Ifike mahala sisi kama Taifa tujielewe nini tunataka.
Tunafuata mila na desturi zetu ama tunaflow na mabadiliko ya kiduni.

Sielewi Zanzibar wanafuata kipi.
 
Serikali ya mapinduzi ya zanzibar imetangaza adhabu ya zaidi ya dola 400 za kimarekani au kifungo cha miezi sita kwa wanaume wote wanao suka. Msemaji wa serikali ya SMZ ameeleza kuwa kusuka sio utamaduni wa zanzibar wala dini.
Haya ni ya huko zanzibar vipi kwenu umofia?

 
Kwa hiyo akina nasib na rajabu hawataruhusiwa kukanyaga zanzibar wakiwa wamesuka. Kusuka kwao mwisho kimbiji
 
Aisee..
Huyo Dr Omar awekewe ulinzi upesi
 
"... sio utamaduni wetu ...". Waunde kabisa wizara inayoshughulikia masaala ya dhambi kama kulee ili pia wasaidie kukamata wasiofunika vichwa vyao sawa sawa!

Kwa mara ya kwanza nakuona ukiunga mkono maana wewe ni mtu wa kupinga tuu kwa waislamu, Uislamu unakaza huo ujinga wa mwanaume kujibadilisha kuwa mwanamke na mwanamke kuwa mwanaume n.k, achana na utamaduni tu, wewe ulishaona nchi za kiislamu wanafanya huo ujinga wa kusuka minywele isipokua nchi za wazungu na Afrika!!

Tena wanakosea sana kuomba kibali, wanatakiwa kupigwa marufuku mazima, akionekana mtu anafanya huo ujinga apigwe para la nguvu na iwe fundisho kwa wengine


Bhujiku ng'waka nkoi
 
Chanzo kipya cha mapato ? Kwann wasipige marufuku tu ,bila kulipa kibali
 
Mngejiondoa na kwenye Muungano wa kikafir ingependeza zaidi …
 
Katibu Mtendaji Baraza la sanaa, Sensa ya Filamu na Utamaduni, Dkt.Omar Adam leo kwenye Asubuhi Njema ya ZBC ameelezea mengi yanayohusu sekta ya sanaa, filamu na namna wanavyosimamia Mila, Desturi na Utamaduni wa Zanzibar.
Kumbe kwa wanaume kusuka sio shida uwe na hela tu. Waislamu bwana!
 
"... sio utamaduni wetu ...". Waunde kabisa wizara inayoshughulikia masaala ya dhambi kama kulee ili pia wasaidie kukamata wasiofunika vichwa vyao sawa sawa!
Islamic State (IS)
 
Serikali ya Zanzibar imesema ni kosa kisheria mwanaume kuingia au kuishi viziwani Zanzibar akiwa amesuka nywele.

''Kwa mujibu wa sheria zetu ukikutwa utatozwa faini ya milioni moja za kitanzania ambayo ni zaidi ya dola 400 za kimarekani au kufungwa jela miezi sita au adhabu zote kwa pamoja,” imeeleza Serikali ya Zanzibar.

Akizungumza na BBC, Katibu Mtendaji Baraza la Sanaa, Sensa ya Filamu na Utamaduni Zanzibar, Dkt Omar Adam amesema serikali kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi imeanza operesheni ya kukamata wanaume wote waliosuka nywele ikiwa ni utekelezaji wa sheria inayokataza wanaume kusuka nywele ili kulinda maadili na tamaduni za Zanzibar.

Dkt Omar amesema vijana wengi visiwani humo wamekuwa na hulka ya kusuka nywele kinyume na taratibu za wazanzibar.

Alisema,” Sifahamu kama kuna mzee yoyote hapa Zanzibar ambaye atamchukua mwanae wa kiume halafu ampeleke saluni kusuka nywele. Huu si utamaduni wa Zanzibar na sisi kama wasimamia sheria lazima tuzuie hili.”

SOURCE: BBC SWAHILI
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…