha kuona mazingira aliyopo na alikuwa mwanajeshi. Kuna haja hivi vyombo viongezewe mishahara. Nikija kwenye hoja, mtoto ni mtoto ndugu, hata huyu jamaa naye ana watoto, baba anampenda mwanae, ameacha mke na wajukuu, na huwezi kujua mazingira ya huyo askari hadi anafanya tukio....hapo analia vilio viwili, cha kwanza cha mtoto wake kutia nuksi familia, cha pili kumpoteza mtoto uliyemzaa na kumlea hadi kufikia umri ule, cha tatu anaisikitikia familia ya wafiwa upande wa pili. Huyo mdingi yupo kwenye wekati mgumu sana.
 
Lakini hata kesi ya Zombe na wenzake baada ya tume kuundwa na kutoa majibu kuhusu ukweli, tatizo likaja kwenye uandishi wa mashitaka!

Mtu wa taaluma hiyo alipokwisha kulambishwa mlungula akajifanya mamuma wa taaluma, akaandika kesi miguu juu kichwa chini, hali iliyofanya Zombe akaonekana ni muungwana, afisa mpole na hajashiriki kabisa kwenye mauaji hayo na kuachiwa huru kula pensheni na hewa tulivu ya uraiani!

Na hata sasa nasikia harufu ya mambo hayo kujirudia ingawa Makamo kafoka sana hadi povu limemtoka kumshurutisha Igp aingilie kadhia ya mauaji yanayoendelea kote nchini, lakini mwisho wa jambo hili tusitarajie lolote la maana.
We subiri siku saba ziishe uone? Kuna watu watamwaga unga
 
Wamemuuwa polisi wenzake kwenye ili kupindisha kesi, safari hii jamuhuri isifanye uzembe wa Kama kesi ya zombe ambapo kwa kujua kesi itakavyokuwa walimtorosha SADI aliyeamuliwakupiga...
Kwel wakimaliza rais watarudi kwa viongozi mama awe makini sana
 
Back
Top Bottom