Bavicha kwenda uwanja wa Mkapa huku mmevalia rangi nyekundu ni wazi kuwa mliwabagua Yanga, kwa mantiki hii mnadhihirisha CHADEMA ni wabaguzi

Hakuna mtihani mgumu kama kukaa jukwaa la Simba wakati wewe ni Yanga. Inabidi uwe na mtu wa kukumonitor kila wakati. Hapa Simba walikuwa 3 na Yanga tulikuwa 3. Kikubwa tulikuwa na special mission ya kupeleka Agenda ya #KatibaMpya kwa Mkapa. Tuliingia kwa Shangwe kama lote


 
Kwa nini msivae rangi nyeupe? Hii ni wazi kuwa hata kura za wanaYanga hamzitaki huko mbeleni.View attachment 2041065

Ni kuwaza kwa kasi ya 4G tu, kwani NYEUPE haina timu??

Hii ni kuendekeza mawazo mfilisi, unashindwa kutumia rangi nzuri kwa sababu ya mawazo mfu.

Ungetafuta rangi ambayo haina affiliation na kitu chochote Tanzania hii,
iwe mpira au chama cha siasa lakini nyeupe bado uko kulekule.

Jitahidi kuwaza kwa kutulia na ukitafakari vyema kwanza.
 
Post zote mbili ni za mtu mmoja! JF imetoka kwenye GT's na kuwa ya vibaka.
Walioweka mabango ya Samia hawakuwabagua wasio wanaccm?
 
Ulishaona wanaCcm wanavaa kijani na njano siku ya kariakoo derby? Tumia akili we pimbi

Acha derby, wanavaa hata kwenye misiba ina maana huwatenga wafiwa? Au huwa mnawauliza waliofiwa ni chama gani?

Jiulize, je kuna siku sare za chama cha CCM zilivaliwa siku isiyo ya shughuli za kichama? Ukipata jibu nijulishe. Tuache mihemuko isiyo tija.
 
Achana na Bavicha, habari ya mjini ni Polepole kwa sasa.
 
Nyie maUVCCM mkiwa mnavaa yale makanga yenu ya manjano huwa mnawatenga mashabiki wa simba???
 
Mimi siwezi kuangalia mpira nikawa na sura hiyo na mikono imetulia hivyo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…