Bado Km 51 ili Kigoma-Dar iwe lami. Rais Samia anaenda kuunganisha mikoa yote kwa lami

Wewe taktaka hizo km zinajengwa wapi?

Njoo hapa ukonga uone kulivyochakaa
Ukonga ndio Mkoani ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

Zinajengwa kila Mkoa wa Tanzania ikiwemo huko Dar sio lazima iwe hapo Ukonga.
 
Hakuna Cha uchwara ni facts tuu hata kama hutaki.Zinamalizika mwaka Hadi mwaka ndio maana ya takwimu.

Na Kwa taarifa Yako kama mama atajaaliwa Hadi kufika 2030 hakuna Kipande Cha Barabara kuu Tanzania hii litakuwa na vumbi ,kote itakuwa ni mkeka.
We uvccm ni shida sana.
 

Wabunge wa hiyo mikoa wamekuwa na kazi gani?
 
Na mwalimu wangu kutoka Pale TIA Dar, alishaanzisha Branch nyingine ya TIA hapo Kigoma tangu mwaka 2010 au 2011
Ukifika maeneno kama ya Mwakizega, unakuta watu wapo kijijini wanaishi kwenye Beach nzuri mno kando kando ya Ziwa Tanganyika, utadhani wako Ulaya
Kigoma ni kuzuri mno nilipapenda sana. Hatuwezi kuwa tuna-rate uzuri wa sehemu kwa kutumia uwingi wa maghrorofa yaliyopo mjini.

Huu mkoa Mungu bariki ngoja Mama aufungue halafu utaupaisha uchumi wa nchi yetu kwa kasi isiyotarajiwa; ni hakika
 
Wewe ukipata gepu piga mzee baba,hakuna kiongozi mwenye huruma na wewe mwananchi.
 
MBONA MIKOA MINGI TU. Manyara na Simiyu haijaunganishwa kwa Lami, Arusha na Simiyu haijaunganishwa na Lami, Manyara na Tanga bado, Morogoro na Ruvuma n.k
Bora Kwa Sasa Morogoro na Ruvuma Ina mkandarasi wa EPC

Manyara,Simiyu,Tanga Ina mkandarasi wa EPC +F
 
Mimi nimeishi Kigoma.Hapo naona unapiga propaganda tu.Unaweza kumulaumu JPM kwa mambo mengine lakini siyo kwa jitihada za kuboresha miundombinu ya barabara.
Hakuna kiongozi aliye boresha miundo mbinu ndani ya nchi hii kuanzia barabara ,vyanzo vya umeme , Elimu kumzidi kikwete hayo mengine ni propaganda.
 
Kazilambwa-Chagu ilikuwa na lami? Unajua kwamba Hadi anachukua kutoka Kwa JK ni km hizo hizo zilikuwa mavumbi na zilimshinda Kumalizia?
Tuambie kwa wakati wake alikuta kiasi gani na akajenga kiasi gani ila ukileta porojo wakati fika tunajua utendaji wake, utaonekana kituko tu.
 
Barabara zote zilizo jegwa kipindi JPM ni waziri wa ujenzi sifa zina takiwa kwenda kwa kikwete kwa sababu ndo alikuwa rais kipindi hicho.
 
Umeandika pumba na mashudu

Halafu JPM bado anawasumbua sana eeh vichwani mwenu hawatoki๐Ÿ˜alijua kuwakomesha mpaka mnashindwa kumsahau
 
Tuambie kwa wakati wake alikuta kiasi gani na akajenga kiasi gani ila ukileta porojo wakati fika tunajua utendaji wake, utaonekana kituko tu.
Amejenga chini ya km 2500,taarifa hii utaikuta Kwenye Bunge la kufunga Bajeti
 
Hakuna kiongozi aliye boresha miundo mbinu ndani ya nchi hii kuanzia barabara ,vyanzo vya umeme , Elimu kumzidi kikwete hayo mengine ni propaganda.
Samia atafunika wote hao, wengine walikuwa wapiga propaganda
 
Punguza uchawa. Magufuli ndo baba wa taifa katika eneo la ujenzi wa Barabara nchi hii.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ