Tatizo ni hao wanaojidai kumtoa mapepo na hawana uwezo huo
Wachungaji sio Waganga wa Kienyeji.....! Wala Mungu hafanyi kazi Kwa namna ya Kibinadamu...!
Yesu alipokua akiponya Watu... aliwaambia nenda ila USITENDE DHAMBI TENA...!
Sijui kama unaelewa maana ya maneno hayo, na Biblia inasema Mapepo yanapomtoka Mtu, huenda kutangatanga na yakikosa pa Kukaa, hujaribu kurudi kwa Mtu yule yule, yakikuta Mtu yupo Msafi hayawezi kuingia Tena, ila yakikuta Mtu Yuko mchafu, yanaiingia yakiwa na Nguvu mara 7.
Kanuni za Mungu zipo wazi Ndugu, Sasa unakuta Mtu ana Mapepo kaombewa Mapepo yameondoka, anarudi kwake, kumbe anaishi na Mwanaume hajafunga nae Ndoa, ama anaishi na Mwanamke hajafunga nae Ndoa, means anaendelea kuzini, ama hajaacha njia zake Mbaya ambazo zilipelekea tatizo lake... Mapepo hayataondoka...
Mafuta ya Upako hayatakusaidia, Keki ya Upako haitakusaidia.
Kitu pekee kitachokusaidia ni kuamua kuishi Maisha safi ya kumpendeza Mungu ama Kwa Lugha nyingine Maisha Matakatifu...!
Tena ukiamua kuishi Maisha Matakatifu Huna haja kupoteza muda kuombewa, hayo Mapepo yataondoka yenyewe haraka Sana (Mimi ni Shahidi)
Tatizo letu Binadamu tunataka Mungu atufungue na akishafanya hivyo tunataka kuendelea na Maisha yetu ya zamani, Starehe, Ngono, Na Dhambi zingine Mbaya...!
Always huwashauri Watu, kama Kuna Watu wanatakiwa kuamua kumgeukia Mungu Moja Kwa Moja ni Watu wenye Mapepo na Majini Mahaba....! Na ipo sababu Kwa Nini baadhi ya Watu husumbuliwa na hizo Spirit, na siku wakijua Sababu.... WANGEACHANA NA UCHAFU WA HII DUNIA NA KUMTEGEMEA MUNGU.
Tatizo ni hao wanaojidai kumtoa mapepo na hawana uwezo huo